SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUTOKA KWA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA UPPSALA, SWEDEN, KWA NDUGU ZETU HAPO TANZANIA WALIOPOTEZA FAMILIA ZAO KWA AJALI YA MELI ZANZIBAR.
Pole kwa wale wote walio poteza ndugu zao kwenye ajali iliotokea tarehe 10 sept 2011. Tumepokea taarifa izi za msiba mkubwa kwa masikitiko na majonzi
Tanzania tumepata janga kubwa sana. Inasikitisha sana. Poleni ndugu zetu, tukaze mioyo, Mungu atatuona watu wake. Pumzikeni kwa amani mliotangulia.Tunawaombea na Mungu awape nguvu nyotee mlio okolewa, na mnao endelea na zoezi zima la uokoaji. Na Roho za marehemu zipumzike mahala pema peponi.
Janbert Kiwia,
Kwa niaba ya wanafunzi wa Kitanzania,
Uppsala University Sweden


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...