Mama Salma Kikwete akitoa zawadi kwa wageni waliofika kufuturu Ikulu ndogo la Lindi leo

JK akitoa neno la shukrani kwa wageni wake baada ya futari
 JK akiongea na wakwe zake baada ya kufuturu na wananchi wa Lindi 
Mwakilishi wa Globu ya Jamii Mtwara na Lindi, Mdau Abdulaziz Video baada ya kusalimiana na JK
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwasili uwanja wa ndege wa Lindi. 
Nyuma yake ni Mkuu wa Mkoa huo Mh. Meck Sadiki.

Kufuatia tatizo sugu la maji lilodumu kwa muda mrefu katika halmashauri ya manispaa ya Lindi,Rais Kikwete amewaagiza madiwani wa halmashuri hiyo kukaa kwa pamoja na mamlaka ya maji safi na maji taka Lindi(LUWASA)  ili kuzungumza na kufikia muafaka wa kumaliza tatizo hilo la maji.

Rais Kikwete ametoa agizo hilo katika futari ya pamoja na wakazi wa mkoa wa lindi iliyofanyika nyumbani kwake, na kuitaka halmashauri ya Manispaa Lindi kuikopesha fedha LUWASA shilingi milioni 12 kila mwezi hadi Mwezi Disemba mwaka huu kwa ajili ya kusaidia kupunguza tatizo la maji,na baadaye fedha hizo  zitarudishwa na wizara ya Maji. Picha na habari na Abdulaziz Video wa Globu ya Jamii, Lindi


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. That's JK bwana! Very good! Kila m2 anapendeza t-shirt na jeans.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...