Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, akimtambulisha mwanae wa kiume kwa Waziri Mkuu, MIzengo Pinda katika sherehe za kumwapisha Rais huyo Mjini Kinshasa leo mchana
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na mke wa Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Olive katika sherehe  za kumwapisha Rais huyo Mjini Kinshasa. Picha na mdau Hilary Bujiku wa PMO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Huyu kabila nae ataleta vita nyingine DRC..kachakachua matokeo,na kawahi kujiapisha rais..mwanzie nae anataka kujiapisha kuwa rais pia..i hope mh w.mkuu umemwambia ukweli kuwa tz tumechoka na wakimbizi kwani serikali kutoa huduma kwa raia wake imewashinda..

    ReplyDelete
  2. Hii nchi niliko, niko na wacongo yaani kila mara wananieleza kuwa hawamtaki kabila maana si mkongo, ni mtz, na wanaapa akitangazwa kuwa rais tena vita havitaisha kwao. Ooh come one rais wa africa achieni wengine nao waongoze.

    ReplyDelete
  3. Noana JK anaanza ku-revenge kama kawaida yake. Mzee wa visasi. Hawakuja kwenye miaka 50 ya uhuru wetu na yeye anasusa kwenda kwenye matukio yao. Kazi kweli kweli.

    ReplyDelete
  4. Kulikoni bwamkubwa kashindwa kuhudhuria mnuso huu?

    ReplyDelete
  5. mkubwa naye bwana na tie zake !LOL
    mdau paris

    ReplyDelete
  6. Tie zinahusu nini bana. Kwanza hazina asili yetu. Western attire is not always the best. TZ inaweza kumtumia Kabila kukuza biashara na congo guys....

    ReplyDelete
  7. Kwa siasa za afrika kabila atatawala tu wapende wasipende.

    ReplyDelete
  8. Jamani akienda nje JK maneno sasa kampa shavu Mtoto wa mkulima bado hampendi, mtoto wa mkulima mmeona wapi safari za nje mwachieni naye atanuetanue jamani

    ReplyDelete
  9. Kabila anakubalika na jeshi, Upinzani unakuablika na umma. Jamani patakalika huko? Ee MUNGU uwarehemu na balaa la machafuko

    ReplyDelete
  10. Pm anavyovaaa sijui nani anasimamia wardrobe malfaksheni hii tai duu... Na pia sijui nani amshauri kuhusu kufunga vifungo vya koti anaposimama maana huwa hafungi hii ina sababu zake.. moja ni presentation na heshima, mbili ni tahadhari kwa zipu, na pia koti laweza kunasa kwenye mlango au chupa mezani ukajitia aibu. Hivyo unaona unapokaa unafungua vifungo uwe comfortable na ukisimama unafunga usije ukawa ka gangwe.....
    Tafadhali ashauriwe...Mama Pinda huoni hii urekebishe au nawe huelewi??!!

    ReplyDelete
  11. Picha ya juu kila mtu amenuna isipokuwa Mkuu na Rais Kabila... Jamani kama unakutana na Rais wa nchi si lazima ku-smile ili akuone kidogo.... Picha ya chini kuna njemba nyuma ya Mkuu anachekelea... mhh mi nna wasiwasi, mbona amacheklelea my wife wa Rais, hajipendi au...?

    ReplyDelete
  12. Mi sielewi kitu kimoja,kiongozi mkubwa kama Pinda kuvishwa identification badge.
    Sababu ya mtu kuvaa identification badge ni kutambiliwa na security au kupata access ya restricted area.Sasa kama kiongozi kama yule Waziri mkuu wa nchi kweli anahitaji introduction au badge ya kumtambulisha? They should know who are the prime guests or the VIP's are and not by the badges.
    Heshima.

    ReplyDelete
  13. Yes, beji kwa w. mkuu sio sawa.

    ReplyDelete
  14. Wajameni Bwamkubwa hakuhudhuria mnuso huu kwa dalili zilizopatikana awali ktk vyanzo mbalimbali vya uangalizi mwenendo wa uchaguzi na kutoa maoni kuwa UCHAGUZI WA DRC HAUKUWA HURU NA WA HAKI!

    HIVYO INASEMEKAMA KUWA NDUGU YETU JOSEPH ZAIDI YA ANAVYOTUHUMIWA KUWA NI MWENZETU M-TZ KTK MCHAKATO WA UCHAGUZI DRC AMEFOSI KING!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...