Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge William Lukuvi akiongea na ujumbe wa wawekezaji wa mradi wa uzalishaji umeme wa Liganga na Mchuchuma kutoka China wakati wa hafla ya chakula iliyoandaliwa na makampuni ya China leo kwa lengo la kuwekeza katika uzalishaji wa umeme ambapo amesema kuwa serikali imeshawapa maelezo ya kutosha yatakayowawezesha kuja nchini kuwekeza kwa wakati.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge William Lukuvi akimkabidhi zawadi ya kinyago mwenyekiti wa ujumbe wa wawekezaji na Mwenyekiti wa Bodi ya wawekezaji hao Mr. Liu Chang Long wakati hafla fupi ya chakula iliyoandaliwa na makampuni ya China kwa lengo la kuwekeza katika uzalishaji wa umeme nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Mary Nagu akiongea na ujumbe wa wawekezaji wa mradi wa uzalishaji umeme wa Liganga na Mchuchuma kutoka China utakaojengwa kwa ushirikiano na serikali ya Tanzania wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na makampuni ya China leo jijini Dar es salaam.

Ujumbe wa wawekezaji kutoka China na baadhi ya viongozi kutoka Tanzania wakishriki hafla fupi ya Chakula iliyoandaliwa na makampuni kutoka China yatakayokuja kuwekeza katika mradi wa uzalishaji wa umeme wa Liganga na Mchuchuma.
Ujumbe wa wawekezaji kutoka China na baadhi ya viongozi kutoka Tanzania wakishriki hafla hiyo fupi ya Chakula. Picha na Aaron Msiga wa MAELEZO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...