Yusuf Ahmed Alley a.k.a Bwan'Chuchu
( wa pili kulia) akiwa na wenzie wa bodi ya Sauti za Busara
HABARI ZIMETUFIKIA PUNDE TOKA ZENJI ZIKISEMA KWAMBA MSANII MAARUFU WA HUKO VISIWANI YUSUF AHMED ALLEY MAARUFU KAMA BWAN'CHUCHU HATUNAYE TENA. HABARI HIZO ZINASEMA BWAN'CHUCHU AMEFIA JIJINI NAIROBI, KENYA, ALIKOKUWA AMEKWENDA KIKAZI. CHANZO CHA MAUTI YAKE HATUJAAMBIWA ILA IMETHIBITISHWA KWAMBA MWILI WAKE UMESHAREJESHWA ZENJI NA MSIBA UKO KWAO SEHEMU ZA KISIMA MAJONGOO NA MAZIKO YATAFANYIKA LEO SAA 10 KWENYE MAKABURI YA MWANAKWEREKWE.
BWAN'CHUCHU ATAKUMBUKWA KWA UHODARI WAKE KATIKA MUZIKI HASA ALIPOUNDA BENDI YA CHUCHU SOUND ILIYOTAMBA SANA KWA VIBAO VYAKE VIKALI NA CHAPUO ZA MAONGEZI KATI YAKE NA OMARI MKALI YALIYOKUWA YAKIHITIMISHWA NA NENO LA 'EE! KWAHERI'.
MAREHEMU CHUCHU PIA ALIKUWA MMOJA WA WAJUMBE WA BODI YA TAMASHA LA KILA MWAKA LA SAUTI ZA BUSARA NA PIA ALIKUWA ANAMILIKI STUDIO YA KUREKODIA MUZIKI PAMOJA NA STESHENI YA REDIO.
MOLA AIWEKE MAHALA PEMA ROHO YA MAREHEMU
-AMIN

Kusikia kimoja ya vibao vya Chuchu Sound BOFYA HAPA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 05, 2010

    Its a big loss...Chuchu..daima utakumbukwa na ndugu zako, marafiki zako, majirani zako na wapenzi wako wote...Nenda salama kaka..upumzike pema
    Inna lillahy wainna ilayhi iraji3un.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 05, 2010

    Du, tumempoteza msanii na kiongozi mzuri ktk tasnia ya burudani, tupo pamoja wafiwa na wapenzi wote wa Chuchu sound.

    Pia sijui hiki kitu kikali cha 'Tenda Mtende Nyie' kama kilitolewa angalau DVD/Video, maana kama bado, basi Omari Mkali jaribu kuvuta majeshi mkirekodi ktk DVD/Video kumuenzi mwenzetu Bwan'Chuchu.

    Mdau
    Muscat. Omanni

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 05, 2010

    OMG. May He Rest in Peace.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 05, 2010

    Duh, ama kweli hapa duniani tunapita tu. Yaani katutoka ghafla ghafla namna hiyo! Jamani, tuwe tayari wakati wote maana hatujui siku wala saa.

    Mungu akujalie pumziko jema Bwa'Chuhu! Poleni sana wana familia na wengine wote ambao mmeguswa sana na huu msiba wa ghafla!

    ReplyDelete
  5. Poleni wafiwa , mungu ailaze roho ya maremu peponi .. tumepoteza hazina kubwa katika maswala ya sanaa na habari

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 06, 2010

    Sisi watu wa hapa Washington state seattle tunakumiss tayari.Chuchu Mpenzi wetu,mwanetu,rafiki yetu, na kaka yetu Mungu akulaze mahala pema peponi.

    Watu wengi wa zanzibar wameondokewa jana na kiumbe,alikuwa mtu wa kufurahisha watu pia ni mcheshi.Tunatoa Pole kwa Familia yake yote kuanzia Mkewe Bi Laila na wengine wote.Kutasomwa Hitma hapa Bellevue siku ya jumatatu tarehe saba juni saa kumi jioni kwenye hall la wakina shaaban Moyo nyote mnakaribishwa mliopo hapa WA.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 06, 2010

    R.I.P. CHUCHU. Tunatoa mkono wa Pole kwa familia ya Chuchu yote Hasa mkewe Bi Laila.

    Hapa Bellevue WA state kutasomwa Hitima jumatatu tarehe saba june,ukumbi wa Moyo saa kumi jioni Watanzania na jumuiya yote kizanzibari mnalikwa kwenye kisomo.

    Tutamkumbuka chuchu kwa ucheshi wake na wema wake Mungu amlaze mahala pema.Amin.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 07, 2010

    Doh Michuzi Nuksi yaani bado unatuwekea muziki wake badala ya kumtakia maghfira.Mungu amlaze mahali pema peponi,safari yetu ni sote.Poleni sana wafiwa na mtakieni maghfira kwa sana,kama namuona vile tokea enzi hizo hadi leo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...