January Makamba akiwashukuru wananchi wa Bumbuli kwa imani waliyoonesha kwakeBaadhi ya wananchi wa Jimbo la Bumbuli wakimpongeza Bw. January Makamba, aliyepata ushindi wa asilimia 80.11 dhidi ya wagombea nane wengine, akiwemo Mbunge aliyemaliza muda wake Mhe. William Shellukindo.
kila mtu alitaka kumshima mkono kwa kumpongeza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 24 mpaka sasa

  1. Yaliyomo Yamo!

    ReplyDelete
  2. WADANYANYIKA BWANA, KAZI KWELI KWELI.

    ReplyDelete
  3. habari ndo hiyo,ule mchezo wa kulindana cm umeisha,sasa hivi ukishinda kura za wananchi ndo mgombea,sasa tutaona tanzania ya ukweli,maana tulikuwa tunaekewa watu ambao sio chagua la watanzania.nafurahi kuona vijana wengi wamepitishwa kwenye kura za maoni,na uhakika serikali ijayo vijana wa kumwaga,hatujali mtoto wa nani,tunataka vijana washike nchi na tusonge mbele.

    ReplyDelete
  4. hivi kwa nini na bara isiwekwe serikali ya mseto,rais JK,waziri Mkuu Pro lipumba,waziri wa utalii Slaa,zito kabwe madini,mrema mkuu wa mkoa.

    ReplyDelete
  5. keli vijana wanatakiwa washike nchi,kina vito kabwe na ismail jsa wa cuf chukuweni upinzani,muwatoe wazee kina Slaa,tunataka vijana pande zote,ccm wameonesha nia,wapinzani igeni.

    ReplyDelete
  6. HUYU JAMAA AKISHINDA UBUNGE AELEWE KUWA WAKINA MAMA NDIYO WALIOMPA NAFASI HIYO, KWA HIYO ASIWASAHAU KABISA.....JAMAA ANA SUPPORT KUBWA SANA YA AKINA MAMA....I HOPE ANALIELEWA HILI.. l like the guy though, jamaa ni mchapa kazi na pia ni msomi, na vile vile ni kijana mwenzetu - akiwa waziri fulani anaweza akabadilisha mambos anyways tutaona.

    ReplyDelete
  7. hivi huko kwa kina she-makamba mabati hawabadili maana yana kutu ili mbaya ? au ndo hali ngumu ya kiuchumi?
    Mdau
    Columbus.

    ReplyDelete
  8. ALL THE BEST JANUARI. IHAVE READ YOUR BOOK AND IF YOU MEAN WHAT YOU HAVE WRITTEN, THEN BUMBULI WILL BE HAVEN OF PEACE. CONGRATULATIONS IN ADVANCE. BUT I PRESUME YOU WON'T BE LEADING THE CONSITITUENCY USING A REMOTE CONTROL, BUT RATHER YOU WILL TAKE MORE OF YOUR TIME WITH THE PEOPLE OF BUMBULI, TRY TO SOLVE THEIR SOCIO-ECONOMIC PROBLEMS. AVOID WORDS. PUT WORDS INTO ACTIONS. THE ITALIANS HAVE A SAYING THAT GOES--- IN BOCCA A LUPPO, MEANING ALL THE BEST. YOU RESPOND BY JUST SAYING 'CREPI'.
    Mdau DAILY NEWS.

    ReplyDelete
  9. Watanzania tusipumbazwe na watu wenye tabia ya "Superiority Complex"

    Huyu February kwa mtanzamo wangu ni mtu wakupenda kujikweza

    ReplyDelete
  10. Nasikia kichefu chefu haya majina yakiwa yanataka kuendelea kutajwa tajwa mara baba mara mtoto ...

    Tanzania ni yetu sote na Mungu ni wetu sote si Wa FAMILIA YENU TU

    ReplyDelete
  11. Obama aliandika kitabu ...eti na yeye kaandika kuhusu watu wa Bumbuli wakati kule yeye si mkazi ...

    Hahahahahaa

    Wananchi wa Bumbuli Zindukeni ...CCM wameshindwa kuweka mtu anayewafaa mwaka huu (HUYU JANUARY ANAIGA HAIBA YA MTU FULANI TU HANA LAKE JIPWA)


    Bumbuli must go for another person and not January Makamba

    Januari anatafuta Umaarufu tu hasa kupitia mgongo wa babake

    ReplyDelete
  12. natamani nipate matokeo ya kwetu kasulu... maana kuna maaskofu pia ambao wameacha kofia (ganda la chungwa) wakahamia kwenye siasa.... kweli ubunge ni mtamu. Wakipita vijana wa Kasulu itakuwa poa sana: kasulu itakuwa sambamba na Bumbuli kwa vijana.

    ReplyDelete
  13. Noana lile kundi la wabunge wapiganaji linasambaratishwa kirahisi sana ,nasikia Seleli nae pia katupwa nje.

    ReplyDelete
  14. Hizo ni kura za maoni. Majina yanapelekwa kwenye halmashauri kuu ya CCM. Shellukindo atashinda

    ReplyDelete
  15. huyo mtoa maoni hapo juu aliyesema bara iwekwe serikali ya mseto na mrema awe mkuu wa mkoa , kanoa hapo , yaani mrema alivokuwa na madaraka alikuwa ni miamri yake ya ajabu ajabu tuuu , watu walikuwa hoi , mara leo katoa amri hivi watu lazima wafuate mara akilala akiamka mara hivi , sijui zilikuwa amri za mkewe ! maana kila siku zinabadilika .. mrema akishika madaraka nahama nchi ...hatumtaki kasha expire

    ReplyDelete
  16. Jina la January kiboko kweli, yaani watu wanaitwa Mwezi wa Kwanza. Lakini Afrika Kusini pia kiboko, kuna Tokyo Sexwale, jina linanikosha sana hili kuliko yote.

    Je, kuna February na December pia?

    ReplyDelete
  17. Kuleana peter (Japan)August 02, 2010

    Hongera makamba.
    Dr Hildebrand shayo na John Mashaka mko wapi?????
    Au ndiyo mmemtanguliza makamba katika ile asma yenu ya mwaka 2015?

    Hongereni vijana

    ReplyDelete
  18. Kwa bara kama ni serikali ya mseto Slaa ndiye waziri mkuu kwa sababu kaonyesha uwezo mkubwa wa kufichua kshifa nyingi kuliko Lipumba pili Slaa anauzoefu bungeni kakaa zaidi ya miaka 15 wakati Lipumba hajawahi kuwa hata mbunge tatu litakuwa jambo si la haki yaani Rais,Makamu wa Rais, Waziri Mkuu,Rais wa Zanzibar, Waziri Kiongozi wote waislamu katika nchi ambayo wakristo na waislamu ni nusu kwa nusu itakuwa ni ukosaji wa maarifa Lipumba atafaa kuwa waziri wa fedha. Mrema mambo ya ndani

    ReplyDelete
  19. US Blogger naye kashinda ama vipi?

    ReplyDelete
  20. Ukiangalia kwa umakini utaona kwamba inajengwa ngome kuu ya kulinda na kutetea maovu na wizi serikalini. Hakika sasa imefika wakati maana ya siasa tuipitie upya kwani imefanana na uwekezaji binafsi. Kusikia fulani kaula ni kawaida kwa sisi.Kwa siasa hizi najuta kua mtanzania maana wakati wenzetu wanapigania uchumi si twapigania posho na dili za siasa

    ReplyDelete
  21. welldone bumbuli labdha this time kutakuwa na maendeleo kwenye jimbo langu la bumbuli. Yangu macho keep what you have promised us January hatutaki Febuary

    ReplyDelete
  22. Akimaliza huyo mda wake wa kula nchi atakayefuatia ni February Maminyororo.Huyo ndo watang`oa na mabati yenye kutu waezeke na makuti mana Duh?Mi naona wizi mtupu hamna lolote kutoa CCM na kuirudisha hiyo hiyo.

    ReplyDelete
  23. Kweli bongo mambo tambarare yaani jamaa haoni hata aibu sehemu anapo hutubia panatia huruma wakiingia madarakani ni kula feza wapiga kula wanabaki vile vile tangu nizaliwe mpaka na zeeka nchi hiko vile vile....
    kidumu chama cha mapinduzi!!!!!
    Mpenda nchi

    ReplyDelete
  24. Duh, salaaaaalllehh! Yule mama mwenye kilemba kafuraaahi true true utadhani kaambiwa atagawiwa posho atakayopata mbunge mtarajiwa. Utadhani kaambiwa hatakufa kamwe! Mweeeeh. Job Is true true (Kazi iko kweli kweli)!!

    Chiazi Mchizi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...