sehemu ya barabara ya ocean road jijini dar kutoka pale hospitali hadi feri ni marufuku kupita baada ya saa 12. ila kuna wadau wengine aidha hawaoni hilo tangazo ama ndio yale yaleeee. maana haipiti siku unakuta jamaa kapigwa mkono baada ya kukatiza sehemu hiyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Kupita kwa miguu tu au na kwa gari??

    ReplyDelete
  2. imeanza lini habari ya mwisho saa 12 kupita hapo?je ni kwanini??naomba wadau mnijulishe.

    ReplyDelete
  3. Mimi naona huo ni UBAGUZI unaanza.

    Vibao vya aina hiyo karibu tutaanza kuviona kwenye mahoteli na baadhi ya mitaa hapa mjini.

    Mbona haikuwahi kufungwa huko nyuma, kwa nini iwe sasa.

    ReplyDelete
  4. Kweli si haki kufunga barabara ya umma kwa masaa 12. Unayesema enzi za Mwalimu ninafikiri ni kutomtendea haki Mwalimu au unasoma vibaya historia. Enzi za mwalimu sio tu kwamba barabara ya ocean road haikuwahi kufungwa, bali pia Mwalimu aliishi nyumbani kwake mchachani, na ikulu haikuwa na ukuta mnene kama huo unaouona leo hii. Kama tulikuwa hatujazaliwa jamani tuwaulize wazazi watueleweshe vizuri.

    ReplyDelete
  5. wametoa lingine wazee wa mji. Tangazo jipya baada ya kanisa la mtakatifu petro oysterbay ukitaka kukata kulia unakutana nalo. sasa we kaidi uone; kichura mpaka kwa mjomba wako.

    ReplyDelete
  6. acheni upuuzi mimi ninakaa sea view foleni la hapo jioni halielezeki hiyo njia ndio mkombozi wetu japo kuwa nayo ni foleni la kutisha jioni, au kwa kuwa mzee malecela, mkapa na vigogo wengine wanakaa huko? kwa mtindo huu hakuna dereva wa tax atayekubali kukupeleka sieview bila ya sh 10,000/= kutoka posta

    ReplyDelete
  7. MUNAMUONEA NYERERE, NYERERE ALIKUWA HAKAI HAPO WALA HALALI HAPO ALIKUJA ASUBUHI TU KAMA OFISINI. MIMI BINAFSI SIKUBALIANI NA TANGAZO HILO HUO NI UBAGUZI TULIOKUWA TUNAUPINGA SOUTH AFRIKA NA APARTHEID SASA TUNAULETA HAPA KWETU, KINACHOTAKIWA NI ULINZI TU, POLISI WAWE WANALINDA HAPO 24 HOURS. HIYO NI SEHEMU YA UMMA KILA MTU NI YAKE SI YA RAIS TU. KITU KILICHOFANYIKA HAPO NI WAKUBWA KUJIPENDEKEZA TU. MTU KAMA ANATAKA KUMDHURU RAIS SI LAZIMA AJE IKULU, NA ZIDHANI KAMA KUNA MTU MWENYE NIA HIYO. TUACHE UBAGUZI NA TUSIJISAHAU KAZI MLIZONAZO NI ZA UMMA ZETU TUMEWAPA KWA VILE SI WOTE TUNGWEZA KUWA AMA POLISI AU MARAIS WA NCHI YETU NI LAZIMA KWA UTARATIBU TULIOJIWEKEA TUCHAGUWE WACHACHE WATUONGOZE NA TUWALIPE KWA KODI TUNAZOTOWA. TUNAOMBA MAJIBU JUU YA HILI TAFADHALI HASA KUTOKA WA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI, WAZIRI ANAYEHUSIKA NA BARABARA NA SAID MWEMA.

    ReplyDelete
  8. jamani eeh hilo eneo ni hatari sana kwa vibaka kwa kweli hata ukiaribikiwa na gari eneo hilo hiyo mida utashangaa zinakuja kama mtu kumi na mapanga na huwa hazina huruma kitu cha kwanza wanatakaga ni viselula wallet na vingine muhimu siku hizi wameibuka wanabeba na lap top kabsaaa kwa kweli hawa polisi bongo wanazaidiwa na vibaka hadi kutuwekea matangazo ya namna hii ni aibu kubwa! kwani nchi iko vitani??? kazi ya mapolisi si kulinda raia jamani sasa hii imekaaje?? nyie polisi mkimaliza mafunzo hivi huwa mnakulaga viapo vya kula rushwa? wao ni kwenda maeneo yenye ulaji tuu na kudai rushwa wakati maeneo hatarishi wanayajua ovyo sana hili jeshi la polisi itabidi tukodishe askari kutoka israel waje watusaidie manake hawa wakwetu wamelala doro rushwa tuuuuuu hadi mnaboa

    ReplyDelete
  9. kama wamezuia njia basi hata meli na boti za zenji nazo wazipige stop. au wahamishe feli, na soko la masamaki

    mdau

    ReplyDelete
  10. Jamani heeeeeeeeeeeeeee hiyo ndio Capitalism kama hamjui...............hahahaha.Kanchi maskini kufuata sera za matajiri ndio matokeo yake.Hata sehemu za Ufukwe nyingine Tanzania huwezi kuingia ni mali ya mtu.Msishangae that is Capitalism(Ubepari)

    ReplyDelete
  11. Teh teh hapo sijui ni masuala ya usalama, nyerere msimguse, fensi yake ilikuwa ndogo hata mtoto wa miaka miwili anaruka, nasikia hata pale wizara ya elimu, fedha n.k hakuna kupaki gari pale njeeeee

    ReplyDelete
  12. hamisheni li-ikulu lenu mpeleke dodoma msitujazie mifoleni ya ajabu tena kisa apo mnakataza!!

    tangazeni basi kwa umma mzima wa watanzania katika redio,tv na vipaza sauti ili tujue kuna mafala fulani wanaazisha ya ukoloni bongo!

    what is this yu fake people??

    ReplyDelete
  13. maumivu ya kichwa huanza pole pole .......

    tunarudi kule kule walaah

    sina la ziada

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...