katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira,Bw.Eric Shitindi alipokuwa akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Kazi na Ajira.Katibu Mkuu aliwajuza wanahabari kuwa Wizara hiyo itakuwa na maonyesho ya utendaji wake mbalimbali katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru.Maonyesho hayo yataambana na Wiki ya Hifadhi ya Jamii ambayo itahusisha Mamlaka ya Usimamizi na udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya jamii na Mifuko yote ya Hifadhi na jamii Tanzania Bara (GEPF, LAPF,NSSF,PPF,NHIF,PSPF).
Wiki ya Hifadhi ya Jamii ambayo ni mara ya kwanza nchini Tanzania, itazinduliwa rasmi na Waziri wa kazi na ajira Mh.Gaudentia Kabaka siku ya tarehe 08/11/2011 katika viwanja vya maonyesho vya Mnazi Mmoja. Kusudi kubwa la wiki hii ijayo kuanzia tarehe 08/11 mpaka 13/11/2011 katika viwanja vya Mnazi mmoja.Kusudi kubwa la wiki ya Hifadhi ya Jamii ni kuulelimisha Umma juu ya Sekta ya Hifadhi ya Jamii na umuhimu wa kila mwananchi kuwa mwanachama na kuendeleza uanachama katika sekta hiyo.
Wakuu Wa Mifuko ya PPF,PSPF,GEPF wakifuatilia kwa makini maelezo ya katibu mkuu
Mkurugenzi wa mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya HIfadhi ya jamii (SSRA) Bi. Irene Isaka- katikati, na Mkurugenzi mkuu wa LAPF,Bw. Eliudi Sanga wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu
Katibu Mkuu,Naibu katibu Mkuu,Kamishna Wa kazi na ajira,Mkurugenzi mkuu wa SSRA katika picha ya pamopja na wakuu wa mifuko ya Hifadhi ya Jamii Tanzania Bara.
Kijana wa mzee poti umependeza. Irene hujambo!!
ReplyDeleteMdau N.America
Eric is the best. Listen to this interview while he was a Deputy PS at president's office.
ReplyDeletehttp://www.princeton.edu/successfulsocieties/content/focusareas/CS/oralhistories/view.xml?id=264
Mdau, Canada
TUKIJIPANGA, SUALA LA KUJITEGEMEA INAWEZEKANA!...mifuko kama hii inaweza kutukomboa kutoka ktk makucha na masharti magumu ya MISAADA ya WAINGEREZA na Bwana DONALD CAMERON wao!
ReplyDelete