Habari Ankal,

Napenda kuuliza hili ikiwezekana nisaidiwe kujibiwa maswali yangu. Kuna chuo kimoja kiko mitaa ya upanga karibia na scourt kinatoa Digrii ya pili ama kwa kizungu wanaita Masters. 

Nimekua nikituma maombi kwenye chuo hicho kwa takriban miaka mitatu mfululizo kusoma Masters in Business Administration-Accounting and Finance bila ya mafanikio. 

Mwaka Juzi nilipoenda kufuatilia niliambiwa Form zangu zimepotea. Mwaka jana sikufuatilia, mwaka huu nimeomba tena sijapata, wenzangu nilioombana nao wamekosa lakini walipoenda pale chuoni kuuliza wakaambiwa majina yao yalisahaulika na wakapewa Admission. 

Sasa nataka kujua kama ndo utaratibu wa chuo hicho kuwa ili upate lazima uende pale chuo baada ya majibu kutoka??
Au utaratibu wa utendaji kazi wetu wa kitanzania lazima unyenyekee???

Kindly hide my name.

Omar Chuma

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Ndugu yangu kwanza pole sana, pili nataka kujua hicho chuo kinatoa masters chini ya chuo gani cha taifa au kimataifa, kwasababu hatuna chuo kikuu Upanga Dar-es salaam na masters inatolewa na chuo kikuu au chuo kilicho chini ya chuo kikuu fulani tu, ndo maana tumerekebisha pale Mzumbe na sasa tunawaita kwanza chuo kikuu ndo sasa watoe hiyo masters, upo hapo.
    Ushauri wa bure, sio vizuri kwenda kupoteza muda kwenye vyuo visivyotambulika kitaifa au kimataifa "accademic excellence" yako itakuwa doubtiful or dubiuos kwa maneno mengine, nenda UDSM,SUA,UDOM, MZUMBE na kwenye vyuo vingine vinavyo fanana na hivyo, Hutakuwa na haja ya kujieleza zaidi ukiulizwa ulisomea wapi. Achana na usumbufu huo.

    ReplyDelete
  2. wewe mpuuzi mbona ujataja ni chuo gani? pili kwa miaka mitatu unatuma maombi na unasubiri wewe kweli kichwa maji! LOL
    mdau china

    ReplyDelete
  3. Kweli wa hide your name mdau, lakini jamaa wamekutosa mara tatu hushtuki tu kuwa wewe umeover qualify.
    Hivi hakuna chuo kingine kinachotoa Masters sawa na hicho.
    Plz hide mai name michuzi

    ReplyDelete
  4. Kwa location uliyotaja, utakua unazungumzia Mzumbe University Dsm Business School, hata hivyo hawatoi hiyo course, wanatoa Msc. Accounting and Finanace, hawana MBA Accounting & Finance.....

    ReplyDelete
  5. sasa mbona jina limewekwa au hilo la bandia

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...