Uwanja wa Amaan Stadium, Zenji, unavyoonekana leo baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa ambapo tayari zuria la riadha limeshawekwa na nyasi mpya kupandwa huku majukwaa yote na kuta yakiwa yamepigwa rangi na sehemu za mapumziko na maliwato kutengenezwa. Hoteli ya Amaan iliyoko pembezoni nayo haijasahaulika na sehemu hii sasa inatoa taswira njema. Uwanja huu, unaotarajiwa kufunguliwa mapema mwezi ujao, umekuwa hautumiki kwa muda kutokana na ukarabati huo. Hivyo michezo yote, hasa mpira wa miguu, ilihamia uwanja mkongwe wa Mao Tse Tung.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Bado sijafika Zenj, kumbe stadium yao ni sawa na uwanja wa mpira wa wilaya ya Bumbuli, duh makubwa hayo, ndo maana sherif ananadi sera za kujenga kakiwanja ka kisasa, mpeni kura basi abadilishe huo uwanja wa Bumbuli.

    ReplyDelete
  2. Ok bora usifike maana nyie huko ndio kwanza Juzi mmepata uwanja wakati wenzenu wana uwanja wa maana tu siku nyingi.Kabla ya uwanja wa NESHINO kulikua na uwanja gani wenye majukwaa upande mmoja tu!!! Ushike adabu yako!!!! SAFARI HII UWANJA WA NDEGE WA TAIFA UTAHAMIA ZENJI MAANA KILA KITU CHA TAIFA KIPO BARA..

    ReplyDelete
  3. Naona uwanja huo kwa bara unaweza kuulinganisha na ule wa Karume, sijui mashabiki elfu thelethini kama unaweza chukua. Nashauri mjenge kama ule wa Majimaji-Songea au Alhasan Mwinyi-Tabora itavutia wengi kuingia vinginevyo unavyoonekana inanipa wasiwasi kama nitapata nafasi ya kukaa, naona kama kuna mistari si zaidi ya kumi kwenye safu ya mzunguko

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...