Jumuiya ya watanzania waishio nchini Switzerland (TAS-Tanzanian Association in Switzerland) usiku wa tarehe 30 mwezi April 2011 waliandaa harambee kwa ajili ya kutunisha mfuko wa chama ili kupata uwezo wa shughuli mbalimbali kama ilivyoanishwa katika katiba ya Umoja wao, ikiwemo elimu kwa ajili ya wasiojiweza. Sherehe hiyo ilifana sana kwani ilihudhuriwa na watu zaidi ya 200 wa rika tofauti kutoka mataifa mbalimbali duniani.

Wageni waliohudhuria walipata nafasi ya kujionea na kununua vitu mbalimbali kutoka Tanzania vikiwemo khanga, vitenge, vinyago, tingatinga na vitu vingine vinavyoonyesha utamaduni wetu wa kitanzania. Pia waliweza kula chakula kizuri cha kitanzania kilichoandaliwa na wana-TAS. Sherehe ilinoga zaidi kutokana na dansi la nguvu lililoonyesha staili ya ‘’mduara’’ iliyowavutia sana wageni kutoa mabara mengine.

Kama mdau niliyehudhuria nilifurahishwa sana jinsi sherehe hiyo ilivyoandaliwa na utaratibu mzima wa shughuli ulivyokuwa. Napenda kuchukua nafasi hii kuushukuru Uongozi wa TAS, wanaTAS wote pamoja na wote waliohudhuria kwa umoja na ushirikiano wao kuweza kufanikisha harambee hiyo. Mungu ambariki kila mmoja wenu . Ni wazi kuwa watu wanapenda kuweka vikwazo vingi katika uanzishwaji na ustawi wa jumuiya za kitanzania huku ughaibuni na wanasahau matunda mazuri ya kuwa na umoja.

Napenda kutoa changamoto kwa watanzania walioko Uswiss kuendeleza mshikamano huu kwani kutokana na matukio kama haya watu wanazidi kufahamiana na ndipo wanaweza kusaidiana na pia kuwaachia urithi mzuri vijana na watoto wao wanaokulia ughaibuni. Pia napenda kuwashauri watanzania ambao wako popote pale nje ya nchi waendeleze mshikamano ambao utaweza kuwaweka karibu zaidi na kuweza kusaidiana katika mambo mbalimbali ya kijamii. Nina imani kipato kitakachotokana na harambee hii kitawasaidia kufikia malengo yao na kwamba kidogo watakachotoa kusaidia kule nyumbani kitaamsha ari ya wengine kuiga mfano huu mwema.

MUNGU IBARIKI TAS, MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Mdau Uswiss.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 06, 2011

    haya ndo mambo tunapenda kuona. Hongereni wabongo uswiss.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 06, 2011

    Hongereni sana, haya ndo mambo siyo yanayoendelea huku niliko, mnaonekana mko so organised. I love it, mmenikumbusha mbali sana enzi nikiwa Tz na huu wimbo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...