Ndugu wanahabari,
 Karibuni katika mkutano mfupi ambao unalenga kuzungumzia  ama kuelezea masikitiko makubwa dhidi ya Kocha wa Timu ya Yanga TOM SAINTFIET  (pichani) aliyoyatoa kwa vyombo vya habari kuidhalilisha hoteli  yangu   juu ya huduma zake na kiwango chake alichokiita cha huduma mbovu!.
 Kimsingi management ya  Peter safari’s Hotel na Uongozi wa chama cha wamiliki wa Mahotel Mkoa wa Mbeya, tumesoma na kusikiliza kwa masikitiko makubwa lawama zilizotolewa na Kocha huyo kuwa “hajawahi kulala kwenye hoteli ya hadhi ya chini kama hii  katika nchi 20 alizowahi kufanya kazi katika nchi za Afrika”.
Uongozi wa hotel  na chama cha wamiliki wa hotel kwa ujumla kinachukulia suala hili kama kampeni maalumu ya kudhalilisha na kukatisha tamaa wateja kuiona mbeya haina hotel za hadhi za kuishi timu na watu wenye hadhi katika jamii, kitu ambacho si kweli na ni visingizio kutokana kushindwa kwake kuwezesha timu kufikia matarajio  ya mashabiki na wapenzi wa timu hiyo.
 Kimsingi viongozi wa Timu ya yanga waliomba kuwalaza wachezaji wawili katika kitanda kimoja tofauti na taratibu za hotel na hii ilitokana na mipangilio yao hasa kwenye suala la uwezo wa kulipia kila mchezaji chumba chake, aidha, uongozi wa hotel ulijitahidi kwa kadri ya uwezo wake kuhakikisha kuwa wachezaji wanapata huduma walizohitaji na hata wakati mwingine kutoa usafiri kwaajili ya kununua mahitaji ya familia zao kitu ambacho hakifanyiki maeneo mengine kwa gharama za hotel.
 Kwa kutambua madhara yaliyotokana na matamshi ya kocha huyo raia wa Ubelgiji, Uongozi wa hotel ya Peter Safaris  unayaona matamshi haya kama udhalilishaji mkubwa  na wenye nia mbaya ya kuuharibia mkoa wa mbeya  na kuutangaza vibaya kwa wageni  juu ya uwezo wake katika utoaji wa  huduma za hoteli.
 Aidha  kwakuwa maneno ya kocha huyo  yametamkwa na kutangazwa kwenye vyombo vya habari pasipo kukanushwa na viongozi wa Timu ya Yanga ambao ndiyo waliofanya maandalizi na kufanya mazungumzo ya maombi  ya kuwalaza wachezaji wawili katika vyumba ambavyo vina uwezo wa kulaza mtu mmoja (single), Peter safaris inaliona jambo hilo kama ni sehemu ya kashfa iliyojengwa kwa nia ya kuiharibia hotel biashara  na kuipotezea hadhi mbele ya wageni  na watumiaji wa huduma za PETER SAFARIS  ambayo inaendelea kupanua huduma zake kwa mkoa wa mbeya na maeneo mengine.
 Ikumbukwe kuwa Peter safaris hotels imekuwa ikipokea wageni wa hadhi mbalimbali wakiwemo viongozi wa ngazi za kitaifa, wageni kutoka nje wa hadhi za juu na wafanyabiashara wakubwa, hivyo ugeni wa Yanga na hadhi inayozungumzwa na Kocha huyo hauwezi kufikia mahala pa kuidhalilisha hotel kwa kiwango hicho ambacho kocha huyo amevitumia vyombo vya habari licha ya hotel kutopata maoni yoyote baada ya timu  kuhudumiwa   kwenye sanduku la maoni(suggestion box).
 Kutokana na hali hii iliyojitokeza, uongozi wa Hotel unautaka uongozi wa Yanga kuiomba radhi management ya Hotel ya Peter safaris kwa lugha ya kashfa na isiyoendana na utamaduni wa Mtanzania kwakuzingatia kuwa wachezaji wakiulizwa namna walivyohudumiwa wasingeweza kuzungumza hayo ambayo mwalimu wao ameyazungumza kwa utashi wake.
 PETER SAFAR’s inalichukulia jambo hili kwa uzito unaostahili kwakuzingatia kuwa  lugha iliyotolewa na mteja wake huyo imevuka kiwango cha kuvumilika, na njia pekee ambayo tunadhani ni ya uungwana kabla ya kuingia kwenye taratibu za kisheria ni kuwataka YANGA kuomba radhi kwa lugha ya dharau na kashfa dhidi ya hotel yetu vinginevyo tunakusudia kuchua hatua za kisheria kwa kuzingatia kuwa hotel inaendeleshwa kwa mujibu wa taratibu na sheria zinazotawala huduma za hotel na zile za mipango miji  ambazo masuala ya usafi ni miongoni mwa maeneo muhimu ya kukidhi viwango vya uendeshaji wake.
Nawasilisha
MKURUGENZI  MTENDAJI
PETER SAFARI’s HOTEL
MBEYA.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 21 mpaka sasa

  1. weka picha ya hiyo hoteli tuone. weka vyuma, toilets, restaurants na menu zenu... sisi ndio tuamue

    ReplyDelete
  2. Sasa kama ni kweli asiseme?

    ReplyDelete
  3. Duu wachezaji wawili tena wanaume kitanda kimoja, ndiyo maanda Yanga hawakushinda..... Kimaadili ya kitanzania hotel iliruhusu vipi watu wawili wa njisia mmoja kulala kitanda kimoja? au hotel Peter Safari's hamna wateja tokana na huduma nzenu mbaya ndiyo mukawarundika wachezaji wa Yanga?

    ReplyDelete
  4. ama hakika mie naungana na uongozi wa hoteli hiyo kwa kukanusha vikali uongo huo wa kocha huyo. Hoteli hiyo ni nzuri, na ina huduma zote muhimu ambazo mtu wa hadhi ya wachezaji wa Yanga anastahili kuzipata. Mie mwenyewe nilikuwa na wageni wangu wa hadhi ya standard, ambao walifikia pale kwa muda wa wiki tatu, nisisikie malalamiko yoyote toka kwao, maana kama kungekuwa na mapungufu, lazima wangetaka niwahamishie pengine. Isitoshe, walirudi siku nyingine na kukaa palepale.

    Huyu bwana wa kizungu anataka hoteli ya hadhi gani?Nyota tano? Hatuna hoteli hiyo huku Mbeya, lakini tuna hoteli ambazo zinaweza kutunza watu wa standard ya juu, wakaishi comfortably.

    Huyu kocha asitake kuleta visingizio vya kipuuzi, ili ku-justify kushindwa kwake kuifunga Prisons
    -Embe Kidusu

    ReplyDelete
  5. NI WAZI KABISA HIYO HOTEL INAENDESHWA SI KWA MISINGI YA KIBIASHARA, CRITIQUES KUTOKA KWA WATEJA NDIO CHANGAMOTO ZA KUBORESHA HUDUMA ZENU. MSICHUKULIE COMMENTS MSIZOZIPEDA KUWA NI KUBOMOA BIASHARA. BADILIKENI KUBALINI KUKOSOLEWA ILI KUONGEZA UBORA WA HUDUMA KWA WATEJA.

    ReplyDelete
  6. Hotel inayofuata taratibu na sheria hailazi watu wawili kwenye single room, huo ndo udahifu wenu wa kwanza. Mgekataa biashara na yanga kama kweli mnafuata sheria lakini kitendo cha kulaza watu wawili room ya mtu mmoja inaonyesha pia ni likely mkaenda kinyume na standard za huduma.

    ReplyDelete
  7. sasa kwa nini mlishusha standard zenu kwa kukubali kuweka watu wawili? that is the cost!!swallow it!!

    ReplyDelete
  8. Interesting.

    wengine hapa hatujui alichokisema huyo kocha ninini, lakini ni wazi ana huyo kocha ana exposure kwa hiyo kuna nafasi kubwa ya kumuamini kuliko mkurugenzi mtendaji wa Peters safari hotel ambaye tunamjua tu kwa maandishi yake hapo ambayo msomoje yeyote makini ataona kwamba yuko defensive so hana credibility, for example ana defend hoteli lakini anaongelea lugha iliyotumika haiendani na utamaduni wa kitanzania? wewe ni mfanyabiashara kama wateja hawajaridhika lazima waseme. Tafuta hotel inspector BBC uone wamiliki wa hoteli wenzio wanavyopigwa vijembe wazi wazi and they learn.

    Badala ya kuomba kuobwa radhi nafikili mngemuomba huyo bwana awaeleze ninini alitegemea kupata kizuri ambacho hakikuwepo, basi mnajifunza kutoka hapo kama anaongea pumba mnamwambia.

    culture za kitanzania za
    kuambiana kwa kumbelezana inabidi ziishe kikolo, imbombo kamagi.

    ReplyDelete
  9. Huyu bwana Embe Kidusu hapo juu nahisi si mtu wa kiwango na nahisi hata wageni wake si wa kiwango cha kuchukulia mfano. Kama hiyo hoteli ingekuwa ya hali ya kiwango kinachokubalika, basi isingeruhusu watu wawili wa jinsia moja walale kitanda kimoja. Kwa kukubali tu ina maana ni hoteli ya kiwango duni. Hata hao wageni wako ni wa kiwango cha kulazwa wawili katika kitanda kimoja ndio maana hawakulalamika. Kwani ukileta mtu aliyezoea kulala katika tembe unadhani atalalamika. Angalia hadhi ya wageni wako ndio uwafanye kama reference

    ReplyDelete
  10. Kuna mameno mitaani kwamba kocha hakuoga hadi anakwenda kwenye gemu!!! Je, hii nayo ni kweli? Je, chumba alicholala kocha kina hadhi ya kimataifa?

    ReplyDelete
  11. Kuna mameno mitaani kwamba kocha hakuoga hadi anakwenda kwenye gemu! Je, hii nayo ni kweli? Je, chumba alicholala kocha kina hadhi ya kimataifa?

    ReplyDelete
  12. hampendi kuambiwa ukweli, hata mimi nilishalala hapo huduma si za kuridhisha kwa kweli, wabongo tumezoea kusifiwa tu, badilikeni non sense , kama mtu hakuridhika asiseme? ilikuwa inabidi mumumulize wapi mlipokosea , sasa nyie mnakuja juu, na tena ndio mzungu ndio kabisaaaaaa mnatumia muda kusema mnazalilishwa loh. Aibu toeni hapa malalamiko yenu, mkaongee naye mwenyewe, aombe radhi aibu aibu loh. Customer Service zero inavyoonekana, ingekuwa nzuri msingekuja kuweka humu grow up, business ni ushindani. Mteja ni mfalme

    ReplyDelete
  13. Mmejishitaki wenyewe kwa kuvunja sheria na kuwalaza watu mzungu wa-nne. Sasa Polisi watawabebena kama senene, kila siku ka-elfu hamsini na ushehe ili mambo yasifike mbali.

    ReplyDelete
  14. A customer is always right. The only way to prove critics wrong is to transform their negative views into positive by improving services when necessary. Also it is completely unprofessional to assign two unrelated adults a single hotel room. It may be legal in your jurisdiction, but it sounds weird in civilized world. Please feel free to fact-check my comments with other hotel professionals worldwide and try to get better.

    ReplyDelete
  15. Hii mikwara ya kushitakiana walianza watu wa siasa na sasa imeingia kwa huyu jamaa.

    Mtu mwenye kushitaki kweli haongei na vyombo vya habari, anachukua hatua.

    Ignorant

    ReplyDelete
  16. WENYE HOTELI ACHENI USHAMBA. MNALETA PROPAGANDA ZA KISIASA ILI MTETEE HOTELI YENU WATEJA WASIKIMBIE. TUMESHAJUA KUWA HOTELI YENU IMECHOKA NI HOTELI UCHWARA IBORESHENI.
    MSILAUMU KOCHA WALA UONGOZI WA YANGA NYIE NDIO WAROHO WA PESA, KAMA MLIONA VYUMBA HAITOSHI MNGEKATAA KUWA NAFASI HAITOSHI.

    MNAPENDA SIFA WAKATI PERFORMANCE NI SIFURI. KATIKA MAZINGIRA KAMA HAYA KAMWE HAMTABORESHA HOTELI YENU MAANA HAMKUBALI MAPUNGUFU YENU. UJINGA MTUPU.

    SIE WENGINE TULIKUWA HATUJI KINACHOENDELEA ILA UBISHI WENU NA MANAZIDI KUJIHARIBIA. ENDELEENI TU NA KUTANGAZA UOZO WENU MTAONA WATEJA WATAKAVYOPUNGUA

    ETI MNAJITETEA MLITOA HADI USAFIRI WA KUWAPELEKA WACHEZAJI SOKONI KUNUNUA MAHITAJI YA FAMILIA ZAO. KWA HIYO HICHO NDIO KIPIMO SAHIHI CHA UBORA WA HOTELI?

    ReplyDelete
  17. HOJA AU POINTI PEKEE INAYOONEKANA HAPO NA AMBAYO WANAITUMIA KUTETEA HOTELI YAO NI USAFILI WA WACHEZAJI KWENDA SOKINI BASI. HAKUNA JINGINE.
    HII INAONYESHA JINSI GANI WATU WANATAKA SIFA KWA LAZIMA.
    UKILALA HIYO HOTELI INABIDI USIFIE TU HAKUNA KUKOSOA.

    ReplyDelete
  18. Mimi nafikiri imefika wakati kwa watanzania hasa wafanyabiashara kutambua umuhimu wa MTEJA. Na kwamba HAKUNA MTEJA MZURI kushinda MTEJA ALIYE TAYARI KUKUKOSOA. Tuache tabia ya KUJITETEA pasipo MSINGI wowote. Katika karne hii, ni muhimu biashara zikawakumbatia wakosoaji maana WANATUTAKIA MEMA. Tusiwe wale watu tunaojali faida za muda mfupi kwa kigezo cha kuogopa kuchafuliwa..eti tunaaribiwa biashara...TUKUMBUKE KUWA NI WATEJA WACHACHE SANA walio tayari KUTOA MAONI BILA UNAFIKI. JAMBO LINGINE LA MSINGI SANA..KWA NINI MNATABIA YA KUPINDISHA SERA/POLICY ZENU? Kwa kifupi KITENDO CHENU CHA KURUHUSU WACHEZAJI KULALA WAWILI NDICHO KINAWAONGEZEA KASHFA. UONGOZI LAWAMA NI ZENU na KATU MTEJA HALAUMIWI; SIKILIZENI ALICHOWAAMBIA MTEJA..REKEBISHENI KWA MANUFAA ya HOTELI YENU na WAKAZI wa MBEYA...AIBU SANA

    ReplyDelete

  19. 1. Mteja ni mfalme
    2. Usafiri wa bure kwenda na kurudi "mall" hiyo ni standard kwenye hoteli yoyote ya ' kimataifa.
    3. Nyinyi wenyewe ndio aw kulaumiwa kwa kukubali ku check in midume miwili on same room same bed!!!

    4. KAMA HOTELI LAZIMA MKUBALI KUKOSOLEWA NA NDIO MAANA KUNA "SUGGESTION BOXES" yaani masanduku ya maoni.
    Huyo mtu ni lazima amekwishakaa kwenye mahoteli tofauti ndio maana amefikia kusema hivyo.

    ReplyDelete
  20. Hili ndio tatizo letu Watanzania, pale mtu mwenye uelewa na upeo peke anapotoa comments kuhusu mapungufu/ubovu wa kitu fulani huwa anaonekana ni mtu adui!

    Mimi ningefurahishwa na uongozi wa mahoteli mjini Mbeya kama ungeliyafanyia kazi maelezo yaliyotewa na bwana Saintfiet kwa kuboresha huduma katika mahoteli yao na si kusema kwamba aliyoyasema si sahihi!

    Mimi mwenyewe msafiri karibu katika mikoa yote hapa Tanzania, lakini kuna baadhi ya mikoa tena mingi tu ikiwa ni pamoja na Mbeya huwa naboreka sana na huduma zao za kihoteli, sembuse mtu kutoka bara Ulaya?!

    ....tubadilike jamani!!!

    ReplyDelete
  21. Hotel hii kweli si ya hadhi na maneno aliyosema kocha ni ya kweli. Tanzania customer service ni sifuri huduma mbovu mkiambiwa mnaanza kukanusha kama hivi. Biashara inatakiwa uchukue hii changamoto na kuirekebisha sio kuanza mambo ya siasa ya propagana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...