Ndugu zetu Watanzania,

Kwa niaba ya Watanzania na wananchi wote wa Afrika Mashariki waishio hapa Montreal- Canada, tumezipokea kwa majonzi na mshtuko mkubwa taarifa za ajali ya kuzama kwa meli ya MV Spicer jana usiku, tarehe 10/9/2011 iliyosabababisha vifo vingi vya Watanzania wenzetu kutoka Zanzibar.

Kwa niaba ya Uongozi wa Montreal Tanzanians Association (http://www.montrealtanzanians.com/), tunapenda kutoa salamu zetu za rambirambi kwa wananchi wote wa Zanzibar na Pemba na Tanzania kwa ujumla waliopoteza ndugu, jamaa na marafiki zao wapendwa katika kindi hiki kigumu cha maombolezo.

Na pia tungependa kuwapa pole wote waliokoka kwenye ajali hiyo ya kusikitisha na tunawaombea kwa M/Mungu awapuguzie maumivu na awape nguvu na faraja.

Mwisho kabisa, Montreal Tanzania Association (MTA) ingependa kutoa shukrani na pongezi za dhati kwa wote walioshiriki katika harakati za kuokoa maisha ya wahanga wa ajali hii na pia katika shughuli za kuopoa maiti.

Tunamuomba Mwenyezimungu aziweke mahali pema peponi nafsi za wote waliopoteza maisha yao kwenye ajali hii. 

Ameen.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.

Uongozi,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...