Marehemu Timothy Eugen Haule
Mpendwa Baba yetu Leo tarehe 25/07/2011umetimiza Miaka Mitano (5) tangu Mungu alipo kutwaa kwake Mbinguni.
 Ulikuwa Nguzo na msaada wetu mkubwa kwetu sisi wanao na familia kwa ujumla tunakukumbuka kwa mengi mpendwa baba yetu kwani ucheshi, hekima na busara zako tutazienzi daima.Pengo ulilolicha kwetu ni kubwa mno ila kwa nguvu za kristo tumesimama imara. 

Unakumbukwa sana na Mke wako Mpenzi Mrs. Josephine Haule, watoto wako Dorah,Sophia, Beatrice, Magreth, Oliver, Juliana, na Suzan. wakwe zako Gereson, Zawadi, Anikija, na Deo Pia unakumbukwa na wajukuu zako Elinory, Jenice, Victoria, Asharose na Abdieltimothy Kaka, Dada zako na ndugu jamaa na Marafiki, Majirani zako waOceanroad Flats.Tunajua kimwili hauko nasi ila kiroho tuko nawe daima baba mpenzi

Kutakuwa na misa ya shukrani nyumbani kwa Marehemu T. E. Haule 
Ocean road Flats leo  Jumatatu Tarehe 25 Julai, 2011 saa 11 jioni na nyote mnakaribishwa.

RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA MWANGA WA 
MILELE UMWANGAZIE APUMZIKE KWA AMANI
AMEN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...