Kambi ya muda kwa waathirika wa mafuriko Kilosa


Unaweza kupata mpango tulio nao hadi hivi sasa wa kushiriki katika kuchangia wahanga wa mafuriko yanayoendelea nchini kupitia Chama cha Msalaba Mwekundu.


Tumepata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Mkuu wa Kitengo cha Maafa wa chama hicho nchini Bw. Joseph Kimaryo ambaye anatueleza hali ilivyo hadi hivi sasa (Jumamosi Januari 9, 2010).

Kwa kushirikiana na tovuti za Jamiiforums na Mdau wa Jamii Bw. Issa Michuzi; pamoja na kushirikiana na Mtandao wa Wanaataluma wa Tanzania (TPN) tumeandaa mpango wa kuwashirikisha Watanzania mahali popote pale walipo kuchangia katika adha hii inayowakuta ndugu zetu katika mikoa mbalimbali hasa Morogoro, Dodoma, na sasa hivi Shinyanga na hata Mwanza na kuna uwezekano wa sehemu nyingine nchini kwa kadiri siku zinavyoendelea.

Tumeamua kutumia Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania kwani rekodi yao katika kufika na kutoa misaada wakati wa majanga hailinganishwi na chombo au taasisi nyingine yoyote. Zaidi ya yote tumepata uhakika wa kutosha wa misaada yetu kufika kwa walengwa baada ya kuzungumza na Katibu Mkuu wa Chama hicho Mstahiki Meya (Dar) Adam Kimbisa (CCM).

Pata nakala ya mpango huo hapa:
http://www.box.net/shared/g99no7hjkg


Sikiliza:
http://mwanakijiji.podOmatic.com/entry/2010-01-09T22_05_16-08_00
Pamoja tunaweza
- Mzee

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. SHUKURANI MKUU WA KAYA TUENDELEE KUWA PAMOJA MPAKA CHAWA AVUNJIKE

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...