Mabalozi wa Afrika Kusini Mh. Henry Chiliza (kushoto) na Mh. Ibrahim Mukiibi wa Uganda wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania wakisalimiana baada ya kukutana katika zoezi la kujitolea kufanya kazi za kijamii katika shule ya msingi Tandale ya jijini Dar es Salaam. Kulia ni Joymrey Von de Merwe.
Wafanyakazi wa UN na Ubalozi wa Afrika Kusini wakishirikiana kubeba madawati kwa ajili ya kufanyiwa ukarabati.
Pichani Juu na Chini ni Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Tandale jijini Dar Hamisi Kubiga (kushoto) sambamba na Balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania Mh. Henry Chiliza wakihakikisha ukarabati wa madawati unakwenda sawa.
Balozi wa Afrika Kusini nchini Mh. Henry Chiliza akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo katika shule ya Msingi ya Tandale ambapo amesisitiza siku hii ya Kimataifa ya Mandela inaadhimishwa kwa kufanya shughuli za kijamii kwa kuwa Mzee Mandela mwenyewe alikuwa akijitolea muda wake mwingi kusaidia watoto, kufanya shughuli za kijamii, kutetea haki za watoto na wanyonge.
Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tandale Bi. Lucy Mwakibete (katikati) akitoa shukrani kwa UN na Ubalozi wa Afrika Kusini nchini ambapo ameelezea changamoto mbalimbali zinazoikabili shule zikiwemo Uhaba wa Madawati, Vyoo, Ubovu wa Sakafu za Vyumba vya Madarasa na kuwaomba wadau kujitokeza kuwasaidia ili kuboresha mazingira mazuri kwa wanafunzi wa shule hiyo ili kuongeza kiwango cha ufaulu.
http://www.canadahelps.org/GivingPages/GivingPage.aspx?gpID=17276
ReplyDeleteKettles Cares for Africa
Dear friends and family,
Thank you for visiting my donation page. Through the Canada-Africa Community Health Alliance (CACHA), I will be going on a Medical Mission to Ukerewe, Tanzinia Africa this coming October 2012.
I cannot wait to work with Doctors, Surgeons, Pharmacists, Nurses as part of logistics and pharmacy aid, serving 400-600 people a day.This is an opportunity of a lifetime for me to be able to help the people and make a difference. Your donation helps thousands!
Thank you
Correction: Ntate Madiba is 67 years old now. Happy Birthday Mandela. I dont count those 27 years they robbed you!
ReplyDelete