Makumbusho Economic and Social Iniatives Association ni NGO inayojishughulisha uhendelezaji wa utamaduni wa Watanzania usipotee.Tumeona kwa heshima na taadhima kuleta kipeperushi chetu ukiweke kwenye blogspot yako kama press release information.
Maonyesho yatafanyika Tarehe 16-17 Novemba, 2011 kuanzia saa 4.30 asubuhi mpaka saa 11 jioni katika Kijiji cha Makumbusho - Kijitonyama, kiingilio ni bure.
Tarehe 18 Novemba 2011kuanzia saa
1 jioni mpaka saa 6 usiku kiingilio viti maalum ni
- Tshs 100,000/=
- Tshs 50,000/=
- Tshs 20,000/= - Viti vya kawaida
Maelezo ya tarehe 18 Novemba mbona hayajakamilika- Ni kwa ajili ya kitu gani hivyo viingilio?
ReplyDeleteKesho wanyamwezi, harafu waha, wazanaki, wahehe, wazigua, nk tutameguka kidogo kidogo. huu ni mwanzo tu. Viongozi hamuoni?
ReplyDeletesijapenda wazo la kufanya tamasha hili siku ambayo ni ya kazi. Itatuengua wengi. Ningekuwa na mamlaka ya kubadilisha ningeipanga Jumamosi ili watu wengi zaidi wapate kushiriki. kila la kheri japo nimeenguliwa
ReplyDeletewtakaokwenda huko ni mafisadi tu ndio wana hela hizo
ReplyDeletekwanza nyie wahaya hapa tayari mmeshajitengenezea matabaka watu wa juu na chini kiuchumi je mnaona hiyo ni sawa, kwa kweli sijawapenda kabisa mlipaswa kiingilio kiwe reasonable rate ambayo wa chini na wa juu hata wakati waweze kivimudu. hamjapendeza kabisa kabisa
ReplyDeleteKwa mawazo yangu, kuzingatia mila na tamaduni za makabila yetu mbalimbali hapa TANZANIA mfano Wahaya, Wazanaki, Wahehe, Wazigua, N.K. sio mwanzo wa mgawanyiko, bali ndio njia sahihi ya kuikomboa jamii yetu kutoka katika makucha ya tamaduni za kigeni ambazo tayari tumeshayaona madhara yake ambayo ni KUANGUKA KWA MAADILI NA HASA VIJANA KUEGEMEA KTK MILA NA DESTURI ZA KIMAGHARIBI...MPO HAPO?
ReplyDeletewahaya wote kina nshomile watataka wakakae kwenye viti maalum hahahhah!
ReplyDeleteAngalieni hawa jamaa shemeji zetu isije ikawa ni bijampola kiingilio laki au na ile shughuli itakuwepo?
ReplyDeleteHahahahah mdau wa Sat Nov 12, 03:08:00 AM 2011 umenifurahisha sana kunikumbusha wa SHEMEJI zetu BIJAMPORA!!!! watu walikata tiketi za mabasi za usafiri wa Bukoba na safari haikuwa!.
ReplyDeleteIla kwa vile Wahaya wana kawaida ya kujitambua kuwa ni jamii iliyosoma kuingizana mjini ni kama kuchangamshana AKILI, na kuwa NSHOMIRE!...
hapo hakuna kubaguana kama anavyosema mdau ndio fursa ya kujitambua maana kuna sikumoja mtoto aliyekulia mjini aliona ugali wa ulezi akawa ana shangaa
ReplyDelete