MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar leo imetoa hukumu dhidi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Amatus Liyumba. Katika hukumu hiyo Liyumba anakwenda gerezani miaka mwili baada ya kupatikana na hatia ya utumiaji mbaya wa madaraka alipokuwa kazini, hususan wakati wa ujenzi wa ghorofa pacha za makao makuu ya BoT jijini Dar.
===================
Awali Liyumba alifikishwa mahakamani hapo akiwa pamoja na aliyekuwa meneja miradi wa BoT Deogratius Kweka, ambapo kwa pamoja walikabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la kutumia vibaya madaraka aliyokuwa nayo, jambo lililopelekea serikali kupata hasala ya sh bilioni 221, kupitia ujenzi wa majengo pacha ya BoT.
Hata hivyo kabla ya kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka, upande wa mashtaka ulimuachia aliyekuwa mshtakiwa mwenza wa Liyumba {Kweka}, na kumshitaki Liyumba kwa kesi hiyo.Upande huo wa mashtaka uliita mahakamani hapo mashahidi 8, wakiwamo waliokuwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa BoT, pamoja na kutoa vielelezo mbali mbali vinavyohusiana na kesi hiyo.
Baada ya ushahidi huo kumalika kusikilizwa, Mahakama ilifikia uamuzi wa kumfutia Liyumba shtaka la kuisababishia serikali hasala ya bilioni 221 baada ya Upande huo wa serikali kupitia ushahidi na vielelezo vyake kushindwa kuithibitishia mahakama hiyo kama Liyumba alihusika na kosa hilo.Kufuatia uamuzi huo, mahakama ilimtaka Liyumba kujitetea juu ya uhusika wake katika shtaka la kutumia vibaya madaraka aliyokuwa nayo.
Katika utetezi wake Liyumba alijitetea mwenyewe kama shahidi wa kwanza kutoka upande wa utetezi, na baadae alimwiita shahidi wa pili ambaye ni Bosco Ndimbo Kimela, aliyekuwa katibu wa BoT.Baada ya kumaliza usikilizwaji wa ushahidi huo, mahakam hiyo ilizitaka pande zote mbili kuwasilisha hoja zao za kisheria, ambapo alipanga kusoma hukumu dhidi ya Liyumba ifikapo May 24, 2010.
Mambo ya Tanzania kweli ni kichekesho sana, yaani mtu anafanya madudu ya ujanja na kuiba mihela kibao halafu anapewe adhabu ya miaka miwili tu jela? Baada ya miaka hiyo jamaa atatoka na kuja kutanua mitaani kama kawaida kwani atakuwa mtu huru.
ReplyDeleteMali alizonazo zote zinatakiwa zipigwe mnada, ili akitoka awe na nyumba ya kawaida ya kuishi na apande daladala hapo mjini.
Nchi kama China hapo ni kitanzi tu.
HIZI SHERIA ZINA KASORO. ZIREKEBISHWE. ZIWE KAMA CHINA. MIAKA MIWILI KWA HASARA KAMA ALIYOSABABISHA NI UTANI NA USANII MTUPU. PERIOD. HUU SI UTAWALA WA SHERIA BALI SHEREHE.
ReplyDeleteMiaka Miwili? Amekwisha kaa mwaka mmoja mahabusu, hivyo kabakiwa na mmoja? Tulikwisha sema, ukiwa na pesa zako Bongo, wewe ni mfalme!
ReplyDeleteMaskini Liyumba!
ReplyDeletePOLITICAL DRIVEN VERDICT. SERIKALI IMEBEBWA
ReplyDeleteKUTOJIAMINI KWA MAHAKIMU WETU. HE WAS SUPPOSED TO WALK FREE.
kweli na kukamua mipesa yote hio miaka miwili..kweli bongo tambarare..
ReplyDeleteBongo tambarareeeeeeee,kama ulikuwa kiongozi mkubwa na una hela, au ulijua kula na mwenzio vizuri huwezi kufungwa hata siku moja,hapa changa ya macho tu ,coz jamaa ataambiwa akate rufaa, then anatoka,siku zote wanafungwa wasio kuwa na mtandao mzuri,wapi Zombe? Dito?,
ReplyDeleteankal ,acha kubana,huu ndio ukweli unless na wewe upo kwenye system
Tanzania Oyeeh
ReplyDeleteWakati China wangempeleka jela maisha au kumpiga risasi MOJA TU kichwani.........
Tanzania....Tanzania.....Nchi yenye mifumo ya utawala ya KINAFIKI kwa raia wake.
wezi wa kuku miaka thelathini wezi wa mabilioni aka vijicent miaka miwili au free poa tuuu hatufiki ng'ooo labda tuongozwe na wayahudi
ReplyDeleteJAMANI HASARA YA 221 BILIONI SHILINGS NA KUTUMIA MADARAKA VIBAYA NI MIAKA MIWILI TU, WAKATI KIBAKA AKIIBA KUKU ANAKULA MVUA TANO, SAWA WATASEMA KUHUSU 221 BILLIONA ALIFUTIWA ALIKUWA ANAKABILIWA NA MOJA TU LA KUTUMIA MADARAKA VIBAYA, SASA TUULIZANE ALIYATUMIAJE VIBAYA NA ADHARI ZAKE ZILIKUWA NINI? HAPA INAONYESHA FIKA KUNA WATU WAKUBWA WANAHUSIKA WANATAKA KUFUKIA HII KESI IISHE TU KUTUPIGA CHANGA LA MACHO AONEKANE AMEFUNGWA NA HAKI IMETENDEKA, HII SI KWELI. NCHI KAMA AMERIKA HIVI HATA KOSA HILO LA KUTUMIA MADARAKA VIBAYA ANGEKULA MVUA SI CHINI YA MIA MOJA (100)KWA KWELI HATUTOFIKA TUNAKOTAKA TUFIKA UTAWALA WA HAKI NA SHERIA NA MAENDELEO YA KASI KWA WOTE. EBU NENDENI JUST NJE KIDOGO TU YA DAR UONE MAISHA YA WATU YALIVYO YA SHIDA WAKATI PESA ZA UMMA HAZITUMIKI VIZURI. 221 BILIONI ZINGEFANYA MAENDELEO MAKUBWA KAMA ZINGETUMIKA SAWA SAWA.
ReplyDeleteDuh Haya Ndio Maamuzi ya Mahakama si tii neno lakini miaka miwili midogo sana kwa huyu Liyumba ina nipa moyo kwamba tuendako hata viongozi wawe makini hata maisha watachezea Amka Tanzania,Amka Majaji watu wote ni sawa.
ReplyDeleteUsanii mtupu mwakani anasubiri msamaha wa Rais. Ingefaa afilisiwe
ReplyDeleteWHAT A JOKE!
ReplyDeleteOnly miaka 2?????? Kazi kweli kweli. Aibe 221 bill, adhabu 2 yrs???
ReplyDeleteKwa hali hii hat na mimi nitaiba nitakapoingia serikalini, wadau kwa sasa niko private sector, huku ninatafuta CPA, nikiipata tu naenda sirikalini,
wezi wa ng'ombe wamehukumiwa Miaka 30 kule Morogoro. mwizi wa mamilioni anakwenda jela miaka miwili...Bongo Mswano kweli
ReplyDeleteKWA MTAZAMO WANGU FINYU NA UFIKIRI WANGU MDOGO NA UWEZO WANGU MDOGO WA KUCHAMBUA MAMBO NINAONA KUWA TANZANIA HAKUNA HAKI HATA KIDOGO, JAPO SIUNGI MKONO WALA MIGUU UWIZI WA AINA YOYOTE ILE. LAKINI LABDA KWA VILE MIMI SI MTAALAM WA SHERIA, HIVI INAKUAJE MTU ALIYEIBA KUKU AU BAISKELI tena bila kumjeruhi mtu kwanza ANAPATA KICHAPO TOKA KWA WANANCHI kisha AKIFIKISHWA MAHAKAMANI ANAFUNGWA MIAKA MITANO au SITA,NA HAKIMU ANA "NA HII IWE FUNDISHO KWA WENGINE WENYE MAWAZO KAMA YA HUYU" SASA HUYU JAMAA KALITIA TAIFA HASARA YA TSH BILION 221 (MABILION HAYA ETI), ANAFUNGWA MIAKA MIWILI TUU na hii MIAKA MIWILI KWA TZ NI MWAKA MMOJA, HAKUNA KUFIRISIWA WALA NINI, HIVI KWELI KATIKA MABILIONI YOTE HAYO YEYE HAKUPEWA HATA BILIONI KUMI KWELI? HARAFU AKITOKA ANADUNDA MTAANI TU MABILIONI YAMEKWENDA. NA HATA AKIENDA NDANI KWA MAHELA YOTE HAYO WALIYOIBA HATAKULA CHAKULA CHA HUKO MAHABUSU HATA SIKU MOJA. KAMA NDO HIVYO WATU WATAJITOA MHANGA TUU. KWA HELA ZOTE HIZO HATA KAMA AKIPATA KAMISHENI YA BILION TANO KISHA JELA MWAKA MMOJA AAAAAAAAAAAH ILI DILI LINALIPA. ALITAKIWA KUFUNGWA KAMA MHUJUMU UCHUMI HUYU. TUSIFANYE MZAHA ETIII. EBU SOMA TENA HAPA "sh bilioni 221" MY GOD zen JELA MWAKA 1 "ALEKANGI TWIFIKA DEH"
ReplyDeleteKCC-UKEREWE
where is justice liyumba anyongwe
ReplyDeleteHIVI HIYO MIAKA MIWILI INALINGANA NA UBADHIRIFU ULIOFANYIKA? COZ BAADA YA MIAKA HIYO MIWILI MTU ATATOKA NA KUENDELEA KUPONDA MALI ZILIZOCHUMWA KWA UOZO HUO. INGEKUWA BORA KAMA ANGEFILISIWA MALI ZAKE KWA MANUFAA YA UMMA PAMOJA NA KIFUNGO, HELA ZINGEPATIKANA KUENDELEZA MIRADI MBALIMBALI YA UMMA KM BARABARA NA ZAHANATI!
ReplyDeleteyaaani miaka miwili tu, kwa criminal kama huyu? wakati kuna wengine wapo jela zaidi ya miaka 7 kwa makosa ambayo hata hayana maana. T.I.D alihukumiwa kwenda jela mwaka mmoja kwa kosa la kumpiga mtu. huyu anakwenda jela miaka 2 kwa kuiletea serikali hasara ya bilioni, bilioni , bilioni 221, kwa nchi masikini kama Tanzania, nchi ambayo ilikuwa ikiomba kufutiwa madeni, kweli inaingia akilini? Two years!!? Raia wanapata tabu vijijini huko maji hakuna, huduma za afya vijijini huko tabu, hakuna chochote maskini, huyu jamaa katia hasara, bilioni 221, then kahukumiwa miaka 2. YANI MI NAONA HII HUKUMU KAMA INAZIDI KUCHOCHEA ULETAJI WA HASARA SERIKALINI.
ReplyDeleteMMHHH!! NI MTAZAMO TU LAKINI.
huu ni ungese mtupu jizi kama hili serikali gani hii,upuuzi
ReplyDeleteEven with the landmarks? Hiana hiana
ReplyDeletebora wangemuachia tu!hii geresha kesho utasikia wafungwa wenye makosa fulani wametolewa kwa msamaha wa kiongozi fulani na yeye out!vibaka wanafungwa miaka 30 kwa kuiba pochi yenye sh 5000 yeye billions miaka 2!!!!!!!!!!
ReplyDeleteNa wapi kesi ya zombe!!! sheria TZ zipo kwa ajili ya maskini tu.
wangemuachia tu tujue moja!na zombe ndo imetoka!
ReplyDeleteWengine serikalini, manispaa, halmashauri name it...kama kweli mnasafisha basi fagio lisiwe na chelewa MOJA tu......
ReplyDeletehivi nyie mnallamika nini pigeni dili hii ndio style pekee ya kutokea. watanzania vipi mnaonyeshwa how to get rich unalalamika.Uwanja ni wenu. na mhasibu yoyote wa serikalini kama huna hata ka Vogue katika utawala huu jinyonge
ReplyDeleteMdau
POAAAAA,TIJIFUNZE WABONGO KUCHAGUA VIONGOZI BORA,KAMA VIP TUPOTEZEE TUU MANAKE IMESHATOKEA KWANI HAIBADILIKI MKUBWA MKUBWA TU,MDOGO HANA CHAKE,MWENYE KISU KIKALI NDIE ANAEKULA NYAMA
ReplyDeleteJAMANI WATOA MAONI WENZANGU, HIYO MIAKA MIWILI NI KWA KOSA LA KUTUMIA OFISI VIBAYA TU NA HANA KOSA JENGINE HUYO MZEE WA VIGARI VYEKUNDU.
ReplyDeleteKOSA LA KUTIA HASARA YA MABILIONI LILIFUTWA NA MAHAKIMU HAO HAO.
TAFADHALI MSICHANGANYE VIFUNGU VYA SHERIA VYA MAHAKAMA NA VILE VYA PORINI.
Upuuzi mtupu.
ReplyDeleteAkili za kuambiwa! changanya na zako halafu saaaaaafi.
ReplyDeleteNyie watu mbona hamjui kufuatilia kesi. Shtaka la kuisababishia Serikali hasara ya Mabilioni liitupiliwa mbali na majaji wote watatu baada ya mawakili wa serikali kushindwa kuthibitisha. Akabakiwa na kosa moja tuu la kutumia madaraka vibaya,ambapo mahakimu wawili wamemuona ana hiyo hatia na mwingine mmoja amemuona hana hata hiyo hatia.
ReplyDeleteUKWELI NAUNGANA NA HUYO HAKIMU MMOJA KWANI HIYO HATIA IMESHINIKIZWA TUU KISIASA ILI KUWARIDHISHA WATU KINYUME NA SHERIA. Kosa la kutumia madaraka vibaya ni kufukuzwa kazi na siyo KUFUNGWA. LIPUMBA KATA RUFAA MAHAKAMA KUU NA NAKUHAKIKISHIA YOU WILL WALK FREE.
Stupid..plain stupid..they can lock me up for 5 years if they want to if give me half of the money...infact make the a quarter of the money for 10years...Most Tanzanians will live their lives without getting even 5% of the money lost...WIZI MTUPU NDANI YA WIZI MTUPU!
ReplyDeleteKUKU MWIKA 15, MIHELA KA HIYO MIAKA 2 DADAHHHHH!!
ReplyDeleteTUNAKUFA BILA KELELE MASKINI SIE.... MMMMHH. POOOAAA
WEWE MSOMAJI UNAYESEMA KOSA HAPO NI LA KUTUMIA OFISI VIBAYA TU NA SIO KUSABABISHA HASARA, HEBU TUAMBIE AMETUMIAJE OFISI/MADARAKA VIBAYA? SIO NDIO KWA KUFANYA MAAMUZI YA AJABU YALISABABISHA HASARA AU KUNA JINGINE? HAPO NI KUTUZUNGUKA TU ILI AONEKANE HAJATENDA KOSA KUBWA, UKWELI UTABAKI PALE PALE, OTHERWISE ALITUMIA OFISI VIBAYA KWA KUIGEUZA BAA AU HOTELI AU LODGE? ALIKUWA ANAFUGA KUKU NA MBUZI OFISINI! UPUUZI MTUPU
ReplyDeleteYes Nakubali Tz tuna wasomi wa Ukweli Katika kila fani ,na hata wasiosoma wanaona faida ya wasomi wetu bongo (hatari kweli kweli Vyeti mitaani)
ReplyDeletendugu yangu michuzi kwa kweli mpka yaan mwili usikia baridi! yaan madudu yote yale bwana mkubwa huyo! then miak 2 tu! bora wasingetupotezea muda! wa kufatilia mie nadhan wangemuachia huru tu! kama bwana zombe,people are mature!? lakin hapo nyumban ni pagumu sana na laana ipo mie nadhan, iwezekan leo maisha ya mtz halis hakuna asiyeyajua leo inakua ubabaishaji tu! na kutokupendana, mie nadhan sheria zetu zingeangaliwa tena kutokana na maisha yetu halisi!! mfano kaka michu hebu agalia china, hata pia japan wako makin sana kwenye ubathilifu na ndio nchi tajir angalia pia usa,then tunalia tunataka maendeleo maendeleo gani yasiyo a uzalendo!! mwalimu nyerere nadhan wangemdondosha kwa presha mzee wa watu!! jaman kweli mtu anatafuna fedha zote hizo wakati hapo mwananyamal hosp. dawa mtihan!?,amana hosp.wamama wajawazito vitanda haba!? barabara kiwango cha lami ziro folen sasa nasikia ndio usiseme!! inakua kama hawaoni wakitoka nje!! hata flyover kuanzia posta hadi mbezi! jaman!!?? kwa kweli nchi haitufundishi bali inazid kupotosha,hiyo ni laana!!
ReplyDeletemdau japan.
Daudi, upo Juu!
ReplyDeleteVidagaa tu hivi, mapapa bado yanaogelea.
ReplyDeletebill 222.kwa miaka 2? huo wizi unalipa sana.kwa walio na nafasi za kuiba wataiba sana.Hata kama ni 1b. kwa miaka 10 wengi watajitolea,biashara gani utaweza kupata faida hiyo kwa muda huo.
ReplyDeleteUNYESEMA UKAFUNGE MIAKA 10 ILI MRADI UPATE KASEHEMEU KA $$$ ZA MTUHUMIWA UMENICHEKESHA SANA.
ReplyDelete(US BLOGGER)
Msamaha wa wafungwa kila mwaka December 9th ndo Liyumba atakuwa huru. Na hapa hakuna kesi tena. Hongera mafisadi wa Tanzania. Endelea kuchangua Viongozi wabovu. Mmtalionja jiwe. Mafisadi wa Tanzania hawanaga kesi. Tanzania hakuna sheria endapo kama wewe ni fisadi. Sheria huwa inawakumba walala hoi.
ReplyDeleteSIKU YA UHURU DECEMBER 9TH /2010 LIYUMBA JUU ZAIDI, JK atakutoa kwa sababu ndo mlezi wako.
Mdau USA
mimi ninafikiri hastahili hata kufungwa nimpongeze hakimu aliyemwona kuwa hana hatia. Haya matumizi mabaya ya ofisi yanafanywa sana na wakubwa wa nchi yetu. Labda wanefungwa wao kwanza. hapa nchini ufisadi umekuwa sana na wanaofungwa ni watu wadogo tu wasio na kitu. Lakina wakubwa wote ni mafisadi wakubwa wanaostahili kwanza kwenda jela. Pole sana ndg yangu lyumba. baada ya kukuta rufaa utatoka tu.
ReplyDelete