Meneja wa Huduma kwa Wateja na Uhusiano wa Bohari ya Madawa (MSD), Salome Mallamia (kushoto) akimkabidhi Ofisa Muuguzi wa Zamu wa Hospitali ya Temeke, msaada wa aina 107 za dawa zilizotolewa na bohari hiyo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajli ya wagonjwa mbalimbali wanaohudumiwa na hospitali hiyo. Dawa hizo zilizotolewa hospitalini hapo , ni zile zilizobaki baada ya kuwahudumia wagonjwa kwenye Kijiji cha Wizara hiyo wakati wa Maonesho ya miaka 50 ya Uhuru, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam. Katikati ni Ofisa Huduma kwa Wateja wa MSD Dodoma, Lucas Chagula.
Mwandishi wa Habari, Mwandamizi wa gazeti la Jambo Leo, Grace Michael, akisalimiana na Ofisa Muuguzi wa Zamu wa Hospitali ya Temeke, Rolester Kinunda.
Moja ya makasha ya dawa hizo.
Salome wa MSD, akisoma risala kuhusu msaada huo.
Makasha ya dawa hizo yakishushwa kwenye gari yakipelekwa Store ya hospitali hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. mzee wa majunguDecember 19, 2011

    famasi za mitaani zitajaa dawa sasa!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...