WANACHAMA WA TAWI LA CCM UK WAMEPOKEA KWA HUZUNI KUBWA TAARIFA YA AJALI YA MELI YA MV SPICE ISLANDER 1 ILOYOTEKEA   USIKU WA MANANE (SAA 7:00 USIKU) WA TAREHE 10 SEPTEMBA, 2011, IKISAFIRI TOKA UNGUJA KWENDA PEMBA.

WANACCM UK WANAUNGANA NA WATANZANIA WOTE KUOMBOLEZA KWA MAJONZI MAKUBWA AJALI HII ILIYOPOTEZA MAISHA YA WATU TAKRIBAN 200, KUSABABISHA MAJERUHI WASIOJIWEZA NA MSIBA KWA FAMILIA,  NDUGU NA TAIFA ZIMA.

AIDHA CCM UK INAWAPONGEZA WATU NA TAASISI MBALI MBALI ZILIZOJITOKEZA KUSAIDIA KUWAOKOA WATU NA KUWAHUDUMIA MAJERUHI NA PIA KUTAFUTA MIILI YA WENZETU WALIOTANGULIA MBELE ZA HAKI.

CCM UK INA IMANI NA SUBIRA KWAMBA SERIKALI ZITAZIAGIZA MAMLAKA  MAALUM KUFANYA UCHUNGUZI WA KINA NA KULETA MAJIBU YA WAZI NA KWELI JUU YA SABABU ZA AJALI HII MBAYA NA KISHA KUCHUKUA HATUA ZA MAKUSUDI ZA UWAJIBIKAJI ILI KUZUIA AJALI ZISIZO ZA LAZIMA ZISITOKEE TENA.

MWENYEZI MUNGU (ALLAH! (S.A.W)…
                        AWAPOKEE KWA HAKI WALIOTANGULIA KWAKE…
                        AWAPONYE NA KUWATIA NGUVU MAJERUHI WA AJALI HII…
                        AWAFARIJI NA KUWAPA AMANI WAFIWA WOTE…

 Imetolewa na CHAMA CHA MAPINDUZI
                   UNITED KINGDOM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. ccm ungeleza. angalau pole yenu ina maakili kidogo kutaka kuwajibisha serikali yenu ifanyike uchunguzi bila mambo kuenda bwelele kama kawaida yao.

    kitonga mrefu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...