Mwanamama ambaye hakufahamika jina lake kwa haraka,akiwa na sinia lililosheheni Samaki wa Kukaanga aina ya Perege na Kambale aliokuwa akiwauza kwenye stendi ya mabasi ya Mikoani,Ipogolo Mkoani Iringa mchana wa leo.swala la usalama wa afya ya mtumiaji halijazingatiwa kabisa kwa mama huyu kwani samaki hao hawajahifadhiwa katika hali ya usafi.
Mama huyo akikimbilia kwenye Basi ili aweze kuuza samaki hao kwa abiria waliopo ndani ya Basi hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2012

    hujalazimishwa kununuwa usituletee zakuleta hapa, hicho chakula hakina tatizo lolote

    wache wenzako wapate riski zao

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2012

    Hao ni samaki au kuku?

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 15, 2012

    Mtumiaji anatakiwa akawapashe moto mwenyewe nyumbani kwake,huyo mama hapo labda anahangaikia watoto wake,bwana mkubwa hatoi hela ya matumizi,n.k....watoto wanafika hadi chuo kikukuu(nina mfano halisi).Sikubaliani na kutozingatia masharti ya Afya lakini Ukweli ndiyo huo.Tuliokulia huko vijijini ndiyo 'usipime'.

    David V.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 15, 2012

    Nani amekwambia haijali afya?? ....nyie wabeba box mmekimbia nchi mkirudi mnajifanya mnajua ''usafi''....kwa taarifa yako Samaki wanapokaangwa wanawekwa CHUMVI ambayo inazuia microbial spoilage by inhibiting growth of food-borne pathogens such as Salmonella or Clostridium botulinum,so hao samaki ni safe na ni watamu ile mbaya,mbona sisi tunakula na hatuumwi???

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 16, 2012

    Haaa tena miye huku Toronto natokwa na mateeee, I grew up eating that, mama (RIP) ananunua vipande kadhaa, anatengeneza mchuzi wa nazi anavidumbukiza haaa na ugali na mchicha pembeni, I am where I am today, sijapata minyoo wala kipindupindu....

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 16, 2012

    KUNA STUDY ILIFANYIKA UNIVERSITY OF NAIROBI KUHUSU VYAKULA VYA BARABARI, HAVIKUWA NA SERIOUS EFFECT KWA WALAJI. TUACHE TABIA YA KUJIFANYA WAJUAJI. HAIWEZEKANI WATU WOTE TUKAFANYA KAZI ZA AINA MOJA. TUJIFUNZE TUHESHIMU AJIRA ZA WENGINE. NA WEWE UNAEPONGA TULIOKO NJE, HII HABARI INA UHUSIANO GANI NASI. KAMA ULIPIGWA BOMBA KIMPANGO WAKO ACHA HU HATE

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 16, 2012

    Usinunue basi, kwani umelazimishwa??

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 16, 2012

    kuna watu humu fikra hawana.

    Yaani kanuni za afya hazifuatwi halafi wewe unasema "usinunue" au "umelazimishwa?"

    Kumbuka kanuni za afya zinamlinda mtu asiyezifahamu wala kuzijali ikiwemo wewe.

    muige mwehu kula jalalani basi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 16, 2012

    Huyu jamaa ameniharibia siku yangu kabisa. Hao samaki angeweza kuja nao Dar tungegombania. Wakiwekwa nazi, na punga pembeni. Nomaaaaaa!

    Sio kila unachokiona huko ulaya ni kweli. Hakuna tatizo hata kidogoooo la afya. Pumbafu!

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 16, 2012

    KAZI NI KAZI BORA MKONO UENDE KINYWANI!!

    Huyu mama nimempenda, ajira hakuna, bora alivyoamua kufanya hivyo kuliko kuwa ombaomba au changuduo. Bravo mama, hali ya maisha imekuwa ngumu sana hata sasa naona hapa Dar biashara ya kuuza matunda (ndizi, karoti, mapapai, parachichi) ni akina mama walio na mabeseni vichwani wanazunguka kila kona na wengine wakiwa na watoto migongoni.

    Mama ni nguzo ya familia, usafi umezingatiwa hapo. Mbona twala ndizi mbivu barabarani bila kuosha?

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 16, 2012

    Samaki watamu sana hawa, na ukiwapasha moto basi umeharibu utamu . . . "Mama chachandu ipo hapo?".

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 16, 2012

    Hujalazimishwa kununua nenda kale vya nyumbani kwako unavyopikiwa na house girl/boy asiyezingatia usafi

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 16, 2012

    Aliyepost hii habari inabidi ajifunze zaidi, kama ana elimu haimsaidii kabisa. Hii sio njia ya kueleza mazingira ya usafi kwa kumpiga picha mtu hadharani. Alafu hao samaki wamekaushwa ili wawepo muda mrefu, ukinunua unapika au wewe ukinunua unakula bila kuwatayarisha kwanza?. ULIZA KWANZA SIO KUKURUPUKA

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 16, 2012

    Tusiige mambo ya mamtoni, extreme sanitation and cleanliness is not good for us, the body needs a bit of them bugs to create active its own immunity, no bugs exposure leads to pure immunity and less resitance to diseases.
    Dr Gangwe Bitozi.

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 16, 2012

    WEWE BADALA YA KUANDIKA MATAMANISHI UNATULETEA UBWANA AFYA WAKO? HAO NDIO SOMBA BWANA EBO!

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 16, 2012

    Chakula cha barabarani hakina madhara makubwa kama vya makopo na hayo ma burger na Sausages tunayokula kwa ushahidi tizama watu wanavyo nenepa umarekani na nchi za ulaya ni ugonjwa mtupu na siyo sababu ya kuiba pesa kama TZ.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 16, 2012

    wakati mwingine muangalie vitu vya kupost humu hao samaki ni poa sana na mama anapata riziki yake unafikiri atasomesha vipi watoto ?

    serikali inatoa elimu bure? achenmi kuwa na ujinga mwacheni mama apate riziki

    nipo ulaya lakini mate yananitoka nawatamani kishenzi ningekuwa hapo mbona ningemuuingisha mama mpaka akifika nyumbani akanisimulie.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...