Habari iliyoifikia Globu ya Jamii hivi punde,inaripoti kuwa msanii mkongwe wa muziki wa hip hop nchini,Joseph Mbilinyi a.k.a mr II amekamatwa leo mapema asubuhi na watu wanaodaiwa kuwa ni wanausalama wakati anakwenda kwenye kikao cha press talk kinachofanyika kila siku ya jumatatu katika ukumbi wa mikutano wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA),sababu ya kukamatwa kwake bado haijajulikana na haijulikani wamekwenda nae wapi.

Globu ya Jamii inafuatilia kutaka kujua mustakabali mzima wa kukamatwa kwake na italeta taarifa kamili hapo baadae.hivyo tuvute subira.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 28, 2010

    Mtu akitangaza kujiunga na chama cha upinzani anaandamwa namna hii kwa nini jamani? itafika siku kila mwananchi mzalendo ataingia msituni kudai haki yake.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 28, 2010

    recording yake ya kuwataja virusi wanaoharibu tasnia ya muziki wa Tanzania ndo imemponza

    ReplyDelete
  3. E FROM PASSION BARJune 28, 2010

    "wanachotaka wewe upate taabu shida kibao bila sababu.."..na mama hizo nitazikabili...Dawa ya jeuli uwe kiburi...Go go sugu mwana sana hapa Tampere Finland..tupo pamoja mpaka tone la damu la mwisho...

    Pigania usawa....wakikutoa roho bado itikadi zako zitabaki...



    Wanamwita sugu ..sugu sugu sugu.,..

    ReplyDelete
  4. CHANGE WE NEED!June 28, 2010

    WAMESHAANZA HAO,HIVI MAMBO HAYA MPAKA LINI SIASA ZA BONGO,YAANI MTU AKITAKA KUINGIA KWENYE BONGO POLITIKI NI LAZIMA AWE KWENYE HICHO CHAMA CHENU?EBOO HEBU ACHENI UOGA MNA KILA KITU LAKINI HAMJIAMINI SASA MTU KAMA MR 2 NYIE ATAWAATHIRI NINI ZAIDI YA KUMPANDISHA CHART TU MWANASIASA HUYO UNDERGROUND KATIKA SIASA ZA BONGO,MH.HALIMA MDEE WEWE MWANASHERIA HEBU JARIBU KUFUATILIA SUALA LA MWANACHADEMA HUYU MPYA UJUE LIMEKAAJE,

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 28, 2010

    Asije akawa kajiingiza kwenye mihadarati!!! dRU

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 28, 2010

    Chadema nini ? michuzi usibanie Coment za watu zikianza Kudondoka Michuzi jnr tunajuwa anabania sababu ya Clouds. Mwacheni Kijana msimsingizie jamani.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 28, 2010

    wasije wakamnanii kijana wa watu. haki yake wametafuna, bado wanamtafuta? Haya, Chadema .. kijana wenu anaanza kuonja joto ya jiwe!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 28, 2010

    haya ndo matokeo tuliyokua tunayasubili,sugu si umejifanya kujiunga na chadema!bado mkoloni na g-solo nao kutiwa baloni!!habari ndo hiyo ccm ina wenyewe ndugu zangu!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 28, 2010

    wenzako wanavyo chukua kadi za ccm siyo kwamba wanapenda tu au ni kama ccm ndo chama kizuri !!! pole kaka ndo siyasa za bongo system ndo hiyo kweli haki akuna bongo! mumu niebushe nisirudi bongo mimi sitaki sitaki kabisa kuja uko !!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 28, 2010

    Serikali vijana wenye hasira za ku fail maisha tunayaona haya, siku tukiamua watoto wenu wa Oysterbay hawawezi kutuzidi nguvu. Tanzania ni kubwa kuliko Dar es Salaam. Ni hayo tuu!!!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 28, 2010

    Siasa za kizamani sana hizi.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 28, 2010

    Bwana mdogo mr 2 mbona unaingia mkenge kichwa kichwa?

    ReplyDelete
  13. Labda CCM imemkamata kwa sababu SUGU ameamua kujiunga na Chadema ili kupiga vita ufisadi wa CCM.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 28, 2010

    Hawan lolote la kumfanya...Tanzania inaongozwa na Sheria. Kama wana kesi wampeleke mahakamani tusikie makosa yake.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 28, 2010

    Mr Two wewe kichwa cha panzi kabisa. Nilipoona unajiunga na Chadema nikajuwa unajua matatizo uliyonayo na unatafuta namna ya kuyaondoka.
    TZ waachie wenyewe, muulize Mtikila, Seif sharif Hamad, na Jumbe. kumbuka ule msemo unaosema Ukishindwa, jiunge nao.
    Huoni jinsi huyo kabwe, Cheyo na Mbowe wanavyokula nao hao jamaa na kupuliza. Utaishia kuwekwa ndani na kama una ka-green kako ka US, basi ujue jamaa wausalama bongo wanakampango ka kukuharibia. Kubali wamekushinda, jiunge nayo then nyamaza huku ukila asilimia 20 badala ya ile 80 unayotaka wewe. jaribu kukua au kwenda na umri Mbilinyi, unakaribia 40, waza kiforty na sio ki20 sugu.
    pole lakini kw yote yaliyokukuta.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 28, 2010

    Kiranga Haliliwi wala halaliwi Tanga..

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 28, 2010

    hii yote ni kwa sababu ya kuchukua kadi ya Chadema nini?

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 28, 2010

    Nahis jamaa kakamatwa sababu ya wimbo mpya unaitwa Anti-Virus ambapo amewaponda clouds live live.Sikiliza maneno yake.Linki hii hapa:

    http://www.youtube.com/watch?v=hiMGe2HYq2o

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 28, 2010

    Nchi hii haina uhuru binafsi, demokrasia wala utawala wa sheria.

    Kwa nini mtu akamatwe kwa kujiunga na chama halali cha siasa?

    Nchi hii haitaendelea kama haya hayaishi!!!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 28, 2010

    Mmh, huu wimbo umemnyanyapaa mtu, its not right kunyanyapaa mtu mwenye ugonjwa.Tukana utakalo kama mtu kakutukana au kakukwaza, ila unyanyapaaji noo, its too much

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 28, 2010

    We michuzi mbona unabania points za maana ambazo hazina hata matusi?

    Mr II nimeangalia youtube yako (mwangaliaji namba 777).. aisee sema bwana. Bila kusema watu huwa hawasikiagi.

    Nice song by the way.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 28, 2010

    Polisi ilipaswa wawakamate watu waliotamkwa kuwapa mimba watoto wa Tanzania House of Talents, na sio kumkamata MR II. Huu ni ujinga.

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 29, 2010

    nadhani kakamatwa kwa sababu amejiunga na chadema!
    duh siasa za bongo noma.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...