Na Woinde Shizza,Arusha

MBUNGE wa jimbo la Arumeru mashariki Joshua Nasari (chadema) amewasihi vijana,kujifunza uwajibikaji na kuachana na starehe zisizo za msingi hususani unywaji wa pombe wa kupindukia aina ya viroba,hatua ambayo itawasaidia kuwa na maono yenye tija katika kujiletea maendeleo wenyewe na kuondoa dhana tegemezi.

Nasari ameyasema hayo katika hafla ya uzinduzi wa kituo cha watoto yatima cha African Orphanage kilichopo Sakila,uzinduzi huo ulienda sanjari na sherehe za kumuaga mwinjilishaji na mwasisi wa makanisa ya Pentekoste wilayani Arumeru,Askofu Nickson Issangya anayeenda kuhubili injili nje ya nchi katika nchi za Afrika na balani Ulaya.

Aidha alisisitiza kwa kuwataka wananchi katika jimbo hilo kushikamana kwa pamoja na kusahau itikadi zao za kisiasa kwani muda wa kampeni umeisha na mbunge amepatikana.

Alisema wakazi wa jimbo hilo wengi wao wamekuwa wakijengeana chuki zinazosababishwa na tofauti za kisiasa hadi makanisani bila kutambua kuwa uchaguzi sasa umeisha na kinachotakiwa ni kuwajibika kwa kufanyakazi za kuleta maendeleo katika jimbo hilo na taifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine mbunge huyo alitoa ushuhuda wa maisha yake na kudai kuwa wakati akisoma shule ya msingi alikuwa akiuza kwa kutembeza minadani mifuko aina ya plasitiki maarufu kwa jina la Marliboro, kwani wazazi wake hawakuwa na uwezo wa kumlipia ada.

Alisema kuwa wakati akisoma alipandikizwa maono ya ubunge na mwenyezi mungu ,hivyo katika kipindi chote cha masomo yake kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu,ndoto zilizokuwa zikimjia usingizini ni kuhusiana yeye kuwa mbunge .

Aliwataka wananchi katika jimbo hilo kushikana katika kuliletea maendeleo jimbo la Arumeru mashariki,lenye changamoto nyingi ikiwemo ya uhaba wa Ardhi,na kudai kuwa atafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha analeta mabadiliko na kwamba wakazi wa jimbo hilo hawatajuta kumchagua .

Kwa upande wa Askofu Nickson Issangya aliwaomba wakazi wa jimbo hilo kuacha kubaguana kwa itikadi za kisiasa hadi makanisani na kuwataka kupigania maendeleo yao wenyewe wakimtumaini mwenyezi mungu kwa kuwa kampeni za uchaguzi zimeisha na mbunge amepatikana.

Katika sherehe hiyo mbunge Nasari aliahidi kusaidia vituo vya watoto yatima vilivyomo katika jimbo hilo na kuwataka wananchi kujikita zaidi kutoa msaada kwenye makundi yasiyojiweza hususani watoto yatima wajane na akinamama wazee,kwani kabla ya kuwa mbunge aliwahi kufanyakazi kwenye kituo cha watoto yatima wapatao 86 .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 14, 2012

    Na kweli maana kauli alizozitoa nadhani ye mwenyewe alikuwa amepiga VIROBA vya kutosha

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 14, 2012

    hehehe, kumbe Membe hayuko peke yake!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 14, 2012

    Safi sana!

    Mhe. Joshua Nassari hayo sasa ndio majukumu ya Ubunge na sio uchochezi vurugu na uvunjaji wa sheria.

    Hayo ya 'itikadi hiyo' na 'uenezi huo, utakuwa umeyapata kutoka kwa Wanasiasa waliopevuka na kukomaa kutoka CCM (sio CHADEMA) hapo Arumeru Mashariki!

    KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 14, 2012

    Hi ni kweli vijana achekunywa pombe kabisaa hakuna faiida yeyote.zaiidi ya ku haribu afya yako tuu mimi mwenyewe nimeaacha kabisa!!! sasa ni mazoezi tuu Asnte mheshimiwa kwa kulioona hilo wanafiri ni fashion furani kunywa pombe laa hasha!! mdau
    maziku kutoka Amsterdam

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 14, 2012

    Mie NASHANGAA WATU WANAKATAZA POMBE ZA KIENYEJI POMBE NI POMBE TU ZOTE HAZIFAI WACHENI KUONGELEA KITU NUSU NUSU POMBE ZOTE NI MAGONJWA NA DRUG PIA ZINAUMIZA SANA VIJANA TUENDELEE HIVYOHIVYO KUKEMEA HONGERA NASSARI. PAZI.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 14, 2012

    Kwa yale aliyosema kwenye ule mkutano wa Chadema ingefaa yeye mwenyewe aache pombe kwanza.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 14, 2012

    na yeye aache bangi inayomtuma kutugawa watanzania

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 15, 2012

    watakutimua wachaga sasa hivi , hujui kama ni mila yao kunywa pombe na ukisema hivyo masale yatapandwa na nini
    mh. rais wa kanda ya kaskazini angalia !

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 15, 2012

    Huyu jamaa taahira nini, tuache pombe na viwanda vya pombe ndivyo vinavyoilipa serikali. Baba alikunywa mvinyo sisituache kwa nini

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...