Ankal na wadau wa globu ya jamii, wajameni habari za swaumu! (Na magari yetu pia naona yanafunga mwaka huu! Magari yote ya wadau Ramadhani Kareem!).
Ankal tafadhali nifikishie swali au hoja yangu hii, chonde chonde sana! Mimi ni Mtanzania wa kawaida mwenye elimu ya kawaida ya kuhesabia hela zangu niliyosoma kwenye shule za umma bila manjonjo makubwa sana. Nimefikiria nikashindwa kuvumilia; naona niulize wadau. Hivi kweli watanzania wenzangu, especially wajuvi wa mambo waliobobea kwenye biashara, uchumi, mainjinia nk: Hivi tangu tupate uhuru, nchi yetu (kwa maana ya serikali) haina rasilimali au uwezo wa kufanya moja au mawili kati ya haya? (Tafadhali tuelimishane michakato ya kufwanya haya mambo inafwananaje).
Moja: Hivi inaingia akilini kuwa Bongoland haiwezi kuanzisha mradi madhubuti wa kuzalisha umeme hata wa MW 2000 (ukaungana na hivi viMW 700 tunavyokimbizana navyo kila msimu vya maji na mafuta) kwa kutumia gesi tuliyonayo.
Mradi huu hauwezi kuanzishwa na serikali kwa 100% kisha ikatolewa IPO umma na wafanyabiashara wakanunua hisa kuongeza mtaji na kutoa umiliki wa serikali ili kupunguza mzigo na majukumu, labda wanaweza kubaki na 41%. Huu mradi hauwezi kuwa shirika la kuzalisha umeme, na kuua uhodhi na mzigo kwa TAANESKO kwenye umeme?
Ndugu zangu mi ubongo umekataa kabisa kuamini kwamba hatuwezi kufanya hili, 50 yrs after self-rule. Na gesi sio kwamba bado tuna.explore, ipo tayari ya kutosha tu.
Mbili: Kama hapo juu, hivi hatuwezi kwa 100% kuanzisha kampuni ya kitaifa ya kusambaza mafuta ikashindana na hawa walafi wa faida katika miji yote mikubwa nchini kisha ikatolewa IPO umma na wadau wakajinunulia vishea vyao, mtaji ukakua na serikali kubaki na kama 41 au 35% hivi?
Mradi huu ukawa na hifadhi ya kitaifa ya mafuta kwa nyakati za shida (strategic oil/fuel reserve). Hivi kweli mpaka kufikia hapa tangu tujitawale hatuwezi hili? Na wasomi wanataaluma kibao wapo tu? Na rasilimali zote zipo?
Ankal na wadau, nimejaribu sana kuona kwamba haya mambo mawili (mfano mdogo wa mengi tu!) hayawezekani tena kwa vingizio na ekskyuzi zote kuanzia za siasa uchwara na uoga wa kuonekana manunda kwa waliotakiwa wafanye haya, lakini kichwa changu cha mtanzania wa kawaida aliyesoma kawaida kimekataa kabisa kukubaliana. Tafadhalini wadau, hivi kuna wengine vichwa vyenu vibishi kama cha kwangu?
Mbongo pyua, ndani mpaka nje!
KAMA MDAU UNAJIULIZA MASWALI HUPATI MAJIBU, NGOJA NIKUONGEZEE MAELEZO MENGINE ILI UCHANGANYIKIWE KABISA. TANZANIA INAONGOZA DUNIANI KWA KUWA NA VIONGOZO WASOMI WENYE SHAHADA YA UDAKTARI UKIANZA NA RAIS, MAKAMO WAKE, RAIS WA ZANZIBAR NA ASILIMIA KARIBU 70 YA BARAZA LA MAWAZIRI PAMOJA NA VIONGOZO WENGINE WA NGAZI ZA JUU. TUNAO MLIMA KILIMANJARO, MADINI, GESI, MBUGA ZA WANYAMA, ARDHI YENYE RUTUBA. HAKUNA NCHI YENYE RAIS MWENYE SHAHADA YA UDAKTARI KATIKA G-8, EUROPEAN UNION, NATO NA SHIRIKA LA KUJIHAMI LA MAGHARIBI. PAMOJA NA UTITIRI WA MADAKTARI KATIKA UONGOZI WA JUU, WATANZANIA NI MALOFA KULIKO HATA VILE VI-NCHI VINAVYOTUZUNGUKA TULIVYOVISAIDIA KUPATA UHURU NA AMBAVYO HAVINA RASILIMALI KAMA SISI WALA VIONGOZI MADAKTARI. KUTOKANA NA UTAFITI UHUO, KWA MAONI YANGU, NI KUWA TANZANIANS, INCLUDING MYSELF, ARE "VOLUNTARY STUPID". NOW WE PROBABLY LEARN STUPIDIY THROUGH OUR EDUCATIONAL SYSTEM, OR I'M SORRY TO SAY THAT WE WERE BORN STUPID. I KNOW I'VE GOTTEN INTO A LOT OF PEOPLES'NERVES. BEFORE CRUCIFYING ME, PLEASE GIVE ME A LOGICAL REASONING AS TO WHAY YOU ARE RIGHT AND I'M JUST AN IDIOT.
ReplyDeleteUNAFIKIRI KUZALISHA UMEME NI SAWA NA MRADI WA KUPIKA VITUMBUA? TENA UNAONGELEA SERIKALI IZALISHE MEGAWATI 2000, ETI TU MATAJIRI TUNA RASILIMALI?
ReplyDeleteQUICKLY GET DOWN YOUR HIGH PEDESTAL, hata hao wanaokuja kuwekeza kuzalisha umeme wanakopa pesa kutoka mabenki makubwa tena mamilioni ya dola za kimarekani yanatumika kuzalisha megawati 100. Serikali ama ikope pesa ama iongeze kodi ili ipate mtaji wa miradi. Na kwa jinsi ninavyowajua wabongo kwa ujanja ujanja mnataka serikali izalishe umeme kama huduma wakati mitambo inatakiwa kuwa maintaned, wafanyakazi walipwe mishahara na madeni yalipwe.
Nyie mkitaka umeme wa uhakika lazima muwe tayari kuulipia kama wanavyofanya wenzenu kwenye nchi zilizoendelea, kodi unakatwa kubwa na umeme unazalishwa na makampuni ya binafsi yanaoendeshwa kibiashara ukiutaka unanunua kama bidhaa nyingine.
Pili umeongelea eti serikali izalishe megawati 2000, wakati mahitaji ni megawati zinazokaribia 1000, hivi unafikiri hiyo ziada nani atailipia? Umeme sio kama vitumbua au sambusa ukibaki utauweka kwenye friza utumie pale ukiwa na shita, unaozalishwa lazima utumike muda ule ule au uzime mitambo ili uzalishe mahitaji yako tu.
wacha niishie hapa ndio kwanza nimemaliza kufuturu nitarudi tena baadae!
Mdau wa pili anaeendelea kufuturu amejaribu kukuonyesha kuwa si kazi rahisi kama mradi wa kuuza chips barabarani, ni kweli. ila pia niongeze kuwa ni kweli si rahisi ila hatujaonyesha jitihada za makusudi za kupigana na tatizo hili na pia niseme kuwa uongozi hauna connection na kisomo kikuuuuuubwa kama hao madaktari wanaoganga njaa.nchi yetu ingetumia hao madakitari kuinjinia viongozi kwa kukuna vichwa kwenye research ambazo zinaendeleza nchi badala yake wameona ni heri udaktari wao ujikite kubobea kwenye ufisadi kwa kuwa siasa za kichovu tanzania hazimpi nafasi msomi makini kuifanya familia ifurahie matunda.Hii nchi yetu isahau kabisa issue ya maendeleo bila kurudi nyuma na kufund research zitakazotoa manufaa mnashindwa kujua kwa nini kila mradi unaoundwa na serikali unaishia kuwa bomu la maangamizi kwa watanzania.Ni kwa kuwa wanasiasa ndo wanafanya maamuzi tenda wakiwa aidha majukwaani,majumbani mwao au wakiwa na pressure ya umma utaalamu umewekwa nyuma.kwa kila aliyepitia DS vyuoni analijua hili samahani nilishasahau kituo cha utafiti sayansi kilikuwa kinaitwaje ila mojawapo ni kuwa wanasiasa wameua kwa kuwa hawataki kupeleka pesa huko ya kutosha.
ReplyDeleteUdaktari ni majina tu tena kama hao waliopata udaktari aidha kwa nyadhifa zao ndo maangamizi kabisa.kwani Kagame mnajua elimu yake ni kiwango gani?Ni daktari gani anaweza kusimama nae?madaktari wasiomaintain status zao?hao wanatakiwa wawe wanatupublishia kila wakati si kugombania ufisadi kwenye siasa uchwara.
Mdau wa pili ulimaoliza kufuturu; kama huna la kuongea kaa kimya.Pili inaelekea hujasoma vizuri mtoa maoni kasema nini. Mtoa maoni nakupa hongera kwa maoni yako mazuri, wengi wana mawazo kama yako, tatizo tumekuwa 'stagnant'. Mimi binafsi nafahamu wananchi wengi wenye uwezo wa kuiendeleza nchi yetu ikafikia pazuri zaidi. Tunao wakandarasi wazuri mno na watu wa kila fani. Tatizo ni wachache wenye nafasi za juu wameshikilia kila kona, kwa manufaa binafsi. Pia, wapo wenye uchungu kama wewe na mimi lakini wakipata nafasi 'wanajiachia', wanajisahau na kujiunga na hao wachache, mimi na wewe tutaendelea kunung'unika daima. Kinachosikitisha zaidi ni 'natural resources' zetu zinapotea taratibu na hakuna tunachonufaika zaidi ya vijisenti, vizazi vijavyo ndivyo vitakuja kuhangaika. Hakuna maana ya kutumia mamilioni ya pesa kualika wawekezaji kama 'Infrastructure' yetu bado mbovu. Uchumi utakua vipi kama umeme umekuwa wa mgao tangu nazaliwa na nina wajukuu. Maji tuwashukuru wachina(baadhi ya maeneo ya Dar), sisi kilitushinda nini kufanya walichokifanya wao? Kama wabunge wachache walio-raise issue bungeni siku chache zilizopita: Nafasi za kazi zitajazwa na wageni kana kwamba hakuna wananchi wenye elimu/uzoefu, natural resources zitazidi kuondoshwa 'and in return' tutapata 'almost nothing. Tungekuwa tunajivunia na dhahabu yetu hasa kipindi hiki ambacho masoko ya dunia yanayumba, tungeuza mno na uchumi wetu ungeinuka mno.
ReplyDeleteNCHI IKIWA NA WASOMI KAMA ANONYMOUS # 2 WA 11:39 IMEKWISHA. AMEKIRI KUWA WATANZANIA HATUWEZI KUFANYA CHOCHOTE MPAKA TUWEZESHWE. TUNAWEZA KUPIKA VITUMBUA TU, INGAWA HUKUSEMA KAMA NI KWAAJILI YA EXPORT AU DOMESTIC USE. NA WENZETU WANGESEMA WANAWEZA KUTENGENEZA DOUBLE CHEESE BURGER TU, WANASUBIRI KUWEZESHWA ILI WATENGENEZE INTERNATIONAL SPACE STATION, LEO HII USINGEKUWA NA CELPHONE WALA INERTNET YA KUINGIA GLOB YA MICHUZI.
ReplyDeleteHAWA NDIO WALEWALE WASOMI WENYE UELEWA, UJUZI, UTAALAM NA MPAKA LUGHA ZA PLASTIKI. KILA KITU HATUWEZI, KILA KITU EXCUSES! HAPO UTAKUTA JITU LINA DEGREE YA BURE YA NYERERE AU YA LOAN BOARD BADO ANALINGANISHA HOJA HII NA UUZAJI VITUMBUA. YANI HII NCHI BANA, NDOMANA TUKO HIVI. KITU RAHSI SANA KINAONEKANA KIGUMU WAKATI KILA KITU MNACHO. IT DOESNT MATTER MTAJI UNATOKA BENKI KUBWA AU NDOGO AS LONG AS KUNA NIA YA DHATI YA KUFANYA HAYA. WADAU WOTE MLIO NA MTAZAMO HASI NDO MNAIANGUSHA NCHI HII. SASA JITU LINAKURUPUKA NA KUSEMA TUNAHITAJI MW 1000 TUSIZALISHE ZAIDI, HIYO AKILI AU UMEROGWA? KWANI ETHIOPIA WANAOTAKA KUZALISHA MW 40,000 SIJUI KWENYE HUO MRADI UNAOTAKA KUWAPIGANISHA NA EGYPT KWA MAJI YA MTO NILE UMESIKIA WANATUMIA ZOTE? DRC NA ZAMBIA UMESIKIA WANATUMIA MW ZAO ZOTE? HIVI HAMJUI UMEME NI BIDHAA TENA ADIMU KAMA URANIUM? YANI ALIYETULOGA NAONA AISHAKUFA MUDA MREFU SANA, OTHERWISE HATA RUSHWA TUNGEMPA ATUPE KIKOMBE CHA BABU. MITAZAMO HASI YOTE HAPO JUU UKUTE YA MAOFISA, WAKUU WA VITENGO NA WATU NA DEGREE ZAO, SASA KULE KIJIJINI SIJUI NDO ITAKUWAJE?
ReplyDeleteMie nakubaliana na nyie wote watoa maoni na mna point nzuri, kasolo napishana na mwanzilishi wa hii topic kwani yeye anatoa maswali tu halafu hatoi jibu la tatizo au kutoa ideas fulani.
ReplyDeleteJadilini maada na kuelekezana vizuri tafadhali, hii inakatisha tmaa hata kusaidiana kimawazo....
ReplyDeleteTANZANIA TUNAONGOZA DUNIANI (KWA DIRA YANGU MIMI) KWA KUWA NA WATU KAMA SISI (MIMI NA WADAU HAPO JUU) TUNA PIGA DOMOOOO TU LAKINI MATOKEO ZERO.
ReplyDeleteTatizo la hata hao wasomi wetu nao wanatoa majibu ya hovyo hovyo na mepesi mepesi tu, kwa hiyo kama mradi wa umeme hauwezi kulinganishwa na vitumbua, then tunahitaji miaka mia ngapi (manake mpaka sasa tuko 50) ili tuweze kuupata huo wa kukidhi mahitaji yetu? Deep down is a matter of priority na kuacha ufisadi uliopitiliza. Kwa hesabu ya haraka haraka pesa yote iliyopotea kwenye EPA, rada, to mention a few, zingewekezwa huko tusingekuwa na umeme wa uhakika?
ReplyDeleteChoka mie......
Dah, we anonymous wa 5 uwe unasoma unaelewa. Jamaa katoa mfano wa vitumbua akiwa na maana ingine kabisa.Tatizo letu ni kwamba, we never pay attention into details kufikiri tunajua. Haturuhusu vichwa vyetu kusikiliza na kuelewa na kuchukua hatua till its too. Jamaa kaja na hoja ya maana kabisa. Tuijadili kwa maslahi ya hii nchi na sio kutafutiana sababu.
ReplyDeleteWanasema usiemwamshe alielala, akiamka utalala wewe. Ila kwa sasa watanzania hatupati huo usingizi. May be the guy his right aliposema we are idiot by nature. Then tunatumika na wachache kama daraja la kupata mafanikio na familia zao. which can be true.
Tuna wasomi wengi hawapewi nafasi, wazee wameng'ang'ania madaraka. hatuhitaji madaraka twahitaji miundo mbinu thabiti, tujiajiri, tuishi. Kama watu wananunua hisa TBL, CRDB etc, wana uwezo wa kuwekeza kwenye sector ya umeme since sector hiyo ina uhakika wa soko.
viongozi hawaliruhusu hilo mana wanajua ulaji utaondoka. mana kama mimi nina share nyingi nikiboreka namwuuzia yeyote, nasepa. Pili mkiwa na share mnakuwa na say kulingana na kiwango cha share. Serikali inaendelea kuamini kuwa Tanzanians are bogus, idiots, hawajua haki zao, they dont know its too late for that.
Tupe miundo mbinu safi tunyime ajira tutajua tufanyeje. Umetunyima ajira, miundo mbinu mibovu hafu wataka tuwajibike, je ni kwa kupitia njia gani.
GOld ni yetu, gram moja ya currency 24 ni 110,000tshs, na inabadilika kila mwezi. Huo ni utajiri wetu na tumewakabidhi wazungu miaka zaidi ya 7 wachimbe.katika kuchimba kuna wataalamu wamo mule wanaona wanajifunza. Serikali imeshindwa kusema kwenye hayo makampuni kuwa inatosha. Tununue mitambo kama yao kwa mkopo(world bank) tuchimbe wenyewe? Yani mwekezaji akiingia bongo anakaa miaka 40(Mwadui-almas).Anabobea anakuwa mbabe.
Wananchi tujifunze kudai haki zetu za msingi. Serikali iwajibike kwetu kwa kuwekea miundombinu(umeme, maji, barabara za kueleweka) nasi tuilipe kodi ifanye miradi mikubwa.
Hakuna kiongozi aliejitoa kwa ajili ya nchi hii. Kuanzia rais hadi wabunge wa kawaida. Wanawaza matumizi tu hakuna anaekuna kichwa.
Nna hakika kizazi kinachokuja hakitakubali, nimezaliwa simjui nyerere naona mambo mabovu tu niambie nyerere nitaona waniimbia nyimbo tu. Wajukuu zetu watataka maendeleo tuu. U-idiot una mwisho.
Watanzania tunalalamika tu,basi hatuchukui hatua,tutaendeleaje wakati hatuchukui hatuaWatanzania tunalalamika tu,basi hatuchukui hatua,tutaendeleaje wakati hatuchukui hatua
ReplyDeleteKUSEMA KWELI HAPA TUMEBEBA MAWE ILI TUKAMRUSHIE ADUI AMBAYE HATUMJUWI. MAMBO HAYA HAYATAISHA MPAKA WATANZANIA WOTE TUANZE KUFUATA UTARATIBU. MAENDELEO TUNAYOYAONA LEO KWA WENZETU HAYAKUJA TU HIVI HIVI NI MATOKEO YA WATU KUISHI KWA KUFWATA UTARATIBU WALIOJIWEKEA. MPKA HAPO TUTAKAPOWEZA KUFANYA HILI, TUTAENDELEA KUMINYANA TU. KUNA MDAU MMOJA HAPO JUU AMEONGEA JAMBO LA MAANA KUHUSU UWEZO WA WATANZANIA KULIPIA HUDUMA. SWALI NI JE TUPO TAYARI KUTIKISA MIFUKO YETU ILI TUWEZE KULIPIA HUDUMA? TATIZO KUBWA LILILOPO NI KUWA HUKO DUNIANI KWA SASA TECHNOLOJIA ILIYOPO NI YA KISASA ZAIDI AMBAYO UKIHITAJI MITAMBO HUNA NJIA BALI NI KUINUNUA KWA BEI ILIYOPO AMBAYO ILI IWE NA TIJA MLAJI WA MWISHO LAZIMA ABEBE MZIGO NA SISI TUNATAKA BEI CHEE SIJUWI ITAKUWAJE. HATA HIYO MITAMBO WANAYOLETA NA KUIFUNGA ILI IANZE DECEMBER KUZALISHA UMEME HAITAWEZEKANA MAANA WENYE VISIMA VYA GESI SONGO SONGO WASHASEMA KUWA VISIMA VILIVYOPO HAVINA UWEZO WA KULISHA GESI HIYO MITAMBO KWA HIYO YALE YALE YA KUTOKUFANYA TAFITI KAMA ALIVYOSEMA MDAU HAPO JUU. YOTE HAYA NI KUTOKUWA NA UTARATIBU, UKIENDA BENKI WATU HAWAWEZI FWATA UTARATIBU MTU ANAKUJA KACHELEWA ANATAKA AJIPENYEZE KWENYE FOLENI MBELE YA WENZIYE, BARABARANI DEREVA ANATANUA TANUA HOVYO NA KULETA FOLEN, KWENYE TENDA MABAHASHA YANAFUNGULIWA NYUMBANI KWA WATU KABLA YA TAREHE RASMI NA KUPEANA MICHONGO, MAOFISIN AJIRA WATU WANAPEANA BILA KUFWATA UTARATIBU, MATAFITI AKIPEWA KAZI YA KUTAFITI ANAJIFUNGIA JIKONI ANAPIKA TAKWIMU, YAANI TUMEVURUGIKIWA TUU. LABDA ITAFIKA MAHALI TUTAKAA CHINI NA KUANZA KUJIREKEBISHA INGAWA HAIJULIKANI NI LINI. ULIANZA MGAO WA MAJI KWA MIAKA MINGI MPAKA TUKAZOEA,UKAJA MGAO WA UMEME AMBAO NAO SASA UNAZOELEKA SASA KUBWA LAO MGAO WA MAFUTA SSIJUWI UNAFWATA UPI?
ReplyDeleteMdau #2, Mwenye kufuturu ni mfungaji. Mfungaji hutoa hoja yake kwa heshima na sio kwa dharau. Ona sasa unavyoaibika, hata hoja yenyewe ya mtoa mada umeshindwa kuielewa!
ReplyDeleteNI MIPANGO MADHUBUTI INAYOHITAJIKA TENA IENDANE NA UTEKELEZAJI WA 100% SIO KIBRI WALA MANENO YASIOKUWA NA MSINGI, KILA MTU ANA HAKI YA MSINGI YA KUTOA MAONI LAKINI SIO KILA MAONI NI YA MSINGI WENGINE WAPO WAONEKANE TU KWAMBA NA WAO WANATUMIA INTERNET, LAKINI WAJUE HATA HAO WALIOKUJA NA IDEA YA KUANZISHA NET WALISHUGHULISHA AKILI. NAWASILISHA!
ReplyDeleteJAMANI WADAU NA WATANZANIA WENZANGU,NIMEIELEWA HOJA YA MDAU,NA WACHANGIA MADA NAO WA POINTS NZURI KASORO HUYO BWANA ALIE ENDA KUFUTURU NA WANZIE WACHACHE.KWA KWELI NIKIWA KAMA MTANZANIA NAUMIA ROHO SANA KUONA JINSI NCHI YANGU NIIPENDAYO INAVYO MALIZWA,SASA ISSUE NI KWAMBA TUFANYEJE WADAU??HIVI VILIO HIVI VYA UMEME,RICHMOND,EPA etc,TUMFISHIKISHIE NANI ILI ATUSAIDIE??NA KAMA HAKUNA WA KUMFIKISHIA,WATANZANIA TUFANYEJE JAMANI KUONDOKANA NA HAYA?????
ReplyDeleteNAKUBALIANA NA MDAU ALIYESEMA TUNAONGOZA DUNIANI KWA KUPIGA DOMO, LONGOLONGO NYINGI MPAKA KWENYE TAASISI NYETI - TUNA MPANGO WA... TUMEDHAMIRIA KUWA NA MPANGO WA... - NDIO UTAMBULISHO WA UTENDAJI WETU, TOFAUTI NA WATU KAMA WATANI WA JADI KWA MFANO. NA HII NDIO MAANA, KUNA NUNDA MOJA HUMU (NO OFFENSE ILA HII INAKERA TU BANA) LIMEPAYUKA ETI MDAU UMETOA HOJA AFU HUJATOA SULUHISHO, KWANI HII IMEKUA DEBATE SHULENI? SASA KAMA KILA MTU AKITOA HOJA/SWALI NA AKAWA NA JIBU WHY THE HELL ARE WE ALL HERE SEBULENI KWA ANKAL TUKIJADILI NA KUHOJI? WHY THE HELL DO WE HAVE WATAALAM NA SERIKALI NA TAASISI ZAKE? HII NI MENTALITY YA SIMBA NA YANGA (NO OFFENSE), SAA ZOTE WATU WAKO TAYARI KUBISHANA TU HATA KAMA SUALA NI RAHISI NA LA KITAIFA KAMA LA UMEME AU MAFUTA(REGARDLESS YA KWAMBA LINAHITAJI MAAMUZI MAZITO, MTAJI MKUBWA, ETC). HOJA YA MDAU NI RAHISI SANA, NA NDIYO AMBACHO WENGI WANASHANGAA NA KUJADILI MIAKA NENDA RUDI HATA BUNGENI SASA HIVI, GESI TUNAYO, TATIZO LA UMEME TUNALO, WATAALAM WAPO KIBAO, WAKUBWA WANAOHUSIKA WANASHINDWA NINI KUTOA MAAMUZI KAMA ALIVYOULIZA MDAU, MFANO WA KUZALISHA MW 2000 KWA GESI TU, KWA SERIKALI KUANZISHA MRADI THEN KUTOA 'IPO' WATU WAISAIDIE MZIGO? TUACHENI USHAMBA WA HAKUNA HELA AU WATAALAM COZ WOTE TUNAJUA VYOTE VIPO, HAINGII AKILINI KUWA HIZI SSFs ZETU (social security funds - NSSF, LAPF, GEPF, PSPF n.k) ZOTE WAKAKOSA MTAJI WA MRADI MMOJA TU WA UMEME WA MW 2000 WA GESI TULIYONAYO. KAMA MTAJI HAKUNA AU HII HAIWEZEKANI THEN WHAT THE HELL HAVE WE BEEN DOING FOR THE PAST HALF CENTURY? HAPA KILA MTU, ESPECIALLY WATAALAM NA WASOMI (SIJUI HUWA HAWANA KAZI HAWA WADUDU?) ATAKUJA NI VISINGIZIO KIBAO - OOH SIJUI HII SIO KUUZA VITUMBUA, HII INAHITAJI BLAHBLAHBLHA....LENGO TU NI MTU AONEKANE ANAJUA MICHAKATO NA MISELEBUKO! SIO ISHU, HAPA ISHU NI RAHISI SANA. LASTLY, HAKUNA WA KUMPELEKEA HAYA, HUKO DUNIANI HUWA YANAFIKA TU KWA WAHUSIKA KWA WAO KUJIFANYA VICHWAMAJI NA KUTOKUSIKILIZA WANANCHI NA KUDHANI WANAWEZA KUJI-COCOON NA YOTE YANAYOWACHOSHA WANANCHI. FOR OUR COUNTRY'S SAKE, SOMEBODY SOMEWHERE SHOULD DO SOMETHING, HUU (AGAIN, NO OFFENSE WADAU) UFALAFALA WA KUCHEZEA SHILINGI CHOONI UTAJA TUTOKEA PUANI... WE ACHA TUJIFANYE VIPOFU NA VIZIWI TU!
ReplyDelete