Kwanza kabisa napenda kutoa shukurani zangu kwa wizara sabab shule zimeongezeka na hasa kwa vijijini na mijini hii imefanya jamii ya watanzania wengi kwenda shule hata kama ajafanya vizuri kwenye masomo lakini wamejifunza kuishi na watu na mambo mengi iliyoko kwenye jamii.

Kusudi langu kubwa hasa ni, Kuhusu mitihani ya Taifa kweli hasa kuanzia ile mitihani ya kidato cha 4 na cha 6. Oja yangu ni kuhusu mtu anapoumwa ghafla akalazwa au mwingine akachanganyikiwa na hawezi kabisa kufanya mtihani akashindwa kutokana na hali yanayokuwa nayo kwa wakati ule.

Mimi kama mwanajamii na mzazi nilikuwa naomba kipengele kinachosema hata kama mwanafunzi anaumwa afanye mtihani naomba kibadilishwe. Iwe endapo mwanafunzi ameumwa gafula na daktari  akathibitisha, naomba asifanye mtihani bali ahirishe na  afanye mwaka unaokuja kuliko kufanya wakati yuko kwenye hali mbaya na matokeo yakaja ameshindwa na wakati hajaumwa alikuwa na maendeleo ya kuweza kufanya vizuri alikuwa nao.

Naomba Wizara kushirikiana na Baraza la Mitihani la Taifa waliangalie hili manaake mtoto amesoma miaka 4 au 6 inapofikia hatua kwa bahati mbaya akaumwa gafula na jinsi karo inavyoumiza katika masomo tunaomba wabadilishe hiyo sheria make mambo yakusema afanye matokeo yakitoka vibaya arudie kama mtahiniwa wa kujitegemea naona hiyo haiamsaidi mwanafunzi kama huyo.

Naomba kuwasilisha
MDAU WA ELIMU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...