Mmoja wa Wanachama wa CCM Tawi la Mkambarani , Wilaya ya Morogoro , akiwa wamejitokeza kuweka udhamini wa fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM ya Rais Jakaya Kikwete
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Wilaya ya Morogoro vijijini kichama, Mohamed Mzee ( kushoto) akiwa miongoni mwa wana CCM 16 waliojitokeza kudhamini fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho. Mjumbe wa Kamati Maalum, Mariam Ukiwaona Ditopile Mzuzuri ( kushoto)akiikagua kadi ya CCM ya Mwanachama , Mzee Athuman Mohamed Dume ( kulia) wa CCM Tawi la Fulwe, Kata ya Mikese, Wilaya ya Morogoro kabla ya kukubaliwa kudhamini fomu ya mgombea wa kuomba kuteuliwa na CCM katika nafasi ya Urais wa Tanzania kwa miaka mitano
Mzee Sudi Sarah YanyeYange ambaye ni mwanachama wa CCM Tawi la Fulwe, Kata ya Mikese, Wilaya ya Morogoro akiweka saini yake katika fomu ya udhamini wa mgombea wa kuomba kuteuliwa na CCM kuogombea nafasi ya Urais wa Tanzania kwa miaka mitano , Rais Jakaya Kiwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa , baada ya kujaziwa maelezo na Mjumbe wa Kamati Maalum, Mariam Ukiwaona Ditopile Mzuzuri ( kushoto) zoezi hilo lilifanyika Juni 22, mwaka huu.
Juu na chini ni baadhi ya Wanachama wa CCM Tawi la Mkambarani , Wilaya ya Morogoro , wakiwa wamejitokeza kuweka udhamini wa fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM ya Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho, zoezi hilo lilifanyika Juni 22, mwaka huu.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 23, 2010

    Ankal, mbona hao wanachama wanaonyesha kadi zao za kupigia kura?nafikiri kwa udhamini kadi ya CCM ndio muhimu, hakuna namna hapo?tazama picha ya pili toka juu ya mohamed mzee.
    Politician

    ReplyDelete
  2. Dud! Eee Bwana Michuzi ee, huyo ni Mtoto wa Marehemu Bradha DITO?

    Duh! Kumbe alikuwa na Bint Mkubwa/Mzuri hivi.

    Daa! Nisalimie

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 23, 2010

    Wananchi wanatakiwa waelimishwe juu ya siasa,pia katiba ya nchi inatakiwa ifanyiwe REFORM.Sasa utadhamini vipi mtu ambaye hufamiani naye? Hawa Wadhamini labda hawajawahi kumuona huyo Jk vijijini mwao wanachajua ni ccm ccm.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...