Viongozi wa Jumuiya ya Watanzania Roma

Rome: Jana tarehe 30 Januari, Mjini Rome, Italy, kulikuwa na mkutano mkuu wa Jumuiya ya Watanzania Roma. Mkutano huu ulikuwa na agenda mbili, kwanza ni Kupitisha Katiba ya Jumuiya ya Watanzania Roma, pili kuchagua Viongozi.
Mgeni rasmi kati mkutano huo alikuwa Mh. Salvator Mbilinyi, ofisa Utawala wa Ubalozi wa Tanzania nchini Italy ambaye alimuwakilisha Mh. Abeid Aman Karume, balozi wa Tanzania nchini Italia.
Waliochaguliwa kuwa Viongozi ni ndugu Leonce Uwandameno kama mwenyekiti wa Jumuiya, ndugu Erasmus Luhoyo Pindu, kama mwenyekiti Msaidizi, Diana Olotu kama Katibu msaidizi. Katibu na Mweka hazina wamebaki wale wale yaani Katibu Ndugu Andrew Chole Mhella na Mweka Hazina ndugu Awadhi.
Kwa picha na habari zaidi tutembeleeni hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. ondoeni hiyo miziki kwenye blog yenu...inakera, sisi tunataka kusoma information na siyo kusikiliza muziki, Also too much stuff..ondoeni weather, messenger pingbox, exchange rate, and currency converter....zinaifanya blog yenu inakuwa slow and congested...sisi tunaochajiwa kwa bandwith inakuwa soo... JUST MY OBSERVATIONS!!

    ReplyDelete
  2. ni vizuri ndugu zetu Italy mnaonyesha umoja.
    Mdau
    Duniayetukubwa.blogspot.com

    ReplyDelete
  3. Mbona wakristo watupu, hakuna watanzania waislam hapo roma. Nauliza tu!!!

    ReplyDelete
  4. wakristu au waislam wote ni watanzania hatuna ubaguzi angalia vizuri we mdau uliyeulizia khsu suala la muislam au ukristu yupo mweka hazina ni muislamu na muwakirishi wa wajumbe pia ni muislamu. asante sana michuzi umeitoa watanzania wote ni ndugu hatuna udini wala ukabila.asante mi mdau.

    ReplyDelete
  5. Ongeleni sana kwa umoja wenu ndugu zangu Watanzania wa Roma. Watanzania wengine waishio nchi za nje wanashindwa kuwa na umoja kama nyie, wanatawaliwa na chuki na matatizo ya kila aina. Mungu Ibariki Africa mungu Ibariki Tanzania!

    ReplyDelete
  6. Mbona London wote ni waisilamu na hakuna anayelalamika? Na huku Bongo wote ni waisilamu na hakuna anayelalamika. Nilikuwa nashangaa tu.

    ReplyDelete
  7. Watu wengine sijui mtakuwa lini. Karne ya 21, na bado mawazoni mmekalia mambo ya UDINI tu badala ua kufikiria mambo muhimi ya kuendeleza nchi yetu na jamii zenu hapo ulipo.
    Dini yako inakusaidia nini wewe hapo ugenini ? Watu kama nyie ndio mnawarudisha wenzenu nyuma, kwa kung'ang'ania mambo yasiyo na msingi.
    Community nyingi za waTZ ZINAKWAMA kwa sababu watu kama nyinyi. Huyu dini hii, na yule dini ile. Grow up people!!

    ReplyDelete
  8. Muhimu sana, sasa tujiulize nchi nyingine mbona hatusikii? balozi zinashindwa kuwahamasisha watanzania kuanzinsha umoja, kila mtu anajifcha kama panya buku... umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, penye wengi hapa haribiki jambo!

    tuige mfano huuu

    ReplyDelete
  9. sishangai hasilani,kuna imani/dini tu wakiwaona WAKRISTO basi damu zinawachemka na roho ya kuua inawaingia ghafla...wao ni ruksa na kheri kuchukia wakristo.msipate shida kumlinganishia mahali kwingine kwenye dominant religion/pple

    dini zenyewe zililetwa tu afrika

    ila ivi vyama mh!!!aya

    ReplyDelete
  10. Hongera sana.
    kama Mhella ninayemfahamu ni Deo je umeshamaliza shahada yako ya uzamivu? Tulikutana Torino. Kweli nawapongeza sana kwa umoja wenu.
    nduguyo
    Mzalendo kutoka Tabora

    ReplyDelete
  11. Mzalendo toka Tabora hapo juu, Deo Mhella ni kaka yake Andrew Mhella.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...