Msajili wa Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki,Dk John Ruhangisa akifafanua jambo wakati akitangaza mpango wa mahakama hiyo kufungua masijala ndogo katika nchi za Rwanda,Burundi,Kenya,Uganda na Tanzania leo

  ======  ========  =======
Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki(EACJ)imeanzisha Masijala  ndogokatika nchi wanachama ili kuwawezesha wananchi na taasisi zenye lengo la kufungua kesi kwenye mahakama hiyo kufanya hivyo katika nchi zao.

Msajili wa Mahakama hiyo,Dk John Ruhangisa amesema kuwa hatua hiyo ni muhimu sana na ambayo imekuwa ikisubiliwa kwa hamu na wananchi ambao wamekuwa hawawezi  kufika yalipo makao makuu ya mahakama hiyo mjini Arusha.

Amesema  uzinduzi wa Masijala ndogo ya kwanza ya EACJ utafanyika Kigali nchini Rwanda wakati wa utoaji tuzo kwa waandishi bora wa habari zinazohusu jumuiya hiyo.Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni  Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi. Mbali na hilo pia Mahakama hiyo iko mbioni kusajili kesi kwa njia ya mtandao kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia kukua kila siku na mahakama hiyo kuona ukuhimu wa kwenda na wakati

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ahsante Dr.John Ruhangisa,

    Hapa ndio tutakuwa chini ya mwamvuli kamili wa haki ktk maamuzi ya Mahakama.

    Ahsante Shirikisho la Afrika ya Mashariki.

    Mungu Ibariki Tanzania!
    Mungu Ibariki Afrika ya Mashariki!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...