Jumuiya ya wanafunzi wanaosoma na kuishi Bangalore, India ( TASABA ) inasikitika kutangaza kifo cha mwanafunzi mwenzetu dada MaryLauren Ndahani Lista (Pichani), aliyekua mwaka wa pili , chuo cha St. George, Banaswadi Bangalore, India

Marehemu alitwaliwa na Mungu akiwa nyumbani kwao Tanzania kwa likizo, na mwili wa marehemu uliagwa jana Dar es salaam kwenda Dodoma kwa maziko.

Jumuiya yetu itafanya ibada maalum ya kumkumbuka na kumuombea mwenzetu siku ya ijumaa (11-11-2011) saa kumi na mbili jioni ( 6pm) nyumbani kwa kiongozi wa jumuiya yetu jimbo ambalo Marehemu alikua akiishi (Banaswadi), Bi. Susan Kavishe, House # 312 3rd OMBR Layout Banaswadi (near St George College ).

Tunawaomba Wanajumuiya tushirikiane vyeka katika kipindi hiki kigumu cha msiba na kuwafariji walioguswa haswa na msiba wakiwemo dada zake walioko Bangalore kwa masomo pia.

Mungu ailaze Roho ya marehemu dada yetu Mary pema peponi

Bwana alitoa, na Bwana ametwaa...Jina lake lihimidiwe

Kwa taarifa zaidi za msiba na misa, tafadhali wasiliana na viongozi wa TASABA

Vice President ... Mr. Anase Stephen ( +919731339875 )
Katibu....... Ms. Edna Stephen ( +919611145774 )
Mweka Hadhina... Mr. Vincent Nkini ( +919731955664 )
Kiongozi wa TASABA - Banaswadi... Ms. Susan O. Kavishe ( +919916683008 )

Imetolewa na:

UONGOZI wa TASABA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. poleni sana - such a beautiful young girl.
    OM SHANTI, OM SHANTI, OM SHANTI.

    ReplyDelete
  2. Mimi simfahamu ila poleni sana wanajumuia,familia..still young jamani.Dumisheni mshikamano huo huko vyuoni hasa hivyo vyuo vya ughaibuni.

    R.I.P Mary


    David V

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...