Wafanyakazi wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) wakishindana kukimbiza kuku wakati wa kusherehekea siku yao waliyoiita TPB DAY OUT. Nia ya kuadhimisha siku hiyo ni kuwapa fursa wafanyakazi kukutana na kucheza pamoja nje ya sehemu zao za kazi ili kupumzisha akili na kujenga umoja na upendo kati yao. Wafanyakazi wote walishiriki kucheza michezo mbalimbali kwenye ufukwe wa Kunduchi Beach Resort. Pia walishiriki kwenye mashindano mbalimbali kama vile mpira wa miguu, mpira wa wavu (Volley ball), kukimbiza kuku. Kuogelea pamoja na kucheza muziki.
Home
Unlabelled
WAFANYAKAZI WA BENKI YA POSTA WASHEREHEKEA TPB DAY OUT
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...