Mji wetu mkuu Dodoma unazidi kupanuka na kuwa na nyumba nzuri na za kisasa. Hapa ni maeneo ya uwanja wa ndege kama ulivyonaswa leo na Globu ya Jamii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Mimi naona hizo barabara wangeziwahi ziwe pana kabla hakujageuka kuwa Dar...Miaka kumi ijayo basi kutakua kama dar vile na vibarabara vyake vyemabamba. Umeona wenzetu barababara zao zilijengwa miaka ya 1900 na ziko hivi ...sisi tunajenga leo tubarabara huto tudogo hivyo...

    ReplyDelete
  2. Ama kwa hakika jiji limekamilika, sishangai kulifananisha na jiji la District of Columbia

    ReplyDelete
  3. MJI MKUU jina tu, hakuna juhudi za maksudi zilizofanyika ili kulifanya angalau kuwa jiji. Mji mkuu wa kisiasa tu, watanzania bwana, we acha tu, maneno meengi lakini vitendo kidogo. Watu wanafaidika toka mwaka sitini na ngapi sijui kwa jina la kuendeleza makao makuu mpaka leo!!! Inauma sana kwa kweli!!! Nchi hii kama wapo wakereketwa haswa na yao basi ni wachache kweli.

    ReplyDelete
  4. N kweli kama serikali imeshindwa kuhamia Dodoma iseme tu wala isione aibu kuwa imeshindwa kuhamia Dodoma! Kuhamia Dodoma sio kipaumbele bali kampeni za kuingia Ikulu na kushika madaraka ndicho kipaumbele! Makao makuu gani yanajengwa karibu sasa nusu karne!! Serikali ihamie Dodoma ipungue hata foleni ya magari Dar.

    ReplyDelete
  5. kama kawaida mipango miji yetu bado ipo 1900. Mji mkubwa una barabara mbili ambazo hata pikipiki zinashindwa kupishana.

    ReplyDelete
  6. Sisi tulio wazee wa siku, tunajua kuwa Dodoma ilijengwa kwa ajili ya baiskeli!

    ReplyDelete
  7. Tatizo la watanzania ndio hilo, Mji ni miundombinu na plans za maana sio tu majumba ya vigae na barabara za 'baiskeli'.. Inabidi serikali iongeze juhudi za kuboresha miundombinu iendane na hadhi ya Dodoma kuwa mji mkuu.
    Afterall hayo ndio majumba ya pesa zenu za EPA.

    Mimi

    ReplyDelete
  8. kwa nini usituletee maeneo ya majengo ambapo walalahoi wanaishi, dodoma inapendwa na wale waliozaliwa hapo, huu mji unapendeza sana, ukitazama reli ya kati inapasua kati-kati ya mji hapa wametoka wanariadha maarufu kama vile Sunday manara,Kassim manara,Lila shomari,mohamed omar nyange,Hassan gobos,Ali mwanoga,Mohamed saleh(rip) Omar amani,Hussein gobos,Osman matata, bila kuwasahau kimolos family n.k. mdau usa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...