Leo Tarehe 21.11.2012 imetimia miaka
miwili (2) tangu utuache hapa Duniani Mama
Mary Mwingira. Maisha yetu sisi wanao, mama yako, wakwe , wajukuu, wadogo,wifi,
wapwa, majirani, ndugu na marafiki zako wote yamebadilika na si kama ulivyokuwa nasi.
Tunakukumbuka na
kuukosa upendo, ucheshi na uchapakazi na moyo wa kutokata tamaa uliokuwa nao.
Umekuwa chachu ya maisha yetu na msaada mkubwa kwetu sote. Mungu alikuongoza
kwa yote hadi kukujalia kifo chema
ukiwa katika imani thabiti.
Mapenzi yake MUNGU Baba yatizwe kwani ndiye aliyetupa zawadi ya
wewe kuwa mwanetu, mama yetu, bibi, dada, shangazi, mkwe, wifi shemeji, rafiki na jirani yetu mpendwa.
Tunaahidi kuendelea kukuenzi daima kwa somo kuu lako la upendo usio na masharti.
Ulale salama mama yetu! Nasi
tunakuombea kwa Mungu akupokee mbinguni ambako tunaamini umefika. Uendelee
kutuombea sisi wanao na ndugu wote ulituacha hapa duniani.Tunakupenda sana mama
na kamwe hatutasahau mapenzi yako kwetu.
Machozi ni mengi machoni mwetu na
hayapimiki kamwe.
Tunashukuru kwa mafunzo ambayo yamezaa baraka na mafanikio
tele. Ulikuwa hupendi kuona tunasononeka na tunaamini hadi sasa hupendi kutuona
tukisoneneka hivyo tunasherehekea maisha yako matakatifu na tunasema, Asante
MUNGU kwa zawadi hii kubwa ya kuwa watoto
na ndugu zako..Umetuonyesha mfano wa kuigwa nasi wamama,wanawake na
watu wengine wote mama Mwingira..
Tunakupenda na kuta kuenzi daima Milele
na milele!!!
Kutakuwa na Misa
za kumuombea Mama Mary Mwinngira katika kanisa kuu la Mtakatifu Joseph’s tarehe 21 /11/2012 . Ratiba ni kama ifuatavyo:
Saa 12 .45 asubuhi, Saa 7 mchana na jioni ya 11 jioni. Pia Bethania
House-Upanga saa 6:30 asubuhi Siku hiyo hiyo.
Misa hizi zitaendelea kwa wiki hii yote yani tar 22 - 25 Novemba katika
makanisa hayo na kila Jumapili St Gasper, Kunduchi misa ya 2(saa 1 kamili
asubuhi).KARIBUNI SANA!!
Raha ya milele Umpe Eee Bwana,na
Mwanga milele Umuangazie...Mary John
Mwingira astarehe kwa AMANI..
AMEN


.png)
Rest in peace mum,am relieved i have seen your picture,its bitter sweet feelings for me....i just wish you were here and see the woman i become.... am sure you have been my guardian angel,i will keep you in prayers and close to my heart....
ReplyDelete