JK akiwa ameshika sanamu ya Faru wakati wa sherehe za kuwapokea Faru Watano kati ya 32 kutoka Afrika ya Kusini. Sherehe za kuwapokea Faru hao walioko katika Kontena katika gari nyuma ya Rais zilifanyika katika uwanja wa ndege wa Seronera katika mbuga ya wanyama Serengeti leo jioni.Kulia ni Waziri wa mazingira wa Afrika ya kusini Mh. Buyelwa Sonjica aliyekabidhi Faru hao kwa niaba ya Serkali ya Afrika ya Kusini.Kushoto ni Waziri wa Utalii na maliasili Mh. Shamsa Mwangunga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Mume Wangu, Mikanjuni TangaMay 21, 2010

    Nchi yetu kila jambo ni lazima RAIS ashiriki hata kama ni dogo kiasi gani!!
    Hivi nyie wasaidizi wake hamjui kuwa kumshirikisha Rais katika kila jambo ni kuongeza gharama za maisha ya Watanzania wengi tulio masikini??
    Nakupenda nchi yangu Tanzania.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 22, 2010

    Kama aliye post habari hii angeeleza ilikuwje hao Faru 32 walipelekwa South kiasi cha kuwa na sherehe ya kuwapokea hawa watano, tungeweza ona umuhimu wa President kuwepo katika shughuli hiyo. Watoa habari huwa mnatuacha sana njia panda jamani....

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 22, 2010

    Kiswahili kimenishinda hapa. taarifa inasema waliorejeshwa. jee waliibiwa, walikimbia au walipotea? na kuna umuhimu gani wa Rais kuhudhurui tukio hili?

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 22, 2010

    Miaka ya sabini na themanini Faru walikuwa hatarini kupotea duniani kutokana na ujangiri. Mataifa makubwa ikiwa ni pamoja na Uk & SA walichukua jukumu la kuwaprotect hao Faru na wakaamua kuwapeleka kwenye zoo za huko kwao. Kwa sasa usalama wa hao faru upo na ndio maana wanarudishwa nchini, kwa maelezo zaidi google the story about the black rhino.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 22, 2010

    Hivi miaka hio Tanzania ilikuwa ma uhusiano na Afrika Kusini?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...