Heshima yako Ankal
Asante nimeona umeweka comment yangu kuhusu upigaji kura.Kuna tatizo bado kwenye upigaji kura,kama unaweza wasiliana na wizara,waandae maajabu kama 10 hivi yaliyoko Tanzania wavipublish.Itasaidia sana kwa wapiga kura-wapelekee hii email.Walishatngaza lakini nadhani maelezo zaidi yanahitajika katika kupiga kura,angalia eti na Mlima Kenya unakuja kwa kasi..Wenzetu wanapiga kura.
Kwanini?:Kwa sababu upigaji wa kura ni mgumu kidogo,wanakulazimisha utaje vivutio Saba(7) vilivyoko Tanzania-Siyo kwamba unafika na kutick Kilimanjaro,Serengeti, ngorongoro.Halafu ukishavitaja unavituma kwa email kwa mtiririko wa Umaarufu wake, hapo kura yako itahesabika
Ugumu:Siyo wengi wanayafahamu maajabu haya,hata mimi nilipata taabu kidogo kutafuta maajabu ya Tanzania tofauti na hiyo Kilimanjaro,Migration na Ngorongoro Crater!.Kuna Mbeya meteorite(Kimondo),Manyara hotsprings,Kabila la waHadzabe nilitaja(sina uhakika kama ni maajabu),Simba wanaopanda miti kule mbuga za Wanyama.
Mungu ibariki Tanzania
David V
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...