Kwa niaba ya wana-Diaspora wote wanaoishi nchini Canada, Kamati Tendaji ya Zanzibar – Canadian Diaspora Association (ZACADIA) inachukuwa fursa hii kutoa salamu za pole kwa wale wote waliopatwa na maafa wakiwa katika meli iliyozama. Japokuwa tupo mbali na nyumbani lakini roho zetu zipo pamoja nawafiwa wote na majeruhi katika msiba huu mkubwa uliyoikumba nchi yetu.

ZACADIA inawapa mkono wa pole wale wote waliopoteza watoto, ndugu na jamaa zao, na kuwataka wawe na subra kwani hiyo ni miongoni mwa mitihani ya ALLAAH (SW). Tunawatakia afya njema wale wote walionusurika na ajali hiyo.

Mola awalaze mahala pema peponi na awape maghfira waliotangulia katika ajali hii - AMIN!

Katibu

ZACADIA

Toronto, Canada.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 22, 2012

    Tuko pamoja katika kutoa pole. Mpendwa Nova Scotia

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...