Marehemu Mwalimu Innocentia Banzi

Familia ya Michael Gomela wa Reading-United Kingdomo, inasikitika kuwatangazia msiba wa Mwalimu Innocentia Banzi (MAMA YAKE MZAZI MICHAEL GOMELA) kilichotokea alfajiri ya tarehe 12/01/2011 Dar-es-salaam-Tanzania.

Marehemu ni mama wa: Dennis Londo wa Helsinki-Finland; Esther Londo na Walonzi Tatala wa Tampere-Finland; Michael Gomela wa Reading-United Kingdom; Daniel Mtebe wa Stockholm-Sweden.

Habari za msiba huu ziwafikie wakuu wa shule zote za sekondari Tanzania, walimu na wanafunzi wa Kilakala sekondari, Morogoro sekondari na Masanze sekondari. Pia ziwafikie wanachama wote wa chama cha msalaba mwekundu Tanzania; wanachama wote wa chama cha maskauti Tanzania na wanamichezo wote wa Mkoa wa Morogoro.

Mazishi yanatarajiwa kufanyika Morogoro mara tu watoto wa marehemu watakapowasili.Mr Michael anahitaji msaada wenu wa hali na mali ili aweze kuwahi mazishi ya mama yake.

Wale wote ambao mpo Reading Berkshire Msiba upo

48 Surley Row

Emmer Green

Reading

RG4 8NA:

(kwa maelezo zaidi piga simu +44 7872953835 kupata direction)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Poleni kina Walonzi na familia ya Tatala, mungu akupeni faraja katika kipindi hiki kigumu cha mpito. May almighty God Rest the soul of your beloved in Peace.
    B. Kaluwa

    ReplyDelete
  2. Dennis na ndugu zako, poleni sana n msiba huu mzito. I know how difficult this is, please be strong and may you find peace and comfort during these hard times.
    Mungu ampumzishe mama

    Mdau Godfrey,
    USA

    ReplyDelete
  3. Poleni sana ndugu na Familia!
    Huyu alikuwa mwalimu wangu kama sikosei pale Morogoro Secondary, nimemkumbuka nilipoona tu picha, but it was sad after reading what happenned!

    Gone too soon Mwalimu!

    RIP

    ReplyDelete
  4. RIP my sister,tutakukumbuka milele.Grace

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...