baadhi ya watanzania waliohudhuria washa hiyo wakiingia kwenye uwanja wa Expo Shanghai 2010. Kushoto ni Dr. Justinian Anatory (Mjumbe wa Bodi ya TCRA) akiongozana na Dr. Joseph Kilongola (Mkurugenzi wa TEKNOHAMA TCRA).
mabanda mbalimbali ya maonesho ya nchi mbalimbali zinazoshiriki kuonesha jinsi teknolojia ya habari na mawasiliano inavyoweza kuboresha miji duniani na kupunguza uharibifu wa mazingira.
Picha na Habari
na
Innocent Mungy - Shanghai,China
Tarehe 17 ya Mwezi mei kila Mwaka, Dunia huadhimisha siku ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Jamii (TEKNOHAMA). Nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa, kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa la Mawasiliano Duniani, International Telecommunications Union (ITU), huadhimisha siku hii muhimu kwa nia ya kukumbushana umuhimu wa teknologia ya habari na Mawasiiano kwa maendeleo ya dunia na jinsi inavyoweza kuboresha maisha ya wanadamu kwa ujumla.
Maadhimisho ya mwaka huu yanaadhimishwa kimataifa katika jiji la Shanghai nchini China ambako maonesho makubwa ya teknolojia yanafanyika kwa kipindi cha miezi sita. Maonesho hayo maarufu kama Expo Shanghai 2010, yanayoendana na kauli mbiu ya mwaka huu, "Miji Mizuri, Maisha Bora" yalianza rasmi mei mosi mwaka huu na yataendelea hadi mwezi October 2010. Bofya hapa kwa habari zaidi: http://www.itu.int/wtisd/2010/theme.html
Mamilioni ya watu wamefurika kwenye jiji hili la Shanghai linalokadiriwa kuwa na wakazi milioni 22 na ushee katika kusheherekea maadhimisho haya yatakayofikia kilele jumatatu tarehe 17 Mei 2010 kwa hotuba na makongamano mbalimbali yanayolenga katika kuelezea mafanikio ya sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano na mchango wake katika kuboresha majiji na miji ili kuwa mahali pazuri zaidi pa kuishi.
Watanzania kadhaa wako mjini hapa kushiriki katika maadhimisho haya yaliyopata baraka za ufunguzi na Mama Anna Tibaijuka, wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani (HABITAT).
Jana katika Banda la Umoja wa Mataifa, ITU ilifanya washa kuhusu umuhimu wa TEKNOHAMA katika kuboresha mazingira duniani na hasa katika kujenga "miji kijani" ( ICT's: Building the Green Cities of the Future).
Wataalamu mbalimbali walitoa mada zilizoibua hisia mbalimbali kutoka kwa washiriki hususan mapendekezo ya ITU ya kuwa na charger moja kwa simu zote (Universal Charger). Mada ingine iliyosisimua ni ile ya uchafuzi wa mazingira kwa magari yanayotoa hewa chafu ambapo imependekezwa nchi duniani na hasa majiji yajizatiti kuyaondoa magari yanayoharibu mazingira zaidi.
Bofya hapa kupata mawasilisho ya mada hizo kwa undani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 16, 2010

    Teknohama ni kitu gani in English?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 16, 2010

    kanzuri binamu tunategemea mengi toka huko hasa mambo mapya ya teknohama ambayo kizungu chake sisi huku pangani ni taabani

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 16, 2010

    teknohama= teknolojia ya habari na mawasiliano.

    Mdau
    Kariakoo Shimoni.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 16, 2010

    FANYA KAUTAFITI KIDOGO TU, UNA-COMPUTER TUMIA PROFESSOR GOOGLE.COM ATAKUHABARISHA TEKNOHAMA NI NINI. SI KI-ENGLISH NI KISWAHILI, NI KIFUPI CHA MANENO YA FUATAYO: TEKNOLEGIA YA HABARI NA MAWASILIANO SO THEY HAVE JUST TAKEN SOME OF LETTERS IN EACH WORD AND FORM THAT SO CALLED TEKNOHAMA; AS AS FOLLOWING TEKNO-legia ya HA-bari NA MA-wasiliano

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 17, 2010

    Nadhani ni technology

    Lakini nauliza siye tunaenda kuonyesha nini au tunaenda kung'aa macho tu?

    Nilitegemea hizo chance wangeenda vijana wa college wanaosoma vyuo vinavyohusika. Hao watu wakuu wazee wakienda watajifunza nini na tungeomba elimu yao tujue haya majambo wanayajua vipi?

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 17, 2010

    kwako anony wa Tarehe Sun May 16, 07:24:00 PM,
    tembelea, http://www.teknohama.com/ utajua ni nini.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 17, 2010

    TEKNOHAMA ni Teknologia ya Habari na Mawasiliano- Information and Communication Technology-ICT.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 17, 2010

    JAMANI WAVAAJI SUTI, ILE LEBO PALE CHINI YA MKONO WA SUTI INAPASWA KUTOLEWA BAADA YA KUNUNUA SUTI, MSIFIKIRI NI UREMBO. NI USHAMBA KUVAA SUTI NA LEBO. ANGALIA SUTI YA HUYO TALL MWENYE SHATI JEUPE...

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 17, 2010

    Teknohama = Information Communications Technology.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 17, 2010

    wanashangaa tu majengo hao....akimaliza hapo wanunue suti na maredio/tv warudi navyo..with no any implementation ya kilichowapeleka huko

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 17, 2010

    anony wa tarehe Mon May 17, 12:14:00 AM, hivi vijana maana yake nini? Vijana wa shule wanajua technohama? anyway ya wataalamu tuwaachie wataalamu

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 17, 2010

    Asanteni wadau kwa kunieleza maana ya teknohama. Ila nimeangalia tovuti yao (www.teknohama.com) kwa maelekezo ya mdau mmoja na niemona wanatumia neno "wavuti", imenichanganya tena, kwani haipaswi kuitwa "tovuti"? "Wavuti" ni nini?

    By the way, "blog" pia ni nini kwa Kiswahili?

    ReplyDelete
  13. NYONGESA MARTINFebruary 22, 2012

    TEKNOHAMA KWA KINGEREZA NI "INFORMATION AND COMMUNICATIONS TECHNOLOGY".NENO TEKNOHAMA NI UFUPISHO WA ISTILAHI TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO AMBAYO ILITOHOLEWA MOJA KWA MOJA KUTOKA KWA ISTILAHI YA KIMOMBO KWENYE NUKUU PALE JUU.
    NYONGESA MARTIN WAFULA
    MASINDE MULIRO UNIVERSITY OF SCIENCE AND TECHNOLOGY.KENYA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...