Bwana afya wa soko kuu la manispaa ya songea aliyefahamika kwa jina la Mchata akiwasihi wafanyabiashara wa soko kuu la Songea kuacha mgomo wao walioanza jana wakigomea kuongezeka kwa ushuru,
Magunia ya mchele yakiwa yamefunikwa kufuatia wafanyabiashara wake kugoma kutoa huduma hiyo wakigomea ongezeko la kiwango cha ushuru wanaotakiwa kutoa kwa halmshgauri ya manispaa ya songea,ambapo umeongezeka kutoka tshs 200 hadi 400,
Meza za wafanyabiashara zikiwa tupu bila bidhaa yeyote kufuatia wafanyabiashara hao kugoma baada ya kuongezewa ushuru na manispaa ya songea kutoka tshs 200 hadi 400,
Hakuna mtu leo sokoni
Mpaka kieleweke
Baadhi ya wafabiashara wa soko kuu la songea wakiwa hawajui la kufanya kufuatia mgomo mkubwa wa wafanyabiashara hao wakigomea kuongezeka kwa ushuru katika bidhaa zao kutoka tshs 200 hadi 400 bila manispaa kuzingatia aina ya biashara.
Picha na Muhidin Amri wa Globu ya Jamii, Ruvuma
Hii ni uonevu mkubwa kwa wafanyabiashara. Sio haki kabisa kwa manispaa kupandisha ushuru 100%.
ReplyDelete