Ankal Pole na libeneke,
Ebana ankal Kuna Mdau wetu wakaribu ameondokewa na Kausafiri kake kakisasa sana ambacho hata sisi kinatusikitisha kwakweli. Ilikua ni Cadillac Escalade moja nyeupe matata sana Hapa tauni iliyokua inajivinjari sana maeneo Ya Sakina ambayo jana imepata ajali ya moto maeneo ya Mto Nduruma barabara ya Moshi road pale eneo la tukio siuna pajua nazile Speed hump bora kuliko zote Tanzania.
Uwez amini ile gari imeisha imekua kama RAV4 ivi . Ilikua mida ya saa moja ivi jana jioni tukio lakutokea lilitokea ingawa hakuna aliye dhurika pia hakuna kilicho okolewa. Wadau msiweke tu Sticker za Fire Brigerde kwenye kioo angalau kamtungi kakuzimia moto kawepo.
Mdau Arusha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. We unadhani moto wa gari utaukabili na kifaya extinguisher? Utaumia bure halafu upate hasara mara mbili - ya mwili wako na ya gari lako.

    Gari ikiwaka moto kimbia, acha bima wakulipe. Ndio kazi ya Bima na ndio maana unashauriwa ukate comprehensive.

    ReplyDelete
  2. Two things involved,,,,either limungua bahati mbaya au....ili insuarance ilipe kama

    ReplyDelete
  3. eehh sasa wewe Anko umezidi sasa kama umeamua kutuweka na vifo za magari mmmmh tutawekewe na vya baiskeli sasa!!

    ReplyDelete
  4. Ankal, mimi naona kama watu hawawezi kututmia habari kwa lugha ambayo ni ya kueleweka, basi watulie, kuliko kutuletea habari kwa lugha ambayo mie naiita ni ya kipuuzi.

    Kama ni kiingereza, tumia kiingereza, na kama ni kiswahili basi tumia lugha ya taifa hiyo ambayo asili mia kubwa tunaijua.

    Sasa mtua napotumia lugha ya mchanganyiko wa ajabu ajabu kama huu, kuna sababu gani ya kutuelewesha habari ambayo haieleweki..?
    Hebu tujirekebisheni jamani.
    mie binafsi huwa naboreka sana nikutapo habari zimechanganywa kwa lugfha za ajabu ajabu..

    ReplyDelete
  5. Kweli bongo tambarare watu wanakula kilaini,Hizi sticker za zima moto sijui zinasaidia nini?wangekuwa wanakupa basi za vifaa vya kuzimia sawa,lakini ni kikaratasi tu cha kukolezea moto tu gari likiwaka.Wiziii mtuupuuu

    ReplyDelete
  6. Kaka Ankali,
    Nawashauri wanunuaji wa Magari kutoka marekani wawe makini sana. haya magari yanaonekana makubwa na imara lakini utengenezaji wake ni kama makaratasi (fiber) si kama gari nyingi za japan. Unaona kama hilo Cadilac hiyo "body" ni kama karatasi likishika moto kimbilia na si rahisi kuliddibiti,
    Mdau Majuu

    ReplyDelete
  7. Hapo swali la kujiuliza ni kwanini hayawaki moto huku US na canada! Kinachojitokeza hapo ni kwamba kuna uwezekano kabisa kuwa hayo magari hupelekwa kufanyiwa services hasa za kiumeme kwa mafundi uchwara na hivyyo hufanya mfumo wa nyaya (Wiring) mbovu na matokea yake ndio haya. Pia inawezekana kuwa mafuta wanayoweka kwenye gari si masafi hivyo kusababisha uchonmaji (Combustion) kuwa mbaya na kushika moto. Nawakilisha tu.

    ReplyDelete
  8. Arusha kuna tukio the same lilitokea , na lili toke the same place, lilihusisha range rover vogue,ss ni mawili km mdau hapo juu alivyosema either insuarance ili alipwe lipya ama kweli ajali, ila nampa jamaa pole maana gari ni kali mno

    ReplyDelete
  9. HUWEZI KUZIMA MOTO WA GARI NA KI-FIRE EXTINGUISHER NDOGO HUO NI WIZI WA VIGOGO SERIKALINI MRADI WAO

    ReplyDelete
  10. acheni ujinga magari hayo watu wanaedesha mpaka engine inazima yenyewekwa km kibao bila kuhunguan itakuwaje zikifika bongo ndio zinaungua moja zinaingia kwa tax exemption (bule) kwaiyo wanaonyesha kiwango halisi cha hiyo gari wakati wameinunua kwenye auction kwa bei poa sana hakifika huko bango ina register hiyo ela kwenye insualense kwaiyo ikiunguzwa pesa hanayopata ni mara mbili ya aliyo nunulia

    ReplyDelete
  11. Kwa nini haya magari makubwa yakija huko yanaungua? hayajazoea jua au vumbi?

    ReplyDelete
  12. Ankal, waambie wadau wakitoa habari kama hizi wawe wanatoa number za gari. sisi watu wa insurance pressure zinapanda, ohhhh

    ReplyDelete
  13. Poa tu..Japo kuwa wengi mtaona km roho mbaya...Wabongo mnanunua magari ya kifahari km hayo na hali ya barabara na huduma zetu mwazijua...Tumezidi kutoishi na hali halisi ya mazingira yanayotuzunguka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...