Mmoja wa Makuli wa kupakia mifuko ya Saruji kwenye malori kutoka kiwanda cha saruji,Wazo jijini Dar akiwa ameuchapa usingizi mzito nyuma ya lori hilo lililokuwa linatembea katika barabara ya Sam Nujoma,Jijini Dar.Ulalaji wa namna hii ni hatari sana kwa maisha yake kwani linaweza tokea lolote kwake,japo hatuombei litokee.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 18, 2012

    poa tu raha jipe mwenyewe au unataka alale kwenye mashangingi? kwani yeye mbunge?

    huyo ni masikini mtaji nguvu zake ana raha gani ya kuishi? waache hao wabunge wale maisha na mafisadi lakini kina sisi hata tukifa hatuna neno.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 18, 2012

    Pole Bwana kaka na msukosuko wa wimbi la maisha!

    Hapa ndio yale mazingira Kibarua kinakuwa ni cha kufukuzia, huku ukipata inakuwa ni zamu za usiku tu hadi asubuhi!

    Kwa mtaji huo sio ndio haya ya kulala juu ya gari tena?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 18, 2012

    Duhhh jamani kiumbe wa Mwenyezi Mungu anateseka na mshike mshike wa maisha Duniani!

    1.Hapo ndoto zake ktk usingizi huo juu ya Lori anaota ameshafariki yupo ndani ya kaburi!

    2.Kama akiota yupo hai anaota anaanguka kutoka juu ya pango kwenda bondeni!

    3.Kama akiota ana afadhali yupo ktk ndoto akiwa ktk kazi ngumu kama kubeba zege kwa kuwa yupo juu ya mavumbi ya simenti!

    4.Akiota anajuta, atakuwa anajuta kwa nini hakuzaliwa Mbunge au Fisadi?

    5.Akiota anakula, ni kuwa anakula mavumbi na mawe kwa vumbi la simenti linavyomwingia puani!

    Ndio maana Bob Marley aliimba,,,
    ''So much trouble in the world X 3''

    Ahhh maisha ya namna hii yana raha gani tena?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 18, 2012

    1.Kukosa usingizi sawasawa,
    2.Kazi ngumu na ya suluba,
    3.Dishi la kubabaisha,

    Kulingana na aina ya kazi kama hii maisha yake yanazidi kuwa mafupi kwa miaka zaidi ya 10 hivi!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 19, 2012

    Wasi wasi wako tuu mbona hamna shida hapo jamaa yupo makini kuliko unavyofikiria.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...