robert na marilyn baada ya kumeremeta katika kanisa la mtakatifu joseph jijini Dar
wakionesha nondozzzz za kumeremeta
wakipozi na familia zao baada ya kumeremeta
wakiwa na wapambe wao kabla ya mnuso hoteli ya golden tulip
wakiwa na familia ya bw. harusi
wakiwa na wafanyakazi wenzie bw. harusi
familia ya Bi. harusi
wakiwa na marafiki toka ughaibuni
na kamati ya maandalizi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 19 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 28, 2010

    hongera maharusi ila bwana harusi asingevishwa 3 piece dar joto sana asije kuanguka bure.

    Ushauri wa bure:

    Kuanzia sasa marafiki chagueni, si kila mtu ni rafiki tu wale wapenzi ambao kwa sasa ni X wakome, kama hawajataka kufunga maisha wakati mko singo kwa sasa lazima watolewe nje. Sio leo tuone mnacheka hapa kesho inakuwa habari nyingine. Magomvi yenu yaishie chumbani sio kilaa mtu mnamwambia (watu wengine wanafurahi) wakubwa zenu lazima wapewe heshima zao.
    Bi harusi jihakikishie nyumba yako ni safi sio watu wanakuja wanashangaa mbona hafagii, hatandiki kitanda, hapiki, kunakuka tu samaki nk. Na sio kuomba pesa ya kila kitu hata chumvi tu lazima mumeo atoe unazorudi nazo sokoni zingine hifadhi vitu vidogo vidogo unamaliza mwenyewe (kuwa strong)
    Bwana harusi, marafiki zako wale mnaokutana nao kwenye bia iwe mwisho ndio mwanzo wa ugomvi nyumbani, uwe unasaidia pia kutandika, kujipashia mwenyewe chakula, kupiga pasi, nk sio kila kitu afanye mkeo tu.

    Huu ni ushauri wa bure mengine ambayo nimeshindwa kuyaandika sababu kamichu hataposti najua mtakuwa mshafundwa (haswa yale ya chumbani)

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 28, 2010

    lakini mnaona wazungu walivyovaa harusini? ni kawaida tu ila sie waswahili ni lazima dhahabu tukaazime, nguo ing'ae na wanja kwa wingiii ndio maana hatuendelei.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 28, 2010

    bib harusi nguo sikuipenda kabisaa ila nywele imetoka kweli na hizo gloves mmmmh dar joto sana ya nini wangemwacha tu kawaida kama hii picha aliyokaa ila harusi inaonyesha ilifana sana.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 28, 2010

    Nyie wa juu hapo mliochangia kweli wanafiki mnaonekana kwenye arusi mlikuwepo sasa mmekula mmeshiba mnaanza kukandia !! hayo mambo ya ushauri mngewapa before ya wedding !!! kwani inaonyesha mnawajua sana hao watu!!sasa na wewe unasema ujapenda nguo ya bibi arusi wewe hina kuusu nini wenyewe ndo walivyo penda!! acheni uchaku bimbi !!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 28, 2010

    Ah! Bwana Ben Mashibaaa! Honera sana kiongozi wetu wa zamani. Naona soon unakuwa babu kwa mara nyingine tena. Hongera sana sana sana

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 28, 2010

    "Bwana harusi, marafiki zako wale mnaokutana nao kwenye bia iwe mwisho ndio mwanzo wa ugomvi nyumbani."

    hakika wewe anony wa kwanza uliyeandika hayo maneno ni punguani!!!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 28, 2010

    Haya sasa nasubiri kina kanyau walete hoja....

    nways hongereni sana Maharusi..

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 28, 2010

    Ushauri wa anon namba moja una walakini sana. Sijui kama unaweza kutoa ushauri wa aina hii kwa watu usiowafahamu kiundani....

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 28, 2010

    Mbona sijamwona, JK, Mama Pinda na Mama Salma !!!!!!!!!!! Au hawakualikwa kwenye harusi??? Mana kwenye send-Off Walikuwepo

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 28, 2010

    Hongereni mmependeza saaaaaana.
    Mungu awajaalie furaha tele na amani ktk nyumba yenu.
    Mnaoponda Wivu tuuu haujapenda gauni la bibi harusi wewe mgonjwa kweli bibi harusi kapendeza hivyoo!
    Tuoneshe harusi yako wewe ilikuwaje?

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 28, 2010

    Hongereni mmependeza sana.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 28, 2010

    Aisifiae mvua, imemnyea.
    Anon wa kwanza kama ni mwanamke basi bwana harusi alikua kitu chako na kama ni mwanaume bi harusi alikua kitu chako.
    Dhahiri kuna elements za wivu ndani ya ujumbe wako.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 28, 2010

    Niko tayari kukosolewa. Kwa sasa hapa Bongo ndoa za 'makaratasi' zishaanza kuja taratiiibu. Kuna wanawake wanaingia kwenye ndoa bila upendo wa dhati, sababu ikiwa hasa ni kupata 'recognition' na muda mwingine kupata mtu wa kumbeba hapa mjini, akishapata hilo karatasi ndo basi tena, inakuwa vurugu ndani ya nyumba, anashindwa kubeba nafasi ya umama kimajukumu nyumbani kwake, hataki kukosolewa n.k. Wanaume pia wanaweza kuwa na mapungufu yao pia, lakini ujumbe umefika.

    Nkyabo - Bongo

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 28, 2010

    we anoy wa kwanza ni mwongo mnafiki na mzandiki na ushauri wako wa kijijini

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 28, 2010

    yani umu bloguni/globuni:yani nikiwa na hasira gani au stress kibao
    nikija umu ndani basi naanguka tu cheko la kufa mtu!!yani apa mbavu zimevunjika kwa comments uko juu

    hahahahaaa tih tih tih!!

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 28, 2010

    hee heee heeeee NAKUBALIANA NA MDAU. KABISA NIKIWA NA STRESS HATA MIE NAINGIA HUMU MWENYE BLOGU YA MHESHIMIWA MICHUZI. Yani lazima naishia kucheka hata mood mbaya nilotoka nayo kazini inaiiiiisha.
    duh ' ETI HUYO MLULUGA ANASEMA HAJAPENDA GAUNI LA BI HARUSI, JAMENI WATU MKOJE? mwenyewe kalipenda kila mtu na style yake na fashion yake roho yake inavyopenda/
    NA YEEEES tunasubiri kina DAUDI KANYAU waje na MUTA RWAKATARE jee. heee heee heee. nimecheka sana na ushauri wa bure alotoa mmoja hapo juu jamani ni uko kijijini ama? Bwana harusi akome tena kwenda kukutana na rafikize kunywa bia ndio inaleta ugomvi nyumbani? hii kali jamani. MIE NAONA ANARUHUSIWA KUKUTANA NA RAFIKI ZAKE ILA ALINDE TU HESHIMA YA NDOA. Sijakubaliana na ushauri wako. mengine mazuri lakini mengine duh! haya naomba kuwakilisha, na Mheshimiwa Michuzi usiniminyie maoni yangu. Shukrani.
    bwana uongo BI HARUSI KAPENDEZA MNO.

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 29, 2010

    I know hata mimi nikija humu nafuatilia comments tu.. nimeona hii harusi nikasema imependeza kweli. nimependa royal blue color yao lakini wala sikukumbuka ni ile juzi tu tulilonyeshwa kuwa JK na Pinda walihudhuria. Nilivyosoma hizi comments ndio nikakumbuka.

    Mhhh kweli kuna chekesha sana humu. Inaelekwa watu wana uchungu sana hawa watu walivyooana. Na pia naona hata wenyewe walijua hili mpaka wakaamua kuwaonyesha vyeti vya harusi. Kuwa hakikishia kuwa sasa "tumeona"....

    Duh Bongo kweli tambarare...Kuna comments huku unaona kabisa mtu ana uchungu sijui wivu , sijui huzuni...Hey be happy mwenzio kaoa/kuolewa iko siku yako tu na wewe utapata mtu wako, kama na wewe utabebwa au utambeba mtu ndio maisha hayo don't act like a grumpy old lady.

    Hongera Mr and MRS Robert....Mungu awazidishie baraka...

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 29, 2010

    jamani huyo dada kapendeza na huyo aliyesema ajapenda nguo yake sijui anamaanisha nini. lakini mtu unavaa unachopenda na anavyoonekane ni kama yuko mjamzito vile labda ndio maana kavaa aina hiyo ya nguo. mdau wa texas

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 29, 2010

    jamani wenye wivu wajinyonge.Robert na mkeo mmependeza sanaaaa,hao wanaokosoa ni wivu tu unawasumbua mimi nilikuwepo na nimeshuudia live,maharusi walitoka mwaaa,ukumbi ulipendeza sana,vinywaji ushindwe wewe,watu full kupendeza,bi harusi full uchangamfu hadi raha,bwana harusi pia full kuchangamka,yani huyo anony wa kwanza hapo juu hanielezi chochote.kama huna cha kucoment si unyamazee.kwenye harusi yako ndo utafanya utakavo wewe.harusi ya robert na mkewe wamefanya wanavotaka wao sio unavotaka wewe!lako hiloooo!UTAJIBEBAAAA!(MFD)

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...