Msajili wa Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki,Dk John Ruhangisa akifafanua jambo wakati akitangaza mpango wa mahakama hiyo kufungua masijala ndogo katika nchi za Rwanda,Burundi,Kenya,Uganda na Tanzania leo
====== ======== =======
====== ======== =======
Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki(EACJ)imeanzisha Masijala ndogokatika nchi wanachama ili kuwawezesha wananchi na taasisi zenye lengo la kufungua kesi kwenye mahakama hiyo kufanya hivyo katika nchi zao.
Msajili wa Mahakama hiyo,Dk John Ruhangisa amesema kuwa hatua hiyo ni muhimu sana na ambayo imekuwa ikisubiliwa kwa hamu na wananchi ambao wamekuwa hawawezi kufika yalipo makao makuu ya mahakama hiyo mjini Arusha.
Amesema uzinduzi wa Masijala ndogo ya kwanza ya EACJ utafanyika Kigali nchini Rwanda wakati wa utoaji tuzo kwa waandishi bora wa habari zinazohusu jumuiya hiyo.Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi. Mbali na hilo pia Mahakama hiyo iko mbioni kusajili kesi kwa njia ya mtandao kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia kukua kila siku na mahakama hiyo kuona ukuhimu wa kwenda na wakati
Msajili wa Mahakama hiyo,Dk John Ruhangisa amesema kuwa hatua hiyo ni muhimu sana na ambayo imekuwa ikisubiliwa kwa hamu na wananchi ambao wamekuwa hawawezi kufika yalipo makao makuu ya mahakama hiyo mjini Arusha.
Amesema uzinduzi wa Masijala ndogo ya kwanza ya EACJ utafanyika Kigali nchini Rwanda wakati wa utoaji tuzo kwa waandishi bora wa habari zinazohusu jumuiya hiyo.Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi. Mbali na hilo pia Mahakama hiyo iko mbioni kusajili kesi kwa njia ya mtandao kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia kukua kila siku na mahakama hiyo kuona ukuhimu wa kwenda na wakati



Ahsante Dr.John Ruhangisa,
ReplyDeleteHapa ndio tutakuwa chini ya mwamvuli kamili wa haki ktk maamuzi ya Mahakama.
Ahsante Shirikisho la Afrika ya Mashariki.
Mungu Ibariki Tanzania!
Mungu Ibariki Afrika ya Mashariki!