Katika salamu zake,Katibu Mkuu amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kuzama kwa kivuko hicho katika pwani ya Zanzibar na kwamba Umoja wa Mataifa uko pamoja wananchi wa Tanzania katika kipindi hiki kigumu
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa Katibu Mkuu na nakala yake kupatika Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa. Salamu za pole za Katibu Mkuu, pia anazituma kwa Serikali na wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar na familia za waathirika wa ajali hiyo.
Katibu Mkuu Ban Ki Moon, pia amewatakia kila la kheri na nafuu ya haraka majeruhi na wote walionusurika wa ajali hiyo.
IMETOLEWA NA UBALOZI WA TANZANIA NEW YORK



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...