Leo natimiza miaka sitini tangu kuzaliwa. Huu si umri mdogo, nami namshukuru Muumba kwa kunipa fursa ya kuwepo ulimwenguni kiasi hiki. Ninavyokumbuka maisha yangu, ninatamani kama ningekuwa nimefanya mengi na makubwa zaidi kuliko niliyofanya kwa manufaa ya wanadamu. Ninatamani kama ningekuwa nimejiepusha na mabaya, nikawa mtu bora wa kupigiwa mfano. Lakini haiwezekani tena kuirudisha miaka iliyopita. Bora niangalie mbele, nijaribu kufanya bidii zaidi, ingawa sijui nimebakiza miaka mingapi hapa duniani.


Kumtembelea Prof Mbele BOFYA HAPA



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera profesa kwa kutimiza miaka 60, tunatazamia umefanya uvumbuzi wa kutuletea maendeleo katika nchi yetu!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...