Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa wa Morogoro, Ahamed Msangi ( kushoto) akiwaongoza baadhi ya askari na wananchi katika ujenzi wa mahema kwa ajili ya kuishi watu waliokubwa na mafuriko na nyumba zao kibomolewa na mafuriko hayo , kwenye shule ya Msingi Mazinyungu ya Mjini Kilosa. Picha zote na mdau John Nditi
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Magomeni , Mjini Kilosa wakipita kwenye barabara iliyojaa maji ya mafuriko ya mvua pamoja na mizingo mikononi na vichwani kwenda kwenye makambi yaliyotengwa mjini humo
Vijana wa mjini Kilosa akitumia fursa ya mafuriko yaliyowaathiri wakazi wa Kata mbalimbali za mjini humo kuwasafirishia mizingo yao kwa kutumia usafiri wa mkokoteni na kutoza gharama ya sh: 1,000 hadi 2,000 kutokana na umbali. Mama akimwesha uji mwanae mchanga baada ya kufikishwa eneo la kambi iliyotengwa kwa ajili ya walioathiriwa na mafuriko ya maji katika mji wa Kilosa kwenye Shule ya Msingi ya Kilosa Town. Mafuriko hayo yaliaza tangu Desemba 26, mwaka huu.
Baadhi ya wananchi waliokubwa na mafuriko ya mvua kutoka Kata ya Mbumi, wakitelemsha vifaa vyaao kutoka katika gari la Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mara baada ya kuwafikisha kambi ya Kilosa Klabu.
Kijana akikatisha katika barabara iliyojaa maji na baiskeli yake mgongoni
kambi ya dharura ya walioathirika na mafuriko kilosa
Mkazi wa Kilosa akielekea kwenye kambi ya dharura








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kama mkuu wa libeneke ungeweza kutupasha vilevile viongozi wa kitaifa wamechukua hatua gani ingekuwa bomba sana!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...