Afisi ya Mufti wa Zanzibar na Afisi ya Kadhi Mkuu wa Zanzibar kwa kushirikiana na Jumuiya mbalimbali za Kidini Nchini, inawaalika Waislamu wote katika Kisomo maalum cha Kuwaombea Ndugu zetu wapenzi waliofariki katika Ajali ya kuzama kwa Meli ya "MV SPICE ISLANDERS" tarehe 10/09/2011, kitakachofanyika katika Uwanja wa Maisara siku ya Jumatatu tarehe 12/09/2011, baada ya Sala ya Alasiri.
Kabla ya Sala hiyo ya Alasiri patasaliwa sala Maalum ya "GHAAIBU" kwa kuwaombea ndugu zetu wote waliofariki katika Ajali hiyo.
Shime Waumini wote Wanaume kwa Wanawake tuhudhurie kwa Wingi na Kwa Wakati ili tuweze kuwahi Shughuli zote zilizopangwa kwa Ajili ya Kuwaombea ndugu zetu wapenzi.
Inapendeza kwa wote watakaohudhuria kuja na MISALA na si vibaya pia kuchukua MISAHAFU.
AHSANTENI.
F.S. Soraga
KATIBU WA MUFTI,
ZANZIBAR.
Kabla ya Sala hiyo ya Alasiri patasaliwa sala Maalum ya "GHAAIBU" kwa kuwaombea ndugu zetu wote waliofariki katika Ajali hiyo.
Shime Waumini wote Wanaume kwa Wanawake tuhudhurie kwa Wingi na Kwa Wakati ili tuweze kuwahi Shughuli zote zilizopangwa kwa Ajili ya Kuwaombea ndugu zetu wapenzi.
Inapendeza kwa wote watakaohudhuria kuja na MISALA na si vibaya pia kuchukua MISAHAFU.
AHSANTENI.
F.S. Soraga
KATIBU WA MUFTI,
ZANZIBAR.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...