Rais wa Kampuni ya RBP Oil & Industial Technology (T)Ltd ,Mama Rahma Al Kharous akizungumza na wanahabari leo juu ya udhamini wake wa shilingi mil. 30 kwa ajili ya ukarabati wa msikiti wa Al - Auwariyya uliopo eneo la Gongoni,Bagamoyo.
Unavyoonekana msikiti huo hivi sasa kwa upande wa mbele,ambao ndio msikiti wa kwanza kujengwa katika mji wa Bagamoya ukiachana na ile iliopo kule Kaole.Msikiti huu ulijengwa mwaka 1889 na kuufanya kuwa ni moja ya sehemu za historia katika mji huo.
Sehemu ya nyuma ambayo imeshaanza kuanguka kutokana na kukaa kwa siku nyingi.
Mama Rahma Al-Kharous (katikati) akiwa na viongozi wa msikiti ambao ni Sheikh Abdul Rahman Bura (pili kushoto) na Mweka hazina wa Msikiti huo,Sheikh Mohamed Shariff (pili kulia) pamoja na kijana aliekuwapo msikitini hapo.
Mama Rahma Al - Kharous (katikati) akiwa na baadhi ya ndugu zake alioongozana nao leo kwenda kuuona msikiti huo.toka kushoto ni Mama Rahma Ibrahim,Sharifa Ismail,Amina Kasiga pamoja na watoto wao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. ukijenga nyumba ya allah hapa duniani yeye atakujengea huko akhera.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...