Gari aina ya Toyota Premio likiwa limetumbukia mtaroni katika barabara ya zamani ya Moshi-Arusha katika eneo la Moshono mjini Arusha baada ya kujaribu kuikwepa pikipiki aina Toyo inayolotumika kwa biashara ya kusafirishia watu maarufu kama boda boda iliyoingia kwa ghafla barabarani wakati ikiwa na abiria ambaye ni askari wa Jeshi la wananchi wa Tanzania.Katika ajali hiyo dereva wa gari ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja pamoja na wanafunzi wawili waliowapakia waliumia vibaya na kukimbizwa katika hospitali ya Mount Meru wakati mwendesha pikipiki na abiria wake walinusurika.pikipiki iliyosababisha ajali ikiwa imeingia kichakani.

(picha na Novatus Makunga)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 22, 2010

    Boda Boda naona zimekuwa kero. Zimekuwa zikisababisha ajali sana na sehemu nyingi hasa mijini. Nadhani sasa ni muda mwafaka serikali iliangalie hili jambo. Madereva wa boda boda itabidi wapewe mafunzo mazuri ya sheria za usalama barabarani na wapewe leseni. Vinginevyo wataendelea kusababishia ajali ambazo zinagharimu maisha ya watu na mali zao.
    Mdau

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 23, 2010

    hivi ni kwanini makandarasi wanojenga barabara za Tanzania bado hawazibi mifereji inayopitisha maji?; nauliza hivyo kwa sababu picha nyingi za ajali kwenye hii blogu zinahusu magari yanayotumbukia mitaroni.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 23, 2010

    Naona zote zina namba mpya, inaonekana ndo kwaanza walikuwa wanasafisha nyota barabarani.


    Nkyabo - Bongo

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 23, 2010

    Jamani na sisi wananchi tusikimbilie usafiri wa hizi boda boda, kama kweli kuna ulazima wa kutumia basi tumia lakini tuendelee tu na daladala zetu kwa usalama zaidi, yaani kwa akili ya upesi upesi ya kumsoma mtu ukiangalia vijana wengi wanaondesha hizi bodaboda si wazoefu, hawajatulia ki-akili wao wanachowaza ni kutengeneza pesa za haraka haraka bila kujali usalama wake na wa abiria, sasa mtu asiyejali usalama wake binafsi atajalije usalama wa abiria.??!! akili ku-mkichwa sio kila kitu tufundishwe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...