Na Mohammed Mhina, Zanzibar

Kiongozi wa Jumuiya ya kikundi cha UAMSHO, Sheikh Farid Hadi Ahmed
ZANZIBAR IJUMAA JUNI 1, 2012. SIKU moja tu baada ya Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein, kuzungumza na Waandishi wa Habari Ikulu mjini Zanzibar kuhusiana na Vurugu zilizotokea wiki iliyopita, leo Kiongozi wa kundi la Uamsho Sheikh Farid Hadi Ahmed, amezungumza na Waandishi wa Habari na kusema kuwa wataendelea na harakati zao ya kupinga Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mpaka kieleweke.

Sheikhe Farid ambaye amelaani vikali vitendo vya uharibifu wa mali ukiwemo wa uchomwaji moto magari na baadhi ya makanisa mjini Zanzibar, amesema pamoja na wao kulisaidia Jeshi la Polisi katika kukusanya taarifa za kuwabaini wale wote waliohusika na uharibifu huo, lakini pia wataendeleza harakati za kudai kura ya maoni ya kupinga Muungano wa Jamhuri ya Tanzania.

Ingawa alikataa wafuasi wake kushiriki katika vurugu, lakini amesema leo wanakesha msikitini kuwaombea heri vija wote waliokamatwa kufuatia vurugu hizo ili waachiliwe bila ya masharti.

Sheikhe Farid pia amewalaumu baadhi ya vijana wakiwemo wa chama kimoja cha siasa kuwa wao ni miongoni mwa wanzilishi wa vurugu hizo.

Amesema kwa hatua hiyo anajenga imani kuwa miongoni mwa watu waliochoma makanisa siku ya tukio hilo, walikuwa ni mmoja miongoni mwa vijana hao na wanakamilisha taarifa zao ili kuwapatia Polisi kwa hatua zao.

Amesema mbali ya kuwa Serikali imepiga marufuku mikutano na maandamano, lakini Jumuiya yao ya Uamsho itafanya Mhadhara mkubwa Jumapili Juni 3, mwaka huu kwenye Viwanja vya Lumbumba mjini Zanzibar mhadhara ambao utafuatiwa na  maandamamo yatakayofanyika Juni 26, mwaka huu.

Wakati wa mkutano huo, Sheikhe Farid pia amevilaumu baadhi ya Vyombo vya Habari hapa nchini na kusema wameandika habari zenye chumvi nyingi na kuupotosha umma kwa kuongeza hofu miongoni mwa wananchi wa ndani na nje ya Zanzibar.

Hata hivyo Shehe huyo ameshindwa kufafanua baadhi ya hoja alizoulizwa na waandishi wa habari kwa mfano kuzibwa kwa barabara kwa mawe na magogo ya minazi ama kuchomwa matairi na makanisa kuwa inauhusiano gani na madai ya kuwepo kwa muungano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 30 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 01, 2012

    deal hilo ustaadh endelea kukazana....zanzibar ukiwa mbishi sana unaingizwa kwenye serikali kama CUF hivyo nanyie jitahidini mpate nafasi yenu kwenye serikali ya umoja.hicho ndio mnataka na njaa zenu hakuna lolote.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 01, 2012

    mmeona wapi wachochizi waliopo, mnawasingizia bure waislamu kama yale yale yaliyotokea marekani na duniani kwengineko, wazanzibar bwana waungwana toka mwanzo tulikuwa na wakiristo wetu wa kizanzibar na mbona tulikuwa hatuwachomei nyumba zao za kuabudiwa iweje leo,
    ukweli kukidhihirika uongo hujitenga, mnaona sasa rahman inshalla atatusadia sisi na wenginewe wanaopenda amani katika viziwa hivi viwili pamoja na bara amin

    Los Angeles

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 01, 2012

    safi sana sheikh hapa mpaka kieleweke kimoja tu, hatuna haja ya muungano hii ndio mada kubwa ya mihadhara

    sisi wanzanzibari huu muungano hatuutaki, hayo ya makanisa, magari kuchomwa moto ni hao hao ccm, sio mihadhara kwani sisi lengo letu nikuwa huu muungano hatuweebu

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 01, 2012

    Naona mwarabu anataka kurudi kwa nguvu

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 01, 2012

    Sh Faridi safi sana

    Hawa waserikali wanajaribu kudivert hoja ya msingi "kura ya maoni ya muungano"

    Haya ni primary madai, hii kuchoma makanisa , gari ni janja na mbinu za kizamani ambazo hazina nafasi katika siasa za leo

    Kinachotakiwa ni kura ya maoni, ndugu zangu wa Tanganyika amkeni hali si shwari tena, musilale mukishikilia makanisa, Zanzibar ukristo uliingia mwanzo kuliko Tanganyika na kanisa lililojengwa 18s mpaka leo liko, haya ni kudanganyana tu na kupakaziana chuki. Ukitaka kumuua mbwa unamwita jina baya kwanza.

    Madai ya Mwamsho ni very credible, watanganyiaka waungeni mkono tupate muungano nzuri wenye maslahi kwa pande zote mbili. kinachopiganiwa ni structure ya muungano na si ukiristo,uislam wala ubudha.

    Amkeni na nyinyi mupate serikali yenu ya Tanganyika musionewe na vijisiwa kadogo

    Mdau LA

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 02, 2012

    sasa nyinyi wa zanzibari hivi mnaweza kupigana vita na wabantu? muungano utakua pale pale hizo ni kelele tu lkn wembe ni ule ule hao wakina sultan warudi kwao mbona wanangangania eeeh

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 02, 2012

    tatizo ni kwamba bongo au zenji kawauzia hawa waaarabu wa ki oman uraia wa tanzania ndo wanaleta haa malumbano. piga shaba hao wazamiaji wote wa kiarabu warudi ma kwao oman nk!!! africa kwa waafrica tu. minyaa ni hii piaaa misupu? meseji senti

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 02, 2012

    We want "rule of law" ili tupate amani. Kwani Zanzibar hatuna sheria ya kuwadhibiti wafanya fujo?

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 02, 2012

    Nyerere alipowakataa baadhi ya watu kuwa Marais, watu walimuona hafai. Sasa tumeanza kuyaona!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 02, 2012

    mie nimesoma yote tuu

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 02, 2012

    yaani kama HAMAS kabisa au TARIBAN - chadema wataingiza hii nchi kwenye mashaka makubwa jamani !

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 02, 2012

    Haya matatizo nilazima yapate ufumbuzi.

    Haiwezekani tusumbuliwe na watu wachache huko Visiwani.

    Ni bora tuuvunje Muungano lakini Bara tunaweza kubakia na jina hili hili la TANZANIA badala ya JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

    Hao Wazanzibar pia watake kuuvunja Muungano lakini wasifikiri kuwa na manufaa ya upande mmoja, mfano wavinje Muungano halafu waendelee kukaa bure kwetu na kutumia rasilimali zetu bure na fedha zetu za kodi.

    Kama wanataka Muungano uvunjike na uvunjike lakini wawe tayari kukabiliana na SERA ZETU MPYA DHIDI YAO.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 02, 2012

    Inawezekana pia kama Kila mmoja atajitegemea, Zanzibar na Tanganyika.

    Lakini sio Muungano uvunjike halafu mmoja anufaike na mwingine ilhali hakuna Muungano!

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 02, 2012

    waarabu warudi oman na huyu sheikh akae akijuwa hii ni africa sio oman na wala si alshabb tunasema tukiamuka watarudi oman na boti bantu people hawakutokea oman

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 02, 2012

    Kazi ni rahisi sana!

    IBADA NA KAZI SERIKALINI!

    Sheikh Farid apewe Uimamu wa Msikiti wa Ikulu Zenji atatulia tu, kwani tatizo nini?

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 02, 2012

    tungepata cv ya huyo sheikh ndoyo tungeweza kuchambua vizuri kama anaelewa anachoongea na kukipigania au ni kibaraka tu! Maana wengine wanapambania hoja kwa nguvu na wala si nguvu ya hoja. Mimi bado nina mashaka nae sana huyu!

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 02, 2012

    Huyu kiwango chake cha elimu ni kipi? maana elimu nayo ni muhimu ukiwa unawaongoza watu. Bila elimu ya kutosha huenda ikawa ni tatizo hata unachokiongea kitakuwa na upungufu au mapungufu ya busara.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 02, 2012

    Sheikh Faridi msimo huo huo ni mpaka kieleweke, muungano hatuutaki hizo njama zao ni za kitoto kabisa. na ndugu zetu watanganyika tunawashangaa hamtaki utaifa wenu huo ni utumwa munaogopa vivuli vyenu wenyewe sisi tukitembea dunia nzima tunaona fahari kujinasibu na uzanzibari wenu ila nyie munakataa utaifa wenu hebu sisi tuazcheni tutoke then kama nyie muna njaa na utanzania mutaendelea kujiita watanzania. sisi muungano basi

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 02, 2012

    wewe unaesema piga shaba hao warabu hivi nikikuuliza wewe na huo msaada wa mabasha zako wa kimarekani unaowategemea

    ambao sasahivi wamepitisha sheria ya kuoana wanaume sheria ambayo kwakuwa mnategemea misaada kutoka kwao mtaingizwa kwenye sheria hizo na kesho utakuja kumuoa kaka yako ulale nae kitanda kimoja


    hivi nikikuuliza warabu utawaweza wewe kivita? hivi dunia inatetemeka kila siku kwa vita za warabu

    leo hii wewe mgona nesara au mlala njaa unajisifu eti unaweza vita za warabu?

    hivi kuna nchi hata moja ya africa inaweza kuzichapa na mwarabu?

    mwarabu anawatesa mabasha zako wamarekani na ulaya yote kwa ujumla kila siku wanarudishwa makwao wakiwa maiti

    hivi unajuwa vita ya mwarabu inaweza kudumu miaka mingapi?

    hahaha wacha nicheke mimi wanaume wakiongea nawewe unataka kuongea na kujigamba na hilo panga lako ukapigane vita na mwarabu?

    pigana na njaa zako na magonjwa alafu ndio umtafute mwarabu mwenye kulalia kitanda cha dhahabu


    ANKALI CHONDE CHONDE NIWEKEE HAYA MAJIBU YA HUYO ANAEITA WATU WARABU ALAFU KESHO ANALALAMIKA KUWA DUNIA INA UBAGUZI?
    NANI ANAANZISHA UBAGUZI?

    MTANZANIA MWENYE ASILI YA KIARABU AU KIHINDI UNAMUONA KUWA SIO MTANZANIA?

    JE MZUNGU AKIWA NA URAIA WA KITANZANIA UTAJISIFU KILA SIKU NCHI YENU INA WAZUNGU?

    ACHANA NA MAMBO YALIYOPITA NA WAKATI NDIO MAANA HUTOONA MWARABU ANASHIRIKI KWENYE MICHEZO AU UMISS SABABU MNAJULIKANA WALALA NJAA KWA UBAGUZI MNAONGOZA.

    ASANTE ANKALI KWA KUZALIWA MUUNGWANA.

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 02, 2012

    chonde chonde watanzania wenzangu tusijiingize kwenye vita ya kidini

    hivi hao warabu au waislamu wakiamua kweli watuletee alshababu tu patatoka mtu hapo?

    wale watu wana uzoefu wa kupiga vita na kulenga watu usiombe
    tusikae tunategemea jeshi letu ambalo kula kulala

    hao warabu wapo fiti sana kivita mtake msitake tunaweza kufutiwa nchi yetu kwa wiki moja tu.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 02, 2012

    kumbukeni libya ya miaka ile ya idi amini ilikuwa libya changa

    libya ya leo hii ina vifaa na uzoefu wa kupigana vita chama cha muslim brothers kinasonga mbele kutetea maslahi ya waislam

    leo hii mnataka vita na waislamu hivi wakisema waombe msaada nchi jirani somalia libya egypt nigeria patatoka mtu hapo bongo?


    mungu tujaalie amani nchi yetu na tuzidi kuwa wamoja ameen.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 02, 2012

    Watanzania tuwe makini sana Na Daima tuogope ushabiki holela!
    Utengamano huu wanaoutaka hao Uamsho ni Kuelekea UANGUKO Mbaya na wa AIBU. Na baada ya hapo Haitakuwa shwari kamwe. God Bless Us All

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 02, 2012

    Nyinyi watanganyika kwani bila Zanzibar hamuendi ? acheni kujizalilisha nyinyi mna kila kitu si muendelee tu na muwaachie na wazanzibar na zanzibar yao. Nashangaa kuona wazanzibar walio kidogo kila siku wanasema hawataki Muungano ila nyinyi Mlio mamilioni bado hamjamiani ata kuitamka tanganyika mnaona aibu vinywani mwenu.Inashangaza sana dah? Waswahili husema kimfaacho mtu chake kuweni faghari na tanganyika yenu .

    ReplyDelete
  24. AnonymousJune 02, 2012

    Ona namna watu wabara walivyokuwa na akili finyu. kwanza Sheikh Farid asili yake si mwarabu kabisa, ulizeni muambiwe asili ya mababu zake. Pili hao wanaosema wazanzibari kuhimili vita kumbukeni zanzibar tumepata mapinduzi hatukupewa uhuru wa kwenye karatasi kama tanganyika.

    ReplyDelete
  25. AnonymousJune 02, 2012

    HUYO MWARABU ARUDI KWAO OMANI.

    NA WAZANZIBAR WALIOKO TANGANYIKA WARUDI KWAO ZANZIBAR TUONE NANI WATAATHIRIKA ZAIDI. UJINGA MTUPU TU HUO.

    ReplyDelete
  26. AnonymousJune 02, 2012

    daa huyo mwarabu sio kabsa...njia wanayotumia si nzuri japo intention ni nzuri la msingi ni kutumia njia zakibusara bila kuathiri vbaya wengine....lasiivyo hawatafka wanapopataka

    ReplyDelete
  27. AnonymousJune 02, 2012

    sheikh safi sana mpaka kieleweke wanachoma wao CCM makanisa halafu wanatusingizia sisi ili kutuziba kauli zetu tusitete nchi yetu wapi wameula wa chuya this time.

    watanganyika wa kiislamu tungeni mkono sisi ndugu zenu toka zamani tulikuwa tuna amani yetu na tukishi kwa wema na ihsan na upendo mkubwa na ndugu zetu wa kikiristo iweje leo hii watuite wazamiaji,tunaokumbatia waarabu wana jua fika UISLAMU WETU NDO NGUVU YETU NA WANATAKA KUUUWAA LAKINI HAWATOWEZE INSHALLAH

    FANYENI MTAKAVYO FANYA AT THE END OF THE DAY MUNGU MWENYE MILKI YOTE NA UFALME WOTE ATATUPA NCHI YETU AMIN

    ReplyDelete
  28. AnonymousJune 03, 2012

    mimi nasubiri tu vita vya wazenji na watanganyika halafu nione nani mshindi lkn duuh nyinyi warabu sitaki mpigane manaa hapo zanzibari sio kwenu fanyeni mrudi kwenu mkapigane na marekani mnangangania kwani africa ni kwenu? shame on you mlivo tesa waafrica kuwafanya watumwa sasa nasema hivi rudini makwenu mkauze mafuta halafu mlalie vitanda vya zahabu. mbona hamsikii hiyo zanzibari niya waafrica sio ya warabu. omani ni kubwa sana kajengeni huko bado nafasi zipo tena kuna bahari sio mchezo

    ReplyDelete
  29. AnonymousJune 03, 2012

    SIO WAZANZIBAR WOTE WASIOTAKA MUUNGANO WENGINE TUNAUTAKA NA KUPENDA MUUNGANO MSITUJUMUISHE KWENYE MAKUNDI YENU YA FUJO NYIE MTAKUWA WALE WA KISIWA CHA PILI TU, RUDINI BASI MKACHUME KARAFUU MTAWALIWE NA WARABU MTUWACHIE UNGUJA YETU KWA AMANI

    ReplyDelete
  30. AnonymousJune 04, 2012

    wewe wa mwisho si dhani kama kweli mzanzibari wewe,na wa kisiwa cha pili ndo ndugu zetu wa kufa na kufaana na kupona na tumechanganyka nao so siju unasema nini hapa.wewe si mzanzibari wewe ungekuwa kweli mzanzibari ungejua uchungu wa ndugu, jamaa zako wewe.
    nenda huko huko baraa ukaishi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...