Naibu Waziri wa Fedha   Mhe. Saada Salum akifungua mkutano wa Taasisi ya Maendeleo ya Kiuchumi na Mipango ya Afrika- IDEP. Tanzania ni mjumbe wa Bodi ya Magavana katika taasisi hii ambayo hujishughulisha na utoaji wa mafunzo ya kitaalam kwa wataalam wa serikali za nchi za Kiafrika. 

Wajumbe wengine katika Bodi ya Magavana ni pamoja na Misri, Kenya, Nijeria na Zimbambwe. IDEPambayo makao yake makuu yapo nchini Senegal ni moja ya Taasisi za Umoja wa Mataifa na  inatimiza miaka 50 tangu kuanzishwa kwake. 

Hivyo, kupitia IDEP watanzania wanaweza wakanufaika na program mbalimbali za mafunzo zinazotolewa au kudhaminiwa na taasisi hii. Kwa taarifa zaidi tembelea katika website ya IDEP: http://www.unidep.org/ .Kozi za kipaumbele zinazotolewa au kuratibiwa na IDEP ni masuala ya kiuchumi, Mipango, Maendeleo ya Nishati ya gesi, uranium na masuala ya usimamizi wa mikataba
  Prof. Humphrey Mushi  Kushoto na Prof. Mutahaba wa USDM wakifutatilia mijadala pamoja na wataalam wengine.
 Naibu Waziri wa Fedha   Mhe. Saada Salum akiongea na wanahabari wa Senegal

1.    Mhe. Naibu waziri (katikati) akibadilishana mawazo na Prof. Mushi  kulia na Prof. Mutahaba (kushoto) wakati wa mapumziko ya mkutano huo  mjini Dakar,  Senegal. Picha na Thomas M.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...