Baadhi ya maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Serikali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili kwenye lango la kuingia hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara ikiwa ni moja ya mkakati wa kuhamasisha utalii wa ndani nchini.
Maafisa habari wakipata kifungua kinywa katika eneo la Lamadi lililopo mkoa mpya wa Simiyu wakiwa njiani kuelekea katika hifadhi ya taifa ya Serengeti.
Mfanyabiashara wa supu katika eneo la Lamadi mkoani Simiyu Bw. Sobia Majuto akiwahudumia baadhi ya wateja wake ambao ni maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali walipokua njiani kuelekea katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Wanyama aina ya Twiga ambao ni moja ya vivutio vikuu katika hifadhi ya taifa ya Serengeti wakitembea kwa mstari ndani ya hifadhi hiyo.
Kundi kubwa la Nyumbu wakiwa katikati ya Barabara ndani ya hifadhi hiyo na kuufanya msafara wa magari yaliyowabeba maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa serikali kwenda kwa mwendo wa polepole. Kwa mujibu wa taratibu za hifadhi ni kosa kwa dereva kupiga honi, kuendesha gari kwa mwendo kasi au kupiga honi ndani ya eneo la hifadhi.
Mnyama aina ya Simba maarufu kwa jina la mfalme wa mwitu akipanda mti ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuwafanya maafisa Habari na Mawasiliano wa serikali kushangaa uwezo wa Simba huyo.Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 14, 2012

    huyoo anaitwa SIMBA MBAWALA NI NMDOGO KIDOGO UKILINGANISHA NA SIMBA TUMJUAE AMBAE HAPANDI MTI.
    SIMBA CHAI ANAUMBILE KUBWA UKILINGANISHA NA SIMBA MBAWALA.
    SIMBA WALE WA SELOUS UKIWANGALINISHA NA SIMBA HUYU WA SERENGETI UTAGUNDUA TOFAUTI.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 15, 2012

    serengeti highway itajengwa vipi kama hata kupiga honi ndani ya hifadhi hairuhusiwi?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 15, 2012

    misupu hiyo mtaharisha wajomba!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...